Kauli za kisiasa zilizowahi kuwaudhi sana Watanzania

Watanzania

JF-Expert Member
Jul 7, 2009
727
42
Katika kutafakari hali ya siaza za Tanzania nimekumbuka baadhi ya kauli za kisiasa zilizowahi kuwaudhi sana Watanzania. Kauli hizi zinawaelezaje wahusika? Na ili kuweka mambo sawa hebu tujaze mazingira na mwaka wa kauli hizi.

1. Kila mtu ataubeba msalaba wake mwenyewe- Cleopa Msuya akiwa waziri wa fedha wakati wa kikao cha bunge la bajeti mwaka 1989

2. Hata ikibidi watanzania kula nyasi ndege ya rais itanunuliwa - Mramba akiwa waziri wa fedha, mwaka.......

3. Watanzania wana wivu wa kike- Benjamin Mkapa akiwa Rais, mwaka.....


4. Watanzania wavivu wa kufikiri- Rais Benjamin Mkapa akiwa Rais, Mwaka..


5. Kelele za mpita njia hazimnyimi mwenye nyumba usingizi, Rais Kikwete, Mwaka...


6. Atakayegombea na Kikwete atakufa ghafla, Sheikh Yahaya Hussein, akiwa anapiga ramli Channel Ten, Mwaka.....


Baada ya kuziweka kumbukumbu vizuri tujiulize, hivi kauli zao hao wahusika zinawaeleza vipi?. Kwa maoni yangu kauli 1 na 2 zinawaeleza mawaziri wa fedha kama watu wasiokuwa na huruma. Kauli zingine zinawaelezaje wengine?
 
Give mwaw my mashine gun. How many rounds does it habe?....ok..ok, it is enough.
 
Sidhani kaa kuna aliyeudhika na hizo kauli. Maana nijuavyo bongo kila kitu tambarare.
 
3. Watanzania wana wivu wa kike- Benjamin Mkapa akiwa Rais,
mwaka.....................

Kama kumbukumbu zangu ziko sahihi.....nafikiri hiyo statement inafanana na ile iliyotolewa na Mh Pius Msekwa..........

7. "You can Go to Hell"........JS Malecela alipokuwa Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi.........
 
Kama kumbukumbu zangu ziko sahihi.....nafikiri hiyo statement inafanana na ile iliyotolewa na Mh Pius Msekwa..........

7. "You can Go to Hell"........JS Malecela alipokuwa Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi.........

Lakini ni kipi cha ajabu ?

Tumekubali mfumo unaruhusu hawa genge la watawala watutawale ktk mfumo 'fimbo ya chuma' na tumewapa 'blank cheque' ya kuchagua lililo jema kwa niaba yetu bila kutuuliza. Sasa kama ni makosa ni yetu sote kama waTz kwa leniency, indecision & lack of daring.
 
"Wale wote wanaosema Tanzania Railways Corporation inatoa huduma mbaya can go to hell"--John Samuel Malecela alipokuwa Waziri wa Usafirishaji na Mawasiliano mwaka 1980. Kauli ilimgharimu akakosa ubunge. Hiyo nina ushahidi iliwaudhi Watanzania wengi. Hizo hapo juu sina ushahidi
 
Watanzania wana wivu wa kike- Benjamin Mkapa akiwa Rais,
mwaka.....

Alikuwa ni Pius Msekwa , Spika wa Bunge, aliposhauriwa aachane uwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi wa kampuni ya Vodacom, Ili kukwepa mgongano wa maslahi kutokana na cheo chake cha Uspika!!
 
"UKITAKA biashara zako ziende vizuri basi jiunge na CCM, chagueni mafiga matatu ili muweze kupata maendeleo, mkichagua upinzani hatutaleta maendeleo."

Nadhani mnamjua aliyesema hayo, kama haumjui soma HAPA
 
“UKITAKA biashara zako ziende vizuri basi jiunge na CCM, chagueni mafiga matatu ili muweze kupata maendeleo, mkichagua upinzani hatutaleta maendeleo.”

Nadhani mnamjua aliyesema hayo, kama haumjui soma HAPA

Lakini ni lipi la kushangaa ikiwa wafanyabiashara hufadhili kampeni za wanasiasa na wanasiasa in return wana-scratch migongo ya wafanyabiashara ktk obvious transactions za kuuza nchi?

Kipi kipya? Semeni!
 
Katika kutafakari hali ya siaza za Tanzania nimekumbuka baadhi ya kauli za kisiasa zilizowahi kuwaudhi sana Watanzania. Kauli hizi zinawaelezaje wahusika? Na ili kuweka mambo sawa hebu tujaze mazingira na mwaka wa kauli hizi.

1. Kila mtu ataubeba msalaba wake mwenyewe- Cleopa Msuya akiwa
waziri wa fedha wakati wa kikao cha bunge la bajeti mwaka 1989

2. Hata ikibidi watanzania kula nyasi ndege ya rais itanunuliwa-
Mramba akiwa waziri wa fedha, mwaka.......

3. Watanzania wana wivu wa kike- Benjamin Mkapa akiwa Rais,
mwaka.....

4. Watanzania wavivu wa kufikiri- Rais Benjamin Mkapa akiwa
Rais, Mwaka..

5. Kelele za mpita njia hazimnyimi mwenye nyumba usingizi, Rais
Kikwete, Mwaka...

6. Atakayegombea na Kikwete atakufa ghafla, Sheh Yahaya
Hussein, akiwa anapiga ramli Channel Ten, Mwaka.....

Baada ya kuziweka kumbukumbu vizuri tujiulize, hivi kauli zao hao wahusika zinawaeleza vipi?. Kwa maoni yangu kauli 1 na 2 zinawaeleza mawaziri wa fedha kama watu wasiokuwa na huruma. Kauli zingine zinawaelezaje wengine?
....na kauli nyingine iliyochefua ni pale dala dala za Dar zilipotishia kugoma, Mramba akiwa waziri wa fedha alisema "Wananchi watembee kwa miguu kutoka makwao kwenda vibaruani"

Ilituchefua sana hasa sisi wakazi wa Mbagala.
 
