Kauli ya vitu kupanda bei kisa vita ya Ukraine inapindishwa na walioielewa wanafunga mikanda kimyakimya

Tafakari yetu

JF-Expert Member
Apr 19, 2021
1,502
4,408
Imenibidi kwa mara nyingine nijiridhishe kwa kurejelea kusikilizwa hotuba ya Mhe.Rais iliyokuwa inazungumzia kupanda bei kwa vitu kunakosababishwa na vita vya Ukraine na Russia na mapokeo ya kauli hiyo.

Sio kwamba nimetumia muda kusikilizwa tena sikusikia vizuri ila nilifanya hivyo kuongeza uelewa binafsi na kujiridhisha nia ya kutolewa kauli ile. Je, haikupaswa kutolewa au ingetolewaje?

Alichifanya Mhe. Rais ni kuweka kumbukumbu sawa kwa wanaoelewa na wataamua kupotosha na wasiolewa kabisa. Watanzania tuna tabia ya kusahau, kesho Mbowe au Lissu akipanda jukwaani na kudai Serikali imeamua kwa makusudi kupandisha bei ya vitu si wote watakaokumbuka kulikuwa na vita na moja ya madhara ya vita ile ilisababisha vitu kupanda. Watu watakuwa wamesahau na hiyo itakuwa ni agenda na wengi wanaolalamika wanalalamika agenda hiyo kuzimwa.

Ukweli ulio mchungu ambao wanaoujua hawataki watu waujue kwa sababu mbalimbali zikiwemo za kisiasa ni kwamba Tanzania ni 'importer' na bidhaa nyingi tumeagiza kutoka nje ambako ni watumiaji wakubwa wa mafuta na gesi ya Urusi katika uzalishaji na kwa sababu ya vita inayoendelea upatikanaji wa mafuta na gesi umekuwa wa kusuasua kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo:
i) vikwazo
ii) usalama
iii) malipo kutokubalika kwa mfumo uliozoelewa, n.k.
Tutajadili siku nyingine juu ya mambo mpaka kupelekea kuadimika kwa mafuta na gesi.

Hivyo, hata kama mafuta na gesi tunayotumia hayotoki Urusi lakini kwa sababu tunategemea bidhaa zinazozalishwa kwa gesi na mafuta ya Urusi basi kuathirika kwa doko kwao kutaathiri soko zima la nchi tegemezi.

Mfumo wa soko( market system) bei inategemea hali ya uhitaji na upatikanaji wa malighafi na vingine vingi. Tukitumia kanuni ya 'demand na supply' kupanda kwa bei ya mafuta na bidhaa nyingine zinazotegemea au kutumia mafuta kwa nchi yetu pia haiepukiki.

Ni ukweli usiopingika vitu vitapanda bei kutokana na kupanda bei katika soko la dunia sehemu ambayo Rais Samia hawezi kuzuia zaidi ya kuacha kanuni ya soko kufanya kazi.

Katika mazingira haya Serikali inatakiwa kudhibiti upandaji wa bei kiholela upandaji usiozingatia misingi ya kanuni ya soko lakini kusema itaweza kuzuia vitu kupanda bei ni kudanganywa wenyewe. Wanaoratibu bei ya soko ndio wameathiriwa na mfumuko wa bei ,kwa hiyo tutegemee bei Tanzania ibaki ileile?

Nampongeza Mhe.Rais kuwa muwazi na zaidi katuweka tayari kufunga mikanda dunia inapoelekea janga jingine la kiuchumi baada ya Corona kuonekana sio tishio tena.

