Wana jamvi habari?
Jana bungeni mwanasheria mkuu wa serikali mhe. Werema alitoa kauli yenye utata ya kuwa "....kazi ya kichwa si kuotesha nywele tu, ni pamoja na kufikiri...." kauli hii inakuja mda mfupi baada mhe. Lisu, mnadhimu mkuu wa kambi rasmi ya upinzani bungeni kuomba idhini kwa spika kutoa hoja ya kuahirisha shughuli zilizopangwa ktk order paper ili kujadili ajali ya Mv Skagit.
Kuna swali la kujiuliza! Werema analenga kufikisha ujumbe wake wapi na kwa nani na kwa lengo gani?
Majibu ya swali hili ni mengi.
1. Yawezekana anamlenga mhe. Lisu, na wapinzani wote kuwa mbunge huyu (na wenzie) hawezi kufikiri ingawa ana kichwa na nywele, kuwa anatumia kichwa chake vibaya hakitumii kufikiri bali kufugia nywele!
2. Yawezekana alimlenga mnadhimu mkuu wa serikali mhe. Lukuvi (na wabunge wote wa chama tawala) kuwa hawatumii vichwa vyao kufikiri na kuona ni hoja gani iletwe bungeni badala yake wanatumia vichwa vyao kufugia nywele na kuwaachia wapinzani wanaleta hoja nzito kama hizo bungeni na kujiongezea umaarufu, pengine....
3. Yawezekana alimlenga N/spika, na viongozi wenzake ndani ya bunge kuwa anaongoza kiti kinachohitaji mtu anaejua kufikiri na sio kufuga nywele! na kwa udhaifu huo huo N/S anashindwa kuona ni tusi na dharau kwake badala yake anamshabikia na kusema kauli yake haina tatizo!
4. Na pengine bwana mkubwa huyu alikuwa anajizungumzia yeye mwenyewe akilenga kumfikishia ujumbe boss wake aliyemteua kuwa nafasi yake inahitaji mtu anayetumia kichwa chake kufikiri sio kufuga nywele kama afanyavyo yeye.
Kwa kuwa hakupata muda wa kulifafanua hili nje au ndani ya bunge, sisi tusiokuwa na nywele ambao kazi ya vichwa vyetu ni moja tu kufikiri! tunaendelea kufikiri!
Unaweza kuongezea majibu yako hapa!
Jana bungeni mwanasheria mkuu wa serikali mhe. Werema alitoa kauli yenye utata ya kuwa "....kazi ya kichwa si kuotesha nywele tu, ni pamoja na kufikiri...." kauli hii inakuja mda mfupi baada mhe. Lisu, mnadhimu mkuu wa kambi rasmi ya upinzani bungeni kuomba idhini kwa spika kutoa hoja ya kuahirisha shughuli zilizopangwa ktk order paper ili kujadili ajali ya Mv Skagit.
Kuna swali la kujiuliza! Werema analenga kufikisha ujumbe wake wapi na kwa nani na kwa lengo gani?
Majibu ya swali hili ni mengi.
1. Yawezekana anamlenga mhe. Lisu, na wapinzani wote kuwa mbunge huyu (na wenzie) hawezi kufikiri ingawa ana kichwa na nywele, kuwa anatumia kichwa chake vibaya hakitumii kufikiri bali kufugia nywele!
2. Yawezekana alimlenga mnadhimu mkuu wa serikali mhe. Lukuvi (na wabunge wote wa chama tawala) kuwa hawatumii vichwa vyao kufikiri na kuona ni hoja gani iletwe bungeni badala yake wanatumia vichwa vyao kufugia nywele na kuwaachia wapinzani wanaleta hoja nzito kama hizo bungeni na kujiongezea umaarufu, pengine....
3. Yawezekana alimlenga N/spika, na viongozi wenzake ndani ya bunge kuwa anaongoza kiti kinachohitaji mtu anaejua kufikiri na sio kufuga nywele! na kwa udhaifu huo huo N/S anashindwa kuona ni tusi na dharau kwake badala yake anamshabikia na kusema kauli yake haina tatizo!
4. Na pengine bwana mkubwa huyu alikuwa anajizungumzia yeye mwenyewe akilenga kumfikishia ujumbe boss wake aliyemteua kuwa nafasi yake inahitaji mtu anayetumia kichwa chake kufikiri sio kufuga nywele kama afanyavyo yeye.
Kwa kuwa hakupata muda wa kulifafanua hili nje au ndani ya bunge, sisi tusiokuwa na nywele ambao kazi ya vichwa vyetu ni moja tu kufikiri! tunaendelea kufikiri!
Unaweza kuongezea majibu yako hapa!