kauli za ccm ndio zinaweza kuvunja amani nchini tanzania

GHIBUU

JF-Expert Member
Jan 13, 2011
4,432
3,006
Nimekuwa nikifatilia mijadala ju ya vyama vya siasa,nimeona kuwa chadema kimekuwa na upinzani mkubwa nchini tanzania,kitendo cha chadema kupita katika majimbo na kuwaelewesha wananchi jinsi ya serikali ya tanzania chini ya ccm wanavyoiyendesha ovyoo serikali hio kwa kutmia pesa za umma na za watoa jasho katika mikataba mibovu.

Kwa kweli kitondo hichi kwa chadema kuwaelewesha wananchi sio kama ni inaleta madhara au italeta madhara kwa nchi nzima bali ni wajibu wao kuwaeleza wananchi kama ni viongozi na wameteuliwa na wananchi wao.

Nimesikitishwa sana na viongozi wa ccm waliomo ndani ya serikali kutumia vitisho kwa kutamka kuwa watatumia nguvu za dola kuinyamazisha chadema ili wa stop ziara zao na mikotano na maandamano kwa kisingizo cha kuwa wanaweza kuharibu hali ya hewa nchini.

Kwa kweli tanzania inahitaji uwongozi mpya katika serikali hii kwa sabau,maisha yamekuwa magumu,matatizo kama umeme maji,elimu,afya,yamekuwa sugu nchi hii pamoja na ajira,nimeshangawazwa sana kuona rais akitamka kuwa matatizo haya yapo toka nyerere na hayatamaliza,dah hivi nusu karne sasa kweli tushindwe kuayamaliza ?

Mi naona ni mfumo mbovu kabisa,nchi za ulaya tatizo la maji na umeme,na living standard waliyashayamaliza zamani sana,inatokezea matatizo kama ajira kutoka na mzunguko wa pesa tu,lakini tanzania leo hii kila unachokijua wewe bado ni tatizo sugu kwa nini ?

Viongozi acheni kutmumia lugha za kuharibu hali ya hewa nchini na badala yake fanyeni muezalo ili mumalize matatizo haya sugu,serikiali sio masikini kabisa ,tuna rasilimali nyingi tu,kona pesa za watoa jasho,zote zinaenda wapi ?

Kama barabara misaada tunapokea kama,elimu tunapokea ,afya tunapokea,jee pesa za rasilimali zinaenda wapi ?
 
.....wenyewe hawalitambui hilo ndo maana wanaendelea kuropoka badala ya kushughulikiwa mambo ambayo wenzao wanawayapigia kelele kwamba yashughulikiwe!!!!
 
Back
Top Bottom