Tumsaidieni Mhe.Rais kuusema ukweli huu, kwenye vita ya uchumi hatakiwi kupambana mwenyewe. Mwisho napenda kunukuu maneno ya Biblia yanayosema"Watu wataijua kweli nayo kweli itawaweka huru kwelikweli" na ninukuu pia msema wa kiswahili unaosema "mficha maradhi kifo humuumbua"
 
Vita vya Ukraine-Urusi ni janga jengine ambalo dunia imeshaanza kuonja joto ya jiwe
Nalog off Z
 
Nchi zinazojitambua👇
AARD4K.jpeg
Tanzania👇🐒🐒🐒
 
Maneno marefuuuu kama mnazi! Tunachotaka ni kwamba SSH ana mpango katika kutoa nafuu kwa wananchi kama vile kuweka subsidies kwa bidhaa muhimu kama mafuta - kama alivyofanya Kagame kwa wananchi wake?
Badala yake kaongeza tozo ya mafuta.
Bado tunaelekea kulekule tusipojua tunaelekea wapi? Hilo suala ni la kisera zaidi na kwakuwa athari za vita vimejitokeza mapema hivyo ikiwezekana kuwe na sera sio leo tu hata kwa kesho pia
 
Tumetoka kwenye janga la Covid19 na mgogoro wa vita vya Ulaya mashariki kila Nchi inaipata fresh.
 
Mi nilidhani zile billion kadhaa wanazosema ni hadhina inayo weza kulilisha taifa kwa miezi kadhaa zingetumika kwenye kipindi kama hichi ili kubalance hii tabu tunayopitia
 
Imenibidi kwa mara nyingine nijiridhishe kwa kurejelea kusikilizwa hotuba ya Mhe.Rais iliyokuwa inazungumzia kupanda bei kwa vitu kunakosababishwa na vita vya Ukraine na Russia na mapokeo ya kauli hiyo.

Sio kwamba nimetumia muda kusikilizwa tena sikusikia vizuri ila nilifanya hivyo kuongeza uelewa binafsi na kujiridhisha nia ya kutolewa kauli ile. Je, haikupaswa kutolewa au ingetolewaje?

Alichifanya Mhe. Rais ni kuweka kumbukumbu sawa kwa wanaoelewa na wataamua kupotosha na wasiolewa kabisa. Watanzania tuna tabia ya kusahau, kesho Mbowe au Lissu akipanda jukwaani na kudai Serikali imeamua kwa makusudi kupandisha bei ya vitu si wote watakaokumbuka kulikuwa na vita na moja ya madhara ya vita ile ilisababisha vitu kupanda. Watu watakuwa wamesahau na hiyo itakuwa ni agenda na wengi wanaolalamika wanalalamika agenda hiyo kuzimwa.

Ukweli ulio mchungu ambao wanaoujua hawataki watu waujue kwa sababu mbalimbali zikiwemo za kisiasa ni kwamba Tanzania ni 'importer' na bidhaa nyingi tumeagiza kutoka nje ambako ni watumiaji wakubwa wa mafuta na gesi ya Urusi katika uzalishaji na kwa sababu ya vita inayoendelea upatikanaji wa mafuta na gesi umekuwa wa kusuasua kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo:
i) vikwazo
ii) usalama
iii) malipo kutokubalika kwa mfumo uliozoelewa, n.k.
Tutajadili siku nyingine juu ya mambo mpaka kupelekea kuadimika kwa mafuta na gesi.

Hivyo, hata kama mafuta na gesi tunayotumia hayotoki Urusi lakini kwa sababu tunategemea bidhaa zinazozalishwa kwa gesi na mafuta ya Urusi basi kuathirika kwa doko kwao kutaathiri soko zima la nchi tegemezi.

Mfumo wa soko( market system) bei inategemea hali ya uhitaji na upatikanaji wa malighafi na vingine vingi. Tukitumia kanuni ya 'demand na supply' kupanda kwa bei ya mafuta na bidhaa nyingine zinazotegemea au kutumia mafuta kwa nchi yetu pia haiepukiki.

Ni ukweli usiopingika vitu vitapanda bei kutokana na kupanda bei katika soko la dunia sehemu ambayo Rais Samia hawezi kuzuia zaidi ya kuacha kanuni ya soko kufanya kazi.

Katika mazingira haya Serikali inatakiwa kudhibiti upandaji wa bei kiholela upandaji usiozingatia misingi ya kanuni ya soko lakini kusema itaweza kuzuia vitu kupanda bei ni kudanganywa wenyewe. Wanaoratibu bei ya soko ndio wameathiriwa na mfumuko wa bei ,kwa hiyo tutegemee bei Tanzania ibaki ileile?

