Kauli ya UVCCM Bagamoyo kuwa rais hatatoka kaskazini vipi kwa Lowassa, Migiro na Sumaye?

UVCCM haiwezi kuwachagulia Wa-Tanzania Rais...Hayo ni maoni yao binafsi..kwani Kaskazini siyo Wa-Tanzania??

Hao viongozi wote CCM wanao wania nafasi..Sioni kama wana-Majibu ambayo Mkuu wa sasa Jk hana..

Wamefanya kazi chini ya uongozi wake na wameishia kumuaibisha..

Jibu ni CDM pekee..
 
Kuna ukweli kwenye hizi propaganda zinazoenezwa kwenye mitandao hasa facebook?
''CONSPIRING COMMUNITY OF MUSLIMS (CCM)???''
''Nimeshachukua fungu kutoka nchi za kiarabu tuzitumie kuutokomeza kabisa huu ''mfumo kristo'' na hii ni kimya kimya, Si uliona nilianza na kuwachomoa kwenye Chama, tukachuka nafasi na hata serikali tumeishakamata nafasi muhimu. Kwa hiyo andaeni vijana waanze kazi ya kuwatia hofu, chomeni makanisa yao ila kwa awamu ili wapate muda wa kujisahau, Na hawa viongozi wao mwagia tindikali wafie huko, au watilieni polonium wapate kansa za damu na ngozi sawa? Halafu tunazuga kuwapeleka India ili ku'cover'... au siyo? kuhusu mahakamani msihofu tuna majaji wa kutosha, kesi zote zitaisha salama. Halafu nimekumbuka, fanyeni biashara kuongeza pato hata kama madawa ya kulevya kisha tuwakemee viongozi wao waache kuuza madawa, ili kuzugazuga, Si unajua ilee?, enhee halafu make sure hizo pesa zinajenga nyumba za ibada kila kona ya jiji sio kufanyia propaganda tu. Muangalie pia uwezekano wa kupata mafunzo al-shabaab ili hawa wanaojifanya wapinga ufisadi watiwe adabu, kwanza ndiyo maadui wakubwa wa uislam. Majasusi wa nje wameshastukia ila tumewapoza na mikataba minono na hata marais wao wameahidi kushirikiana na sisi na watakuja kuisainia hapa hapa. Si unajua wao wanataka mali tu, Na kale kachama kanajifnya kakiharakati na kizalendo kaacheni tu hakafiki 2015, kuna kijana pale na kundi kubwa tu la kukiharibu, tumeshamshika. Na hili jamaa linalopiga kampeni misikitini na makanisani tunalitafutia dawa yake, Kwanza nadhani ASHA anatosha, kama tulivyofanya kwa spika, si unakumbuka eeh?, Ila limejitahidi sana kujisafisha me nilidhani nimemaliza kazi ile January 2008. Anajifanya ana pumzi sana na mamvi yake. Lakini naomba tena na tena huu mpango uwe wa siri kubwa na waumini wenyewe wasijue wao ni kuwaelekeza tu sawa? Inshallah mwenyezi mungu akijalia mwaka 2030 hii inakuwa dola mpya ya kiislam. Inshallah...
Kanchi kadogo kama haka tuna ulizana udini, ukabila, ukanda mwisho wake utakuwa nini jamani.
 
Huruma yako ni ipi kwa huyu jamaa?

kuwa siku zote anachagua upande mbaya wahistoria ,anaingia ktk game ya kuporwa dkk ya mwisho.Sitaki amini kuwa ujanja wote wa Lowasa ni km wenzie kulinda gate tuu.
 
basi tutamchagua anaetoka katikati ya nchi a.k.a dodoma ili kila upande uweze kufaidika au siyo jamani.
 
Kumbe kwa Nyerere ni Kaskazini? Mimi nilifikiri ni Kanda ya Ziwa? Kweli mtoa mada umevurugwa ma------ni.

