Mwanamke katili hawezi kuishi na mme, sifa ya kwanzaWanabodi,
Moja ya matumizi mazuri ya mitandao ya kijamii ni kuhabarishana, kuelimishana, kuburudishana, nakusaidiana.
Ikitokea kuna jambo unalijua, mwenzako halijui, msaidie kumuelimisha kwa kutumia experience yako kuelimisha wengine nao wajue.
Ila kauli ya Rais Samia aliyoitoa siku ya Uhuru wa Habari kuwa waandishi wa habari watakao mpara, atawaparua, imeleta sintofahamu kwa baadhi ya watu kuanza kumdhania na Rais Samia pia ni rais katili?.
Naomba kukiri, nimekuwa inspired kupandisha bandiko hili Uhuru wa Habari Tanzania: Kati ya Waparaji na Wakunaji Wazuri, Nani Watamsaidia Zaidi Rais Samia?. Tunakuomba Mama, Usiwaparure Waparaji!.
kutokana na post ya Mwanajf huyu
Mkuu Bejamini Netanyahu , sii kweli!. Wewe ndio utakuwa humjui vizuri, hivyo najitolea kukusaidia wewe na wengine wa aina yako Kwa kukuendeshea somo la jinsi ya kumtambua mtu katili. Tena hata kwa JPM, kabla hata ya kuchaguliwa kuwa Rais wa JMT, ile mwaka 2014, kuna kitu nilikisema humu kumhusu JPM Elections 2015 - Mgombea wa Urais Kwa tiketi ya CCM, 2015 "Could Be" John Pombe Magufuli humo nilisema kila kitu kumhusu JPM, ila pia baadhi ya mabandiko yangu, sio mabandiko ya watu wote kama bandiko hili, ni Bandiko kwa watu wenye jicho la tatu only ndio walibaini nasema nini. Sio kila kitu ni kwa watu wote!, vitu vingine ni kwa ajili ya wale tuu wa kiwango fulani na kwa wengine ni hakuna jinsi.
Ukatili wa mtu, haukai mdomoni kwenye kauli, wala haikai usoni kwenye kukunja uso, ukatili wa mtu hukaa moyoni, hivyo kwa jicho la kawaida, sii rahisi kumjua mtu mkatili, lakini watu waliojaaliwa jicho la tatu, huona ndani ya moyo wa mtu kupitia macho yake!.
Humu ndani nimeisha endesha masomo kibao ya utambuzi, moja ya masomo hayo ni somo kuhusu watu makatili na jinsi ya kuwatambua Character Assassination ni Modus Oparandi ya Madikiteta Katili Wote Duniani!
Watu makatili, huitwa ma sadist, namna rahisi ya kuwatambua watu hawa ni ukiona mtu anashangilia vitendo vya ukatili, na sisi Tanzania tuliwahi kuwa na viongozi wa type hii, sisi wengine tukasaidia kuwazungumzia, kama huyu This man is either a sadist or alimuua kibaka, akanywa bia kusherehekea?
Kwa vile ukatili hukaa moyoni, na sio usoni, au mdomoni, ni vigumu kuubaini. Mimi ni miongoni mwa watu waliopitia changamoto kubwa za maisha, hivyo kupitia hizo changamoto zikanifunza by experience. hivyo hapa natumia uzoefu wangu kusaidia wengine.
Kwanza nilioa nikiwa na umri mdogo wa miaka 25tuu, binti miaka 21, tukisoma wote darasa moja Chuo cha TSJ. Baada tuu ya ndoa tuhama nchi kwenda UK, then US kisha tukarudi Bongo, enzi hizo mimi ni mtangazaji maarufu wa Kipindi cha Kiti Moto.
Hivyo by 30 years tayari familia tuna watoto 2, wife akapata scholarship ya 4 years US na mimi kubaki na watoto wawili ( a 4 years girl & a 1.5 years boy). Hivyo scholarship hiyo ndio ikawa mwanzo wa changamoto za maisha. jumla!.
Kwa miaka yote 4 ya scholarship ya wife, kibarua cha kwanza ni kulea familia as a single parent father!. Pale ndipo nilipojua umuhimu wa wadada wa kazi!. Kiukweli hawa wadada wa kazi, waheshimiwe Sana na walipwe vizuri!.