Nampongeza Mhe.Rais kuwa muwazi na zaidi katuweka tayari kufunga mikanda dunia inapoelekea janga jingine la kiuchumi baada ya Corona kuonekana sio tishio tena.

Tumsaidieni Mhe.Rais kuusema ukweli huu, kwenye vita ya uchumi hatakiwi kupambana mwenyewe. Mwisho napenda kunukuu maneno ya Biblia yanayosema"Watu wataijua kweli nayo kweli itawaweka huru kwelikweli" na ninukuu pia msema wa kiswahili unaosema "mficha maradhi kifo humuumbua"
Wajinga wengi walizoea serikali laghai na ya kuongea uongo kama ya Magufuli.
 
Mi nilidhani zile billion kadhaa wanazosema ni hadhina inayo weza kulilisha taifa kwa miezi kadhaa zingetumika kwenye kipindi kama hichi ili kubalance hii tabu tunayopitia
Bado hatujui yajayo, pengine ugumu utaongezeka na ikiwa hivyo akiba ya fedha za kigeni ikitumika sasa tutazalisha tatizo kubwa baadaye.
 
Tuachane na barakoa za corona tutafute barakoa za kukabiliana na ongezeko la bei za vitu. Mkate wa slesi wa 2 500/- Umekuwa 3,000/- ongezeko la 20%. Mafuta ya kula yaneongezeka bei zaidi ya 50%. Uongozi wa Watu na Kiongozi atajulikana katika kupatia changamoto ngumu zinazoikabili jamii.

Tukiendekeza wanao jisifia na kushangilia kurina asali katika mzinga wa Babu/bibi itakuwa si sawa. Yaleyale ya zana zile za ulaya ya wape keki watu wanaondamana kupinga bei ya mkate kupanda na kuadimika kwake.
 
Tatizo Wanasiasa hawana MAONO na PASSION ya kuwasaidia (kwa kuweka sera na mazingira wezeshi na rafiki katika kufanya biashara), Wananchi na kizazi Chetu kinachokuja.

Wanachowaza wao ni kushibisha tumbo na kukaa madarakani...

Wangekuwa na MAONO hakika wangeguswa na Hali ya maisha ya mwananchi wa chini..

Wataguswaje wakati wanajiona miungu na wanatembelea Kodi na kuzitapanya huku wao hata hawalipi Kodi ....??

#Mche wa sabuni umefika 3500 kutoka 2800 miezi miwili iliyopita
 
Imenibidi kwa mara nyingine nijiridhishe kwa kurejelea kusikilizwa hotuba ya Mhe.Rais iliyokuwa inazungumzia kupanda bei kwa vitu kunakosababishwa na vita vya Ukraine na Russia na mapokeo ya kauli hiyo.

Sio kwamba nimetumia muda kusikilizwa tena sikusikia vizuri ila nilifanya hivyo kuongeza uelewa binafsi na kujiridhisha nia ya kutolewa kauli ile. Je, haikupaswa kutolewa au ingetolewaje?

Alichifanya Mhe. Rais ni kuweka kumbukumbu sawa kwa wanaoelewa na wataamua kupotosha na wasiolewa kabisa. Watanzania tuna tabia ya kusahau, kesho Mbowe au Lissu akipanda jukwaani na kudai Serikali imeamua kwa makusudi kupandisha bei ya vitu si wote watakaokumbuka kulikuwa na vita na moja ya madhara ya vita ile ilisababisha vitu kupanda. Watu watakuwa wamesahau na hiyo itakuwa ni agenda na wengi wanaolalamika wanalalamika agenda hiyo kuzimwa.

Ukweli ulio mchungu ambao wanaoujua hawataki watu waujue kwa sababu mbalimbali zikiwemo za kisiasa ni kwamba Tanzania ni 'importer' na bidhaa nyingi tumeagiza kutoka nje ambako ni watumiaji wakubwa wa mafuta na gesi ya Urusi katika uzalishaji na kwa sababu ya vita inayoendelea upatikanaji wa mafuta na gesi umekuwa wa kusuasua kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo:
i) vikwazo
ii) usalama
iii) malipo kutokubalika kwa mfumo uliozoelewa, n.k.
Tutajadili siku nyingine juu ya mambo mpaka kupelekea kuadimika kwa mafuta na gesi.

