Ni fedheha na aibu kubwa kwa naibu waziri ndugu Katambi kutoa majibu yale ya kudhalilisha vijana wa nchi hii Kwa swali aliloulizwa.
Kujibu kuwa vijana ambao hawajafanikiwa kupata mikopo inayotolewa na halmashauri watokako kutokana na fedha kidogo zinazokusanywa na halmashauri ama wingi wa vijana wenye uhitaji kuwa sio wazawa wa Tanzania au ATI ni wakenya haivumiliki na itoshe aiachie ofisi na nafasi yake na ikimpendeza CCM imvue ubunge anaoringia.
Nawashangaa UVCCM wameuchuna kana kwamba kauli hiyo ya Naibu Waziri ni pambio la kusifu na kuabudu.
Mh. Rais Yale mabega uliyoonya yasipandishwe Katambi kaipuuza na kulinanga kundi kubwa la wapiga kura wako ambao kimsingi wanataabika kwa shida mbalimbali zikiwemo kufukuzwa maeneo wanakofanyia shughuli zao na kuharibiwa mitaji Yao ambayo serikali haijui waliipataje.
Nitakushangaa Sana wewe Mh. Rais na UVCCM kumvumilia Naibu Waziri Katambi kwani amejidhihirisha wazi kuwa kati ya viongozi wanaokuhujumu na kukuchonganisha wewe na vijana ambao Kwa wingi wao wakiamua kujibu mapigo itakuwia vigumu mno kuwatuliza! Mtimue aende zake.
Kujibu kuwa vijana ambao hawajafanikiwa kupata mikopo inayotolewa na halmashauri watokako kutokana na fedha kidogo zinazokusanywa na halmashauri ama wingi wa vijana wenye uhitaji kuwa sio wazawa wa Tanzania au ATI ni wakenya haivumiliki na itoshe aiachie ofisi na nafasi yake na ikimpendeza CCM imvue ubunge anaoringia.
Nawashangaa UVCCM wameuchuna kana kwamba kauli hiyo ya Naibu Waziri ni pambio la kusifu na kuabudu.
Mh. Rais Yale mabega uliyoonya yasipandishwe Katambi kaipuuza na kulinanga kundi kubwa la wapiga kura wako ambao kimsingi wanataabika kwa shida mbalimbali zikiwemo kufukuzwa maeneo wanakofanyia shughuli zao na kuharibiwa mitaji Yao ambayo serikali haijui waliipataje.
Nitakushangaa Sana wewe Mh. Rais na UVCCM kumvumilia Naibu Waziri Katambi kwani amejidhihirisha wazi kuwa kati ya viongozi wanaokuhujumu na kukuchonganisha wewe na vijana ambao Kwa wingi wao wakiamua kujibu mapigo itakuwia vigumu mno kuwatuliza! Mtimue aende zake.