KAULI ya rais wangu ajaye!!

Kigarama

JF-Expert Member
Apr 23, 2007
2,492
1,230
Akiwa wa Mwisho kumaliza mbio za Marathoni zilizoshirikisha wakimbiaji 75 huko Mexico John Stephen Akwhari (Huyu ni Mtanzania Jamani) Alipoulizwa ni kwa nini amendelea kukimbia ilihali ameumia Goti na anavuja damu. Akwari alijibu "My country did not send me 10,000 miles just to start the race; they sent me to finish the race."

Nataka mtu yeyote anayetaka kuwa Rais wangu mwaka 2015 aje na kauli hii na kwa dhati tukimtazama awe anafanana nayo ila yeye aseme "wananchi wa Tanzania hawakunichagua ili niwe rais wao, bali wamenichagua niutumikie urais kwa faida yao"

Namshukuru SlidingRoof kwa kutukumbusha kisa hiki cha shujaa wetu Akwhari!
 
kwa kauli kama hii kiongozi, ni viongozi wachache mno wanaoweza kuotoa kwa wananchi wao, wengi hawatambui kuwa kupewa nafasi kuongaza wananchi tayari ni dhamana ya kutenda yale yanayotakiwa kwa maendeleo ya wananchi.
 
TZ hatuna kiongozi mwenye uzalendo kama huo, wengin wapo kwa maslahi yao binafsi, wengi hukimbilia siasa kama sehemu ya kuja kupumzikia (kujihifadhi) baada ya kuchuma kodi za walala hoi!
 
Akiwa wa Mwisho kumaliza mbio za Marathoni zilizoshirikisha wakimbiaji 75 huko Mexico John Stephen Akwhari (Huyu ni Mtanzania Jamani) Alipoulizwa ni kwa nini amendelea kukimbia ilihali ameumia Goti na anavuja damu. Akwari alijibu "My country did not send me 10,000 miles just to start the race; they sent me to finish the race."

Nataka mtu yeyote anayetaka kuwa Rais wangu mwaka 2015 aje na kauli hii na kwa dhati tukimtazama awe anafanana nayo ila yeye aseme "wananchi wa Tanzania hawakunichagua ili niwe rais wao, bali wamenichagua niutumikie urais kwa faida yao"

Namshukuru SlidingRoof kwa kutukumbusha kisa hiki cha shujaa wetu Akwhari!

Angalizo zuri sana hilo lakini naogopa kwa misimamo yako hiyo, huyo unayemuunga mkono yuko opposite na kauli hiyo.
 
Back
Top Bottom