Wote tumemsikia Rais akishauri na kusisitiza wizara ya afya iwasisitize watu zaidi matumizi ya tiba asili kama kujifukiza kwa wagonjwa wa corona. Taasisi ya Rais haiwezi kuongea bila kuwa na taarifa sahihi kutoka vyanzo vyake. Si hilo tu, kuna shirikisho au tuite umoja wa waganga wa tiba asili wanaotambulika na mamlaka hapa nchini.
Kwa vile kirusi cha korona hakina dawa na inasemekana kujifukiza na baadhi ya dawa asili zipo zinazoongeza kinga mwili kwa ajili ya kupambana na magonjwa ikiwemo corona, kwanini wizara ya Afya isitenge karantini maalumu ambayo hawa wataalamu wa tiba asili waliokwisha thibitishwa na mamlaka husika waende nao kuonyesha utaalamu wao kwa kuwasaidia waliopata changamoto ya korona
Imethibitika kwamba wagonjwa wakorona hospitali au kwenye vituo maalumu hakuna dawa mahususi wanayopewa ya kutibu corona zaidi ni kuwaangalia tu na kuwapa dawa za kutibu magonjwa nyemelezi mengine.
Wizara husika hawaoni kwamba hawa wataalamu wa tiba asili wanaweza kuwa msaada zaidi kwenye hizo kalantini na hawa madaktari ambao kimsingi hata hawatoshi wabaki kutibu wagonjwa wengine?
Nashauri hawa waliokwisha thibitishwa ambao sio janja janja wapelekwe kwenye hizo kalantini wakatoe huduma hata kama serikali haitawalipa wagonjwa wenyewe watajilipia maana tunajua namna serikali ya sasa inavyotolea macho kukusanya zaidi kuliko kutumia hata pale ambapo ni muhimu. Serikali nyingine dunia zinasamehe kodi na kutoa unafuu kwa watu wao ila hapa kwetu ndo kwanza TRA wanapita mtaani kusisitiza watu walipe kodi kwa wakati badala ya magari hayo kupita kuhimiza watu wajilinde dhidi ya korona
Madagascar wameshaanza, nasisi tufuate. Tamko la Rais kwamba watu waruhusiwe kujitibu kiasili tena akasema wizara isisitize zaidi hili linaweza kuleta madhara kwa watu wengi kama halitawekewa miongozo. Tunawafahamu watanzania wanavyojua kutumia fursa, kwa hili kuna makanjanja wengi wanaweza kuibuka na kughalimu maisha ya watu.
Kwa vile kirusi cha korona hakina dawa na inasemekana kujifukiza na baadhi ya dawa asili zipo zinazoongeza kinga mwili kwa ajili ya kupambana na magonjwa ikiwemo corona, kwanini wizara ya Afya isitenge karantini maalumu ambayo hawa wataalamu wa tiba asili waliokwisha thibitishwa na mamlaka husika waende nao kuonyesha utaalamu wao kwa kuwasaidia waliopata changamoto ya korona
Imethibitika kwamba wagonjwa wakorona hospitali au kwenye vituo maalumu hakuna dawa mahususi wanayopewa ya kutibu corona zaidi ni kuwaangalia tu na kuwapa dawa za kutibu magonjwa nyemelezi mengine.
Wizara husika hawaoni kwamba hawa wataalamu wa tiba asili wanaweza kuwa msaada zaidi kwenye hizo kalantini na hawa madaktari ambao kimsingi hata hawatoshi wabaki kutibu wagonjwa wengine?
Nashauri hawa waliokwisha thibitishwa ambao sio janja janja wapelekwe kwenye hizo kalantini wakatoe huduma hata kama serikali haitawalipa wagonjwa wenyewe watajilipia maana tunajua namna serikali ya sasa inavyotolea macho kukusanya zaidi kuliko kutumia hata pale ambapo ni muhimu. Serikali nyingine dunia zinasamehe kodi na kutoa unafuu kwa watu wao ila hapa kwetu ndo kwanza TRA wanapita mtaani kusisitiza watu walipe kodi kwa wakati badala ya magari hayo kupita kuhimiza watu wajilinde dhidi ya korona
Madagascar wameshaanza, nasisi tufuate. Tamko la Rais kwamba watu waruhusiwe kujitibu kiasili tena akasema wizara isisitize zaidi hili linaweza kuleta madhara kwa watu wengi kama halitawekewa miongozo. Tunawafahamu watanzania wanavyojua kutumia fursa, kwa hili kuna makanjanja wengi wanaweza kuibuka na kughalimu maisha ya watu.