Kibarua cha pili siku msichana wa kazi amepata msiba hivyo kwenda kwao na wewe kuachiwa uyaya wa watoto wawili wadogo for just two days!. There was no way out, lazima tuu uta import!. Kumbe jirani kaachiwa assignment ya kulinda na kuropoti!. Taarifa ya importation ikafika kusiko. Mtu kumaliza shule akagoma kurudi jumla!.
Ndipo nikakubali matokeo na Kuanza changamoto ya search kumpata mama wa Kambo ambaye hata nitesea wanangu!. Hapa ndipo nikaingia darasani kufungua a third eye kubaini wanawake katili .
Utambuzi wa Mama wa Kambo katili unafanyika kwa kumtazama machoni huyo mwanamke wakati akiwa na wewe mkiwa pekeyenu na kimlinganisha na akiwa na wewe na watoto wako!. Hivyo kuna vitu utaviona!, na utajua huyo mwanamke ni mke mwenye roho mzuri au ni mwanamke katili. That search took me 10 good years to find the right one, na miaka hiyo 10 ya search, produced 3 issues!. By the time you find her the family has 5 issues!.
Hivyo mtu mwenye macho kama haya Ikitokea kuna Kiongozi ana Macho mazuri, na umeyapenda, je, kuna ubaya kumsifia macho yake? Ni ukosefu wa heshima na adabu? hawezi kuwa mtu katili!.
Hebu angalia hayo macho kwenye picha hii View attachment 2216119View attachment 2216122
View attachment 2216124
Mtu kama huyu, kweli anaweza kuwa katili?. Angalia macho!.
Sasa Kwa faida ya wasiomjua vizuri huyu Mama, jielimishe hapa
Siku ya Wanawake Duniani: VP Samia Suluhu: "Womanly, Genuine, Humble, Simple na Down To Earth!”
Wanabodi, Leo asubuhi nimeangalia kipindi cha mahojiano ya Makamo wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumzia Siku ya Wanawake Duniani kwenye TBC akihojiwa na Shabani Kissu. Kwa Waliosikiliza kipindi hiki, kiukweli huyu ni mwanamke wa kupigiwa mfano, mtanisamehe sina maneno ya Kiswahili ya...www.jamiiforums.com
"Watu waachwe Huru kuujadili Muungano"- VP, Samia Suluhu Hassan. Huyu mama anaongea vizuri kwa Unyenyekevu mpaka raha. Huchoki kumsikiliza
Wanabodi, Niko kwenye voluntariy lockdown, hivyo leo nimepata fursa ya kuangalia TV ya Zanzibar, ZBC, Mwandishi wa habari wa CCM Zanzibar, Daudi Ismail anamhoji Makamo wa Rais wa JMT, Mhe. Samia Suluhu Hassan anauzungumzia Muungano, kiukweli huyu Mama Samia anauzumguza vizuri muungano huku...www.jamiiforums.comPsychoanalysis Trends za Viongozi Wetu, Humbleness ya Rais Samia ni Bonafide Genuine, ni asili yake, ni nature yake, ndivyo alivyo, Ila...
Wanabodi, Moja ya topic ngumu sana humu JF, ni topic za kitu kinachoitwa Trends Readings za psychoanalysis trends, kinacho tokana na ku Psychoanalyse Trends kisaikolojia kwa kutumia tabia za mtu za nyuma, tabia zake za sasa kuweza ku détermine tabia zake za huko tunakwenda na ni nini...www.jamiiforums.comWatanzania tumshukuru Mungu kupata mtu mwenye moyo wa kusamehe. Je, tumuombe asamehe tu bila kuombwa msamaha au akomae naye?
Wanabodi, Hii ni makala yangu ya Wiki hii ya Christmas. Kunapotokea kosa lolote, mkosaji ana wajibu wa kushughulikiwa kwa mujibu wa sheria, hivyo kinachoendelea sasa ni kwa sheria kuachwa kufuata mkondo wake, ila sasa kuna kelele nyingi, hivyo hili ni bandiko la swali. "Watanzania tumshukuru...www.jamiiforums.com
Hitimisho
Ile kauli ya "wakinipara nitawaparura" sio kuparura kwa ukatili kutumia makucha kama paka akiparua, au kuparua kama yakupara samaki, hii ni kauli tuu ya tamathali ya semi, kwa media zitakazo mpara, zitaparuliwa kwa kutumia sheria zetu kandamizi zilizopo!
Paskali