Kauli ya Waziri Mkuu kutilia shaka barakoa za kisasa na kutaka watu wajishonee matambara na kuyavaa usoni haiwezi kuachwa bila kujadiliwa

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,641
218,085
Nchi yenye wasomi wengi kama Tanzania haiwezi kunyamazia kauli ya Mh Majaliwa ya ku ignore barakoa zilizotumiwa na madaktari wetu miaka nenda rudi kuwalinda na maambukizi ya magonjwa wanapowahudumia Watanzania kwenye hospitali za umma na nyinginezo.

Hii ni kwa sababu wenye mamlaka ya kuhakiki ubora wa bidhaa zinazotoka nje ya nchi ni serikali yenyewe , leo Waziri Mkuu anapoanza kutilia shaka bidhaa ambazo zinapitishwa na mamlaka anazozisimamia na kulipiwa kodi, tena zilizotengenezwa kwa viwango vya WHO na wakati huo huo akaanza ku promote barakoa za "Dengrizi" zisizo na viwango vyovyote, zilizoshonwa na fundi cherehani wa Buza kwa Mpalange ambaye hata VETA hakupita , inahitajika Maombi mazito sana kwa ajili ya nchi hii .

Nawaomba wasomi na wataalam (hasa wa afya) mtuthibitishie bila uoga kama kweli barakoa za " Climplin au chilimeni ama dengrizi " zinaweza kuwa na ubora kuliko barakoa zinazotengenezwa kwa viwango vinavyoelekezwa na WHO.

Naomba kuwasilisha.
 
waziri Yuko sahihi,kipindi Cha mapambano lazma kujihami katika mazingira yote yenye kutiliwa shaka.lakini pia inshu sio upendeze unapozivaa balakoa,muhimu ni kujikinga.hakuna sababu ya kuongeza pato la taifa kwa nchi za nje kwa kuagiza balakoa,wakati tunauwezo wa kuzitengeneza hapahapa kwa vitenge vyetu,na vitambaa vyetu.tuache ujinga wa kubeza vya kwetu.
 
waziri Yuko sahihi,kipindi Cha mapambano lazma kujihami katika mazingira yote yenye kutiliwa shaka.lakini pia inshu sio upendeze unapozivaa balakoa,muhimu ni kujikinga.hakuna sababu ya kuongeza pato la taifa kwa nchi za nje kwa kuagiza balakoa,wakati tunauwezo wa kuzitengeneza hapahapa kwa vitenge vyetu,na vitambaa vyetu.tuache ujinga wa kubeza vya kwetu.
Mapambano na nani?

Na hapa ndio shida kubwa ilipo. Mnaacha kumtambua adui yenu corona mnalazimisha uadui na mtu mwingine ambae kimsingi nae anapambana na huyo huyo adui yako corona.
 
waziri Yuko sahihi,kipindi Cha mapambano lazma kujihami katika mazingira yote yenye kutiliwa shaka.lakini pia inshu sio upendeze unapozivaa balakoa,muhimu ni kujikinga.hakuna sababu ya kuongeza pato la taifa kwa nchi za nje kwa kuagiza balakoa,wakati tunauwezo wa kuzitengeneza hapahapa kwa vitenge vyetu,na vitambaa vyetu.tuache ujinga wa kubeza vya kwetu.
Kwa akili yako ya kushikiwa, unafikilia mask, ni kitambaa tu kama cha gagulo?!!hizo mask zenyewe zinatofautiana, ubora kutegemea na ufanyaji kazi, hayo ya vitambaa labda kuzuia vumbi, zito, eti VIRUS uizuie na kitambaa cha gagulo???sema wanawapa matumaini hewa watu, ili wajione wako salama, kwani mask zenye viwango wengi hawaziwezi kutokana na gharama!!
 
PM amejaribu Ujinga ama ni mjinga..!!! kwani ana Elimu gani au Phd yake ni ya nini!?

Dah..!! Tunapitia wakati mgumu kama Taifa
emoji25.png
emoji25.png
 
Hata hvyo tatizo kubwa la hii nchi ni Elimu na poor exposure...watu wameishia la saba na degree za kuunga unga , wanaamin uganga wa kienyeji out of scientific solution.

karbia wote wanacheza Ngoma moja kama majuha.. from high command to the bottom ni disaster ..hata kama ugonjwa wameuleta wao still hao hao ndo wanajua namna ya kuukabili sio wewe mpiga tunguli.

wenye ndugu wazee na umri umeenda jiandaeni kuzika wengine next week...shame on you Tanzania
 
Mapambano na nani?

Na hapa ndio shida kubwa ilipo. Mnaacha kumtambua adui yenu corona mnalazimisha uadui na mtu mwingine ambae kimsingi nae anapambana na huyo huyo adui yako corona.
adui ni korona,sote tunakubaliana.ktk kupambana na hii kitu lazma tuweke mazingira ya tahadhari na kujihami,ktk kila Hali yenye kutiliwa mashaka.
 
Hata hvyo tatizo kubwa la hii nchi ni Elimu na poor exposure...watu wameishia la saba na degree za kuunga unga , wanaamin uganga wa kienyeji out of scientific solution.. karbia wote wanacheza Ngoma moja kama majuha.. from high command to the bottom ni disaster ..hata kama ugonjwa wameuleta wao still hao hao ndo wanajua namna ya kuukabili sio wewe mpiga tunguli...wenye ndugu wazee na umri umeenda jiandaeni kuzika wengine next week...shame on you Tanzania
poor minded thoughts. umesoma lakini elimu yako iko kwa makaratasi ubongoni empty!! Ndio maana unaamini wao ndo wanajua namna ya kuudhibiti... Such brain ,ni hasara kubwa.
 
Kwa akili yako ya kushikiwa, unafikilia mask, ni kitambaa tu kama cha gagulo?!!hizo mask zenyewe zinatofautiana, ubora kutegemea na ufanyaji kazi, hayo ya vitambaa labda kuzuia vumbi, zito, eti VIRUS uizuie na kitambaa cha gagulo???sema wanawapa matumaini hewa watu, ili wajione wako salama, kwani mask zenye viwango wengi hawaziwezi kutokana na gharama!!
at least ww umeongea fact.nakubaliana na ww zina quality na quality in reflex na aina ya matumizi/mahali inakwenda tumika.hata hao wazungu mnaowaamini kuliko hata nafsi zenu,wanajua balakoa haiwez Kinga pasee,ni Kama angalau kupunguza risk,ikiwa ni hivyo si ni heri tushone hizo gagulo unazosema kuliko kupoteza pesa nje,wakati hiyo maski ya wanzungu+hizo gagulo zote hazizuii Bali kupunguza risk?
 
Back
Top Bottom