Kauli ya vitu kupanda bei kisa vita ya Ukraine inapindishwa na walioielewa wanafunga mikanda kimyakimya

Kwa nini serikali haijatoa stimulus package kama mataifa mengine wanavyofanya, mishahara kwa wafanyakazi imeendelea kuwa kiduchu miaka nenda rudi huku hali ya maisha ikiendelea kupaa kwa kasi......wanachoweza kufanya ni kukamua tozo kutoka kwa wanyonge.
 
Imenibidi kwa mara nyingine nijiridhishe kwa kurejelea kusikilizwa hotuba ya Mhe.Rais iliyokuwa inazungumzia kupanda bei kwa vitu kunakosababishwa na vita vya Ukraine na Russia na mapokeo ya kauli hiyo.

Sio kwamba nimetumia muda kusikilizwa tena sikusikia vizuri ila nilifanya hivyo kuongeza uelewa binafsi na kujiridhisha nia ya kutolewa kauli ile. Je, haikupaswa kutolewa au ingetolewaje?

Alichifanya Mhe. Rais ni kuweka kumbukumbu sawa kwa wanaoelewa na wataamua kupotosha na wasiolewa kabisa. Watanzania tuna tabia ya kusahau, kesho Mbowe au Lissu akipanda jukwaani na kudai Serikali imeamua kwa makusudi kupandisha bei ya vitu si wote watakaokumbuka kulikuwa na vita na moja ya madhara ya vita ile ilisababisha vitu kupanda. Watu watakuwa wamesahau na hiyo itakuwa ni agenda na wengi wanaolalamika wanalalamika agenda hiyo kuzimwa.

Ukweli ulio mchungu ambao wanaoujua hawataki watu waujue kwa sababu mbalimbali zikiwemo za kisiasa ni kwamba Tanzania ni 'importer' na bidhaa nyingi tumeagiza kutoka nje ambako ni watumiaji wakubwa wa mafuta na gesi ya Urusi katika uzalishaji na kwa sababu ya vita inayoendelea upatikanaji wa mafuta na gesi umekuwa wa kusuasua kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo:
i) vikwazo
ii) usalama
iii) malipo kutokubalika kwa mfumo uliozoelewa, n.k.
Tutajadili siku nyingine juu ya mambo mpaka kupelekea kuadimika kwa mafuta na gesi.

Hivyo, hata kama mafuta na gesi tunayotumia hayotoki Urusi lakini kwa sababu tunategemea bidhaa zinazozalishwa kwa gesi na mafuta ya Urusi basi kuathirika kwa doko kwao kutaathiri soko zima la nchi tegemezi.

Mfumo wa soko( market system) bei inategemea hali ya uhitaji na upatikanaji wa malighafi na vingine vingi. Tukitumia kanuni ya 'demand na supply' kupanda kwa bei ya mafuta na bidhaa nyingine zinazotegemea au kutumia mafuta kwa nchi yetu pia haiepukiki.

Ni ukweli usiopingika vitu vitapanda bei kutokana na kupanda bei katika soko la dunia sehemu ambayo Rais Samia hawezi kuzuia zaidi ya kuacha kanuni ya soko kufanya kazi.

Katika mazingira haya Serikali inatakiwa kudhibiti upandaji wa bei kiholela upandaji usiozingatia misingi ya kanuni ya soko lakini kusema itaweza kuzuia vitu kupanda bei ni kudanganywa wenyewe. Wanaoratibu bei ya soko ndio wameathiriwa na mfumuko wa bei ,kwa hiyo tutegemee bei Tanzania ibaki ileile?

Nampongeza Mhe.Rais kuwa muwazi na zaidi katuweka tayari kufunga mikanda dunia inapoelekea janga jingine la kiuchumi baada ya Corona kuonekana sio tishio tena.

Tumsaidieni Mhe.Rais kuusema ukweli huu, kwenye vita ya uchumi hatakiwi kupambana mwenyewe. Mwisho napenda kunukuu maneno ya Biblia yanayosema"Watu wataijua kweli nayo kweli itawaweka huru kwelikweli" na ninukuu pia msema wa kiswahili unaosema "mficha maradhi kifo humuumbua"
mafuta ya kula ya alizeti inayolimwa hapo Singidae yamepanda kutoka sh. 5000/6000kwa lita hadi sh. 9500kwa lita ndani ya wiki 2.

Utaambiwa Kisa vita ya Ukraine. Tena anayekwambia Ni Rais wa nchi. Tz shamba la bibi limerudi kwa kasi sana.
 
Hali ni mbaya sana, bidhaa zinzidi kupanda bei, gharama za usafiishaji bidhaa kuleta nchini pia zinazidi kupanda, ila kipato hakipandi kabisa.
 
Wakati yeye ndio anazidi kuhamasisha vitu vizidi kupanda bei. Anawakumbusha wafanya biashara wafanye hivyo.
 
Forest of words desert of points,mbolea imepanda kabla ata mawazo ya rusia na ukraine kutabiri kuwa watapigana yani kiufupi mbolea ilipanda siku magufuli wanamzika chato ,week moja baada ya mazishi ya jpm ngano tulinunua 1300 ikapanda mpaka 2000 pkg.
 
Wajinga wengi walizoea serikali laghai na ya kuongea uongo kama ya Magufuli.
We ndo mjinga number moja unayekaa kwa shemeji yako hujui ata bei mahitaji ta hapo nyumbani ya kila siku ni yalikuwa ni shilingi ngapi na leo shilingi ngapi.huo uongo wa magufuli unauonea wapi wakati ni maisha tunayoyaishi.!?
 
Maneno marefuuuu kama mnazi! Tunachotaka ni kwamba SSH ana mpango katika kutoa nafuu kwa wananchi kama vile kuweka subsidies kwa bidhaa muhimu kama mafuta - kama alivyofanya Kagame kwa wananchi wake?
Badala yake kaongeza tozo ya mafuta.
Kifupi mpango huo haupo, hata yeye amesema kupanda kwa bei serikali haihusiki na inabidi tuzoee tu. Mwenzake wa Zanzibar amepiga biti vitu visipande bei lakini huyu ye kavibariki vipande .

Hayati Mwenda alikua na u- Adolf Hitler lakini kuna vitu kweli asingeruhusu. Fikiria kua serikali ili subsidy gharama za kufunga umeme huyu Bibi kaja kaondoa hio subsidy. Sooner or later tutakuja kuambiwa kua hata Elimu bure haiwezekani tulipie tu.
 
Wakati yeye ndio anazidi kuhamasisha vitu vizidi kupanda bei. Anawakumbusha wafanya biashara wafanye hivyo.
Hapa sijamuelewa kabisa, hakutakiwa kusema hivi hadharani. Ni anahamasisha upandaji wa bei. Siku ile amezungumzia tu Tanesco kufunga umeme kwa TZS 27,000/= siku hiyo hiyo bei ikapanda. Mama haoni athari ya matamshi yake.
 
Maneno marefuuuu kama mnazi! Tunachotaka ni kwamba SSH ana mpango katika kutoa nafuu kwa wananchi kama vile kuweka subsidies kwa bidhaa muhimu kama mafuta - kama alivyofanya Kagame kwa wananchi wake?
Badala yake kaongeza tozo ya mafuta.
Vita ya Ukraine haiwahusu Zanzibar?
 
Vita ni kisingizio tu. Bali tumekwapua misaada na tozo kila kona kugharamia safari zisizo na umuhimu kwa Taifa. Hadi wauza mchaichai wamepandisha bei vita imehusikaje hapo
 
Hapa sijamuelewa kabisa, hakutakiwa kusema hivi hadharani. Ni anahamasisha upandaji wa bei. Siku ile amezungumzia tu Tanesco kufunga umeme kwa TZS 27,000/= siku hiyo hiyo bei ikapanda. Mama haoni athari ya matamshi yake.

Hafai ata kua kiongozi wa shule
 
Imenibidi kwa mara nyingine nijiridhishe kwa kurejelea kusikilizwa hotuba ya Mhe.Rais iliyokuwa inazungumzia kupanda bei kwa vitu kunakosababishwa na vita vya Ukraine na Russia na mapokeo ya kauli hiyo.

Sio kwamba nimetumia muda kusikilizwa tena sikusikia vizuri ila nilifanya hivyo kuongeza uelewa binafsi na kujiridhisha nia ya kutolewa kauli ile. Je, haikupaswa kutolewa au ingetolewaje?

Alichifanya Mhe. Rais ni kuweka kumbukumbu sawa kwa wanaoelewa na wataamua kupotosha na wasiolewa kabisa. Watanzania tuna tabia ya kusahau, kesho Mbowe au Lissu akipanda jukwaani na kudai Serikali imeamua kwa makusudi kupandisha bei ya vitu si wote watakaokumbuka kulikuwa na vita na moja ya madhara ya vita ile ilisababisha vitu kupanda. Watu watakuwa wamesahau na hiyo itakuwa ni agenda na wengi wanaolalamika wanalalamika agenda hiyo kuzimwa.

Ukweli ulio mchungu ambao wanaoujua hawataki watu waujue kwa sababu mbalimbali zikiwemo za kisiasa ni kwamba Tanzania ni 'importer' na bidhaa nyingi tumeagiza kutoka nje ambako ni watumiaji wakubwa wa mafuta na gesi ya Urusi katika uzalishaji na kwa sababu ya vita inayoendelea upatikanaji wa mafuta na gesi umekuwa wa kusuasua kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo:
i) vikwazo
ii) usalama
iii) malipo kutokubalika kwa mfumo uliozoelewa, n.k.
Tutajadili siku nyingine juu ya mambo mpaka kupelekea kuadimika kwa mafuta na gesi.

Hivyo, hata kama mafuta na gesi tunayotumia hayotoki Urusi lakini kwa sababu tunategemea bidhaa zinazozalishwa kwa gesi na mafuta ya Urusi basi kuathirika kwa doko kwao kutaathiri soko zima la nchi tegemezi.

Mfumo wa soko( market system) bei inategemea hali ya uhitaji na upatikanaji wa malighafi na vingine vingi. Tukitumia kanuni ya 'demand na supply' kupanda kwa bei ya mafuta na bidhaa nyingine zinazotegemea au kutumia mafuta kwa nchi yetu pia haiepukiki.

Ni ukweli usiopingika vitu vitapanda bei kutokana na kupanda bei katika soko la dunia sehemu ambayo Rais Samia hawezi kuzuia zaidi ya kuacha kanuni ya soko kufanya kazi.

Katika mazingira haya Serikali inatakiwa kudhibiti upandaji wa bei kiholela upandaji usiozingatia misingi ya kanuni ya soko lakini kusema itaweza kuzuia vitu kupanda bei ni kudanganywa wenyewe. Wanaoratibu bei ya soko ndio wameathiriwa na mfumuko wa bei ,kwa hiyo tutegemee bei Tanzania ibaki ileile?

Nampongeza Mhe.Rais kuwa muwazi na zaidi katuweka tayari kufunga mikanda dunia inapoelekea janga jingine la kiuchumi baada ya Corona kuonekana sio tishio tena.

Tumsaidieni Mhe.Rais kuusema ukweli huu, kwenye vita ya uchumi hatakiwi kupambana mwenyewe. Mwisho napenda kunukuu maneno ya Biblia yanayosema"Watu wataijua kweli nayo kweli itawaweka huru kwelikweli" na ninukuu pia msema wa kiswahili unaosema "mficha maradhi kifo humuumbua"

Acha Kuwa kama mbuni mnyama. Embu niwekee statistics /takwimu za uagizaji wa bidhaa za Tanzania kutoka Russia na Ukraine.

Hakuna msiba usiokuwa na waliaji, sasa corona imekwisha kusingiziwa now ni Ukraine na Urussi na hata vita ikiisha itatengenezwa na sababu zingine
 
Bado nakazia, niliyemtaja kwenye mada hii kipindi hicho leo kaanza kazi ya kupotosha.
 
Back
Top Bottom