Kauli za kuwaita mawaziri wapumbavu ama nonsense zitafutwa na Katiba Mpya

Hata katiba mpya ikiwepo mawaziri wataburuzwa na kutukanwa tu. Ni masuala ya kibinadamu zaidi.
Hoja yangu ni kwamba umungu mtu wa rais ukipunguzwa waziri atakuwa huru kutumia utashi wake wa kujiuzulu ama kubakia ktk nafasi yake endapo patatokea misigano kati yake na rais.

Lkn kwasasa wanogopa kushughulikiwa
 
Hivi kumbe bila Sukari maisha yanakuwa hatarini. Kweli mwanadamu na mazoea. Najua hata siku kukosekane Majani ya chai kutachimbika
 
Kutukana au kutoa lugha kali mtu anapoghafilika ipo sana tu kwa watu wengi, hata huyo waziri huenda huwa anawakaripia watendaji wa chini yake, sasa kwa rais inakuwaje ajabu kutoa lugha kali endapo kuna jambo limefanyika kinyume na alivyotarajia.........hata mwalimu Nyerere alikuwa anachukizwa balaa hadi unaona sura inabadilika, Mkapa hivyo hivyo, kikwete na Magu, labda mzee ruksa ndo ulikuwa huoni akionyesha sura ya ukali au kuongea lugha kali.......kwa hiyo leteni jingine, siyo kukomaa na jambo ambalo halina mashiko yoyote.​
 
Muwage mnacomment kwa kuchuja habari kwanza.

Chukua hotuba ya waziri Mkenda inayozungumzia masuala ya mashamba ya miwa, viwanda vya sukari, uhaba wa sukari na utaratibu wa uagizwaji na uingizwaji wa sukari.

Ukitoka kuisikiliza hiyo, chukua hotuba ya rais Samia aliyoitoa Chato wakati wa ziara ya rais M7, utaelewa dhahiri mtoa mada alichomaanisha.

Tukichukulia sura ya rais na baraza lake la mawaziri ni mfano wa familia moja ya ndoa, mtu na mke wake kiutendaji.

Hatutegemei mke wa mtu azungumze jambo, halafu baadaye atoke mumewe hadharani kuliponda ama kulikanusha jambo hilo!

Majirani tutashangaa na kuona dosari iliyo wazi katika familia hiyo!

Haiwezekani jambo moja linalopikwa katika chumba kimoja likatoka na maelezo tofauti ya msigano!

Kwa mantiki ya mfano nilioutoa ni kwamba waziri hawezi kukurupuka kutoa msimamo wa serikali bila baraka za rais, never on earth!

Ikitokea msigano wa wazi hivyo, yampasa waziri kujitathimini na kubwaga manyanga ili kulinda hadhi yake!


Sent using Jamii Forums mobile app
Ndiyo hajabwaga manyanga sasa unafanyaje?
 
Kimsingi nchi yetu kwa sasa imejaa chuki za aina mbili

1. Za kisisa. Kwasabb waliopo madarakani hawakuchaguliwa na wananchi. Na sisa zinendeshwa kwa figisu
2. Za kiuchumi. Kwasabb mifumo ya masoko na ajira inavurugwa na wakubwa. Wao wanajipendelea na hawajali wengine
Point kubwa sana umeongea
 
Ndiyo hajabwaga manyanga sasa unafanyaje?
Mtoa mada kalisemea hilo.

Kubwaga manyanga kwa siasa za Tz, kwa watawala inatafsiriwa kuwa ni kiburi na majigambo na si kuwajibika kisiasa na mifano ipo.

Angalia wale wazee makada wa sisiem waliojiondoa kwenda upinzani walichukuliwaje?

Utatengenezewa zengwe wewe hadi basi bila sababu za msingi!

Ndiyo maana wateule wote pamoja na yote ya udhalilishaji wa kinyadhifa wanaofanyiwa, hawaondoki wanamuangalia mteuzi wao atakavyoamua!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Katiba yetu inampa Rais mamlaka makubwa sana nchi hii. Rais ni kama Mungu kwa mujibu wa katiba yetu.

Mawaziri wanatwezwa lkn hawana cha kufanya. Wakijuzulu "mungu" anaweza kutafsiri hatua hii kama dharau na kuamua kuwashughulikia. Wanalazimika kuipokea kauli ya "mungu mtu" kwa mikono miwili.

Rais Magufuli aliwaita mawaziri Dr. Philip Mpango na Prof. Kabudi WAPUMBAVU mbele ya hadhara. Wakapokea kauli hii kwa mikono miwili. Sote tukabakia tumeduwaa. Ni kwasababu hawakuwa na la kufanya mawaziri hawa. Walimwogopa "mungu" na malaika wake

Rais Samia ametamka hadharani kwamba uamuzi wa Prof. Mkenda kuzuia sukari toka nje ni NONSENSE. Sote tumebaki tumepigwa na butwaa. Hana la kufanya Prof. huyu akirogwa kujiuzulu "Mungu" ama malaika wake watamshughulikia.

Tuiangalie upya Katiba yetu inayomjenga mtu kuwa "Mungu".
Ninachojua kuanzia awamu ya 5, tumeshuhudia unyumbu kwenye uongozi serikalini, 'herding behaviour', Herding behaviour is an occurrence of thoughtful people suspending their individual reasoning because of fear, in this case fearing their leaders
 
Back
Top Bottom