Hivyo, hata kama mafuta na gesi tunayotumia hayotoki Urusi lakini kwa sababu tunategemea bidhaa zinazozalishwa kwa gesi na mafuta ya Urusi basi kuathirika kwa doko kwao kutaathiri soko zima la nchi tegemezi.

Mfumo wa soko( market system) bei inategemea hali ya uhitaji na upatikanaji wa malighafi na vingine vingi. Tukitumia kanuni ya 'demand na supply' kupanda kwa bei ya mafuta na bidhaa nyingine zinazotegemea au kutumia mafuta kwa nchi yetu pia haiepukiki.

Ni ukweli usiopingika vitu vitapanda bei kutokana na kupanda bei katika soko la dunia sehemu ambayo Rais Samia hawezi kuzuia zaidi ya kuacha kanuni ya soko kufanya kazi.

Katika mazingira haya Serikali inatakiwa kudhibiti upandaji wa bei kiholela upandaji usiozingatia misingi ya kanuni ya soko lakini kusema itaweza kuzuia vitu kupanda bei ni kudanganywa wenyewe. Wanaoratibu bei ya soko ndio wameathiriwa na mfumuko wa bei ,kwa hiyo tutegemee bei Tanzania ibaki ileile?

Nampongeza Mhe.Rais kuwa muwazi na zaidi katuweka tayari kufunga mikanda dunia inapoelekea janga jingine la kiuchumi baada ya Corona kuonekana sio tishio tena.

Tumsaidieni Mhe.Rais kuusema ukweli huu, kwenye vita ya uchumi hatakiwi kupambana mwenyewe. Mwisho napenda kunukuu maneno ya Biblia yanayosema"Watu wataijua kweli nayo kweli itawaweka huru kwelikweli" na ninukuu pia msema wa kiswahili unaosema "mficha maradhi kifo humuumbua"
Hoja nyingine ni za kipumbavu tu.Hivi hii Dunia ni lini haikuwahi kuwa na Vita? Vita ya Afghanistan imechukua miaka mingapi? Vita ya Iraq imechukua miaka mingapi? Syria, nk hazikuwa vita? Leo hii Urusi ndiyo imepandisha bei hata ya sabuni? Acheni hizo bhanaa.
Ingawa sisemi kuwa hii vita haijaleta athari kiuchumi kidunia, ila yapo mambo hayana ukweli
 
Hoja nyingine ni za kipumbavu tu.Hivi hii Dunia ni lini haikuwahi kuwa na Vita? Vita ya Afghanistan imechukua miaka mingapi? Vita ya Iraq imechukua miaka mingapi? Syria, nk hazikuwa vita? Leo hii Urusi ndiyo imepandisha bei hata ya sabuni? Acheni hizo bhanaa.
Ingawa sisemi kuwa hii vita haijaleta athari kiuchumi kidunia, ila yapo mambo hayana ukweli
Mafuta na gesi ni muhimu sana katika uzalishaji Ulaya kupanda.
Hoja nyingine ni za kipumbavu tu.Hivi hii Dunia ni lini haikuwahi kuwa na Vita? Vita ya Afghanistan imechukua miaka mingapi? Vita ya Iraq imechukua miaka mingapi? Syria, nk hazikuwa vita? Leo hii Urusi ndiyo imepandisha bei hata ya sabuni? Acheni hizo bhanaa.
Ingawa sisemi kuwa hii vita haijaleta athari kiuchumi kidunia, ila yapo mambo hayana ukweli
Vita nyingine haikuwa na athari kama hii kwa sababu:
i) mwarabu sio tegemeo kwenye uzalishaji
ii) Ulaya walikuwa hawatumii mafuta mengi kama yake
iii) Ukiachana na mafuta na gesi pia russia anazalisha ngano na alizeti kwa kiwango cha kutegemewa duniani.

Hayo machache yanaonesha ni kwa ukubwa gani vita hii zitaathiri nchi walaji na watumiaji
 
Back
Top Bottom