Kauli za Marekani kuilenga Huawei ni mbinu ya ushindani wa kibiashara

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,000
1,019
Fadhili Mpunji

VCG31N1228026874.jpg

Hivi karibuni naibu waziri wa mambo ya nje wa Marekani Bibi Wendy Sherman aliyekuwa ziarani nchini Angola, alisema Angola na nchi nyingine za Afrika kutumia vifaa vya kampuni ya Tehama ya China HUAWEI, ni kuhatarisha usalama wa nchi. Kauli hiyo aliyotoa Bibi Sherman baada ya kutembelea kampuni ya Africell ya Angola inayoungwa mkono na serikali ya Marekani, ni mwendelezo wa hatua za Marekani kujaribu kuzuia maendeleo ya kampuni ya Huawei katika sehemu mbalimbali duniani.

Ushirikiano kati ya kampuni ya Huawei na nchi za Afrika umekuwepo kwa muda mrefu hata kabla ya mivutano kati ya kampuni hiyo na serikali ya Marekani, na maendeleo ya kasi ya sekta ya Tehama yaliyopatikana barani Afrika, yanahusiana moja kwa moja na ushirikiano kati ya kampuni ya Huawei na nchi za Afrika. Takwimu zilizotolewa mwaka jana na kituo cha Afrika cha Baraza la Atlantiki (Atlantic Council’s African Center), zinaonesha kuwa katika kipindi cha miongo miwili iliyopita, kampuni ya Huawei imejenga asilimia 50 ya mtandao wa 3G, na asilimia 70 ya mtandao wa 4G.

Pamoja na kuwa alichokisema Bibi Sherman nchini Angola si kitu kipya, iwe ni kwa China wala kwa nchi za Afrika, ukweli ni kuwa kimezusha maswali mapya. Kwa yeye kutoa kauli hiyo wakati anatembelea kampuni ya Africell yenye uhusiano na Marekani na inayotoa huduma kama kampuni ya Huawei, ni kama njia ya kupigia debe kampuni ya Africell iwe na nafasi nzuri kibiashara barani Afrika.

Tukiangalia mwenendo wa matumizi ya vifaa vya Tehama katika miongo miwili iliyopita barani Afrika, iwe ni vile kutoka China au kutoka nchi za magharibi hatuwezi kuona kile anachokisema Bibi Sherman, kinachoonekana ni kinyume. Kama ni kweli kampuni ya Huawei inahatarisha uhuru wa nchi za Afrika, bila shaka uhuru huo ungekuwa umepotea katika kipindi hicho cha miongo miwili iliyopita. Duniani inatambua kuwa ongezeko la matumizi ya Tehama katika nchi za Afrika, limeongeza uhuru wa aina mbalimbali (freedoms) kama ule wa kujieleza na kutoa maoni, hali ambayo ilikuwa ngumu kabla ya hapo.

Undani wa kauli ya Bibi Sherman ni changamoto zinazoyakabili makampuni ya Marekani kwenye kuwekeza kwenye sekta ya Tehama barani Afrika, na katika sehemu nyingine duniani. Hii inatokana na Afrika si vipaumbele kwenye sera za Marekani, huwa inakumbukwa tu kama inaonekana kuwa kuna dalili za makazi ya watu wanaoleta tishio kwa usalama wa Marekani. Hata kwenye upande wa uwekezaji, watoa fedha wa Marekani (mabenki) wanaona Afrika ni sehemu yenye hatari. China haiitazami Afrika kwa jicho hilo, kwa hiyo inawezekana kuwa sababu kubwa ya makampuni ya Marekani kuwa nyuma kwenye ushindani na makampuni ya China inatokana na mtazamo hasi wa Marekani kwa Afrika.

Mtafiti mwandamizi wa mambo ya China na Afrika katika Taasisi ya washauri bingwa ya mambo ya kimataifa ya Afrika Kusini (SAIIA) Bw. Cobus Van Staden, amewahi kusema kinachoifanya Kampuni ya Huawei na makampuni mengine ya China kuwa mbele kwenye ushindani na makampuni ya nchi za magharibi barani Afrika, ni fursa ya makampuni ya China kupata fedha kutoka kwenye mabenki ya China yenye kufadhili uwekezaji katika nchi za nje, na sera endelevu za serikali ya China kuunga mkono uwekezaji wa China barani Afrika. Hali hii kwa Marekani ni tofauti, sera ya Marekani kwa Afrika si endelevu inategemea kiongozi aliye madarakani au chama kilicho madarakani.

Mara nyingi viongozi wa Afrika wamekuwa wakisema Afrika inavutia uwekezaji kutoka kwa nchi zote. Watakaoitikia mwito huo na kwenda kuwekeza barani Afrika kwa kufuata sheria na kutohatarisha usalama, bila shaka watakaribishwa. Hii ndio maana kampuni ya Hauwei imeweza kushirikiana na nchi nyingi za Afrika.
 
Ngoja waendelee kuwabip akina Jack Chain mvua ya komfuu na karate ikinyesha tujue wapi panapovuja.

Nukuu ya JPM "vita ya kiuchumi si lelemama" inabidi uwe ngangari haswa
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom