Raia Fulani
JF-Expert Member
- Mar 12, 2009
- 10,876
- 2,744
Kuna kauli za baadhi ya watu maarufu hapa nchini zinaleta kizunguzungu cha mawazo. Najua zitakuwa nyingi ukichanganya na za wale wasio maarufu. Kauli kama 'u were born on the wrong part of the world' ambazo zinamaanisha hiyo wrong part ni bongo. Kauli hii imetolewa na madam Rita wakati flani pamoja na salama jana kwenye BSS. Hivi wazungu wanaposikia kauli kama hizi wanatuchukuliaje. Kauli kama hizi ndio zimemnyima mbati na ntepa ushindi. Kama kazaliwa kuzimu ambako si kwake si aondoke? Angeenda kushiriki pop idol USA! Tusijidharau kiasi hiki. Nini kinaifanya tz au afrika kuwa wrong part of the world? Si ajabu hata hawa watalii tunaowaona kwa wingi wao huwa wanavutiwa na kauli kama hizo kuja kuona. Wrong part. Tubadilike