Mkuu usijidhalilishe. Angalia vizuri ramani ya Tanzania. Upande wa kaskazini Tanzania inapakana na Kenya na Uganda. Upande wa kaskazini mwa Tanzania mikoa inayopakana na Kenya ni Arusha(mpaka maarufu kule wa kuingia na kutoka Kenya ni Namanga), Kilimanjaro(mpaka maarufu kule kuingia na kutoka Kenya ni Tarakea, Mara(mpaka maarufu kule wa kuingia na kutoka Kenya ni Silari) na Tanga(mpaka maarufu kule wa kuingia na kutoka Kenya ni Horohoro). Hata kwa uwezo wako mdogo wa jiografia ya Tanzania au Tanganyika. Angalia vizuri ramani ya Tanzania halafu uniambie hiyo kanda ya ziwa iko upande gani mwa Tanzania ukizingatia pande nne za dunia hata pande nne za Tanzania? Iko kusini, mashariki, magaharibi sawa na Kigoma au Kaskazini? Halafu kuna haja gani kutukana. Hapa tunajadili mada tunachotakiwa ni kukubaliana au kukubaliana kutokubaliana bila kutukanana. Kutukana ni kuonedha kiwango cha chini kabisa cha ustaarabu na uwezo mdogo wa kufikiri. Badala ya kujadili mada unamtukana mtoa mada. Fallacy!
 

Attachments

  • Map.bmp
    6.4 MB · Views: 176
Tulimumu, Nyerere na Wasira ni wa kaskazini kweli? Makubwa haya! geografia yako haipo sawa au historia ya watu hawa kwakao haijakaa sawa! Au una maana gani? nakubalina Lowassa, Sumaye na huyu mpare Mama Migiro wanatoka kaskazini.

Mkuu angalia ramani halafu niambie Mara iko upande gani mwa Tanzania.
View attachment 124912
 
Kumbe kwa Nyerere ni Kaskazini? Mimi nilifikiri ni Kanda ya Ziwa? Kweli mtoa mada umevurugwa ma------ni.
Habari za siku mkuu. Ulinitukana kuwa nimevurugwa. Hivi ile ramani niliyokutumia ilikusaidia kujua ulipo mkoa wa Mara katika nchi yetu? Leo mmoja wa watoka kaskazini ametangaza nia. Bado nasisitiza na ndio ukweli wa kijiografia kuwa mkoa wa Mara uko Kaskazini mwa Tanzania kama ilivyo Arusha, Kilimanjaro na Tanga na mikoa yote hiyo inapakana na Kenya ambayo nayo iko kaskazini
 
Ile kauli iliyotolewa na kikao cha UVCCM Pwani, na kutangazwa na vyombo kadhaa vya habari kuwa "Rais ajaye (2015), hawezi kutokea Kaskazini" ndiyo inayoitafuna CCM na kumpa nguvu kubwa Lowassa.

Ukimya wa viongozi wa ngazi za juu wa chama baada ya kauli hiyo iliyolaaniwa kila sehemu ulimaanisha kuwa msimamo huo ulikuwa na baraka za wakubwa wa chama.

Tokea hapo watu walikuwa wanajiuliza mioyoni mwao juu ya ubaguzi huo wa wazi wa CCM, na hata watu wakaanza kuhusisha hali hiyo na yaliyomkuta Lowassa.

Leo Lowassa anapata umaarufu kirahisi pamoja na tuhuma zote za ufisadi kwa sababu tu watu (hasa wanaCCM wenyewe), wanataka kufuta mbegu ya ubaguzi wa kikanda iliyopandwa kwenye chama chao.

Najua kwamba Lowassa sio "the best" kwa chama chao, lakini kwa namna yeyote ile kama Lowassa hatateuliwa kugombea na CCM, itakuwa ngumu sana kuwaaminisha watu kuwa huo sio utekelezaji wa kauli-mbiu "raisi hatatoka kaskazini"...

Vyama vya siasa vijifunze nini cha kusema kwenye hadhira...
 
Kaskazini tumechoka kubaguliwa. Liwalo na liwe atakayewekwa kutoka kaskazini iwe UKAWA ama CCM sisi wakaskazini tutampa kura yetu...
 
Back
Top Bottom