"mtake msitake huyu atakua rais" Julius Kambarage Nyerere alitamka maneno hayo mwaka 1995 huku akiinua bango la benjamin william mkapa, mkoani kilimanjaro..mjini moshi na uwanja mzima kila mtu akiwa ameinua mkono juu ukiwa na alma ya v ambayo ilikua alama ya chadema na nccr mageuzi...........alitupa bango chini kwa hasira na kuondoka kwenye mkutano........sitasahu siku ile nilikua mita chache kutoka alipokua mwalimu alikasirika na wananchi walifurahi
 
Katika kutafakari hali ya siaza za Tanzania nimekumbuka baadhi ya kauli za kisiasa zilizowahi kuwaudhi sana Watanzania. Kauli hizi zinawaelezaje wahusika? Na ili kuweka mambo sawa hebu tujaze mazingira na mwaka wa kauli hizi.

1. Kila mtu ataubeba msalaba wake mwenyewe- Cleopa Msuya akiwa
waziri wa fedha wakati wa kikao cha bunge la bajeti mwaka 1989

2. Hata ikibidi watanzania kula nyasi ndege ya rais itanunuliwa-
Mramba akiwa waziri wa fedha, mwaka.......

3. Watanzania wana wivu wa kike- Benjamin Mkapa akiwa Rais,
mwaka.....

4. Watanzania wavivu wa kufikiri- Rais Benjamin Mkapa akiwa
Rais, Mwaka..

5. Kelele za mpita njia hazimnyimi mwenye nyumba usingizi, Rais
Kikwete, Mwaka...

6. Atakayegombea na Kikwete atakufa ghafla, Sheh Yahaya
Hussein, akiwa anapiga ramli Channel Ten, Mwaka.....

Baada ya kuziweka kumbukumbu vizuri tujiulize, hivi kauli zao hao wahusika zinawaeleza vipi?. Kwa maoni yangu kauli 1 na 2 zinawaeleza mawaziri wa fedha kama watu wasiokuwa na huruma. Kauli zingine zinawaelezaje wengine?
Zinawaeleza kama wamelewa fedha za hazina
 
"Wale wote wanaosema Tanzania Railways Corporation inatoa huduma mbaya can go to hell"--John Samuel Malecela alipokuwa Waziri wa Usafirishaji na Mawasiliano mwaka 1980. Kauli ilimgharimu akakosa ubunge. Hiyo nina ushahidi iliwaudhi Watanzania wengi. Hizo hapo juu sina ushahidi

Vizuri umeongeza nyingine na kuweka jina la mtu, cheo chake na mwaka, na kauli hiyo ilimpa zawadi gani. Tuendelee kujaza sehemu zilizobaki wazi katika kauli zingine ili kukamilisha kumbukumbu ya kauli hizo mbaya. Ni sehemu ya historia yetu watanzania
 
"mtake msitake huyu atakua rais" Julius Kambarage Nyerere alitamka maneno hayo mwaka 1995 huku akiinua bango la benjamin william mkapa, mkoani kilimanjaro..mjini moshi na uwanja mzima kila mtu akiwa ameinua mkono juu ukiwa na alma ya v ambayo ilikua alama ya chadema na nccr mageuzi...........alitupa bango chini kwa hasira na kuondoka kwenye mkutano........sitasahu siku ile nilikua mita chache kutoka alipokua mwalimu alikasirika na wananchi walifurahi
Hii nayo ni kumbukumbu katika historia ya nchi yetu lakini naona umesema watanzania walifurahi, lakini hapa tunataka kuandika historia ya kauli mbaya ambazo wananchi waliudhika sana
 
- Eti jamani zipo evidence za ku-back up hizi claims, kwamba wananchi waliudhika? Yaani hawa wananchi hawakuudhika kuibiwa hela zao katika IPTL, Radar, na Richimonduli, lakini waliudhishwa na kauli tu! Labda ndio maana tupo hapa tulipo! taifa la majungu majungu viongozi mpaka wananchi ni majungu majungu,

- Ninakumbuka majungu Zitto anatembea na barua ya kujiuzulu mpaka leo bado yupo Chadema, ndio taifa letu majungu majungu tu na uongo uongo!

- Vipi evidence?

Respect.


FMEs!
 
Wajanja woe wapo Dar es Salaam....ya Zito Kabwe.So huku Kigoma na mikoa mingine kuna watu wa aina gani??jibu Kinyume na wajanja.Mafa**
 
....na kauli nyingine iliyochefua ni pale dala dala za Dar zilipotishia kugoma, Mramba akiwa waziri wa fedha alisema "Wananchi watembee kwa miguu kutoka makwao kwenda vibaruani"
Ilituchefua sana hasa sisi wakazi wa Mbagala.

Loo, huyu Mramba naona amekubuhu kwa kauli mbaya, na tena akiwa waziri wa fedha, sasa tumalizie ilikuwa mwaka gani?
 
"Wale wote wanaosema Tanzania Railways Corporation inatoa huduma mbaya can go to hell"--John Samuel Malecela alipokuwa Waziri wa Usafirishaji na Mawasiliano mwaka 1980. Kauli ilimgharimu akakosa ubunge. Hiyo nina ushahidi iliwaudhi Watanzania wengi. Hizo hapo juu sina ushahidi

- Mkuu Zakayo, hii kauli Malecela aliitolea wapi?

Respect.


FMEs!
 
Back
Top Bottom