Synthesizer
JF-Expert Member
- Feb 15, 2010
- 11,129
- 18,743
Juzi hapa ajali ilitokea kati ya lori la Fuso na basi la City Boys katika harakati za dereva wa Fuso kukwepa shimo barabarani na kuingia upande wa basi na kusababisha wagongane uso wa uso, na watu 12 kufa na 46 kujeruhiwa.
Nilisema humu JF kwamba ajali zinazosababishwa na mashimo barabarani yanayoachwa muda mrefu, TANROADS wanapaswa kushitakiwa. Na kauli hii imerudiwa tena na Mbunge wa Ulanga Mashariki Goodluck Mlinga kuwa TANROADS wawe wanapigwa faini kwa ajali zinazosababishwa na vitu kama mashimo yasiyofukiwa kwa kuwa na wao wanafanya uzembe. Mbunge Mlinga alisema pia TANROADS wanapenda sana kubambikiza watu faini zisizoeleweka wakati upande wao wanafanya uzembe wa kutorekebisha barabara.
Waziri Mwigulu alijibu kauli ya Mbunge Mlinga kwamba ajali hiyo haikusababishwa na shimo bali mwendo mkali wa dereva kwa kuwa magari mengine hayakupata ajali sehemu hiyo!
Kauli hii ya Mwigulu ni ya kizembe haistahili hata kutolewa na mtu ambaye anajiita msomi na kupewa daraka la kuwa waziri. Ni kauli ya kizembe kwa sababu inatetea uzembe wa TANROADS dhidi ya maisha ya Watanzania na mali zao. Najiuliza;
Refer:
TANROADS wanapaswa kushtakiwa kwa ajali na vifo vinavyotokana na ubovu wa barabara
Nilisema humu JF kwamba ajali zinazosababishwa na mashimo barabarani yanayoachwa muda mrefu, TANROADS wanapaswa kushitakiwa. Na kauli hii imerudiwa tena na Mbunge wa Ulanga Mashariki Goodluck Mlinga kuwa TANROADS wawe wanapigwa faini kwa ajali zinazosababishwa na vitu kama mashimo yasiyofukiwa kwa kuwa na wao wanafanya uzembe. Mbunge Mlinga alisema pia TANROADS wanapenda sana kubambikiza watu faini zisizoeleweka wakati upande wao wanafanya uzembe wa kutorekebisha barabara.
Waziri Mwigulu alijibu kauli ya Mbunge Mlinga kwamba ajali hiyo haikusababishwa na shimo bali mwendo mkali wa dereva kwa kuwa magari mengine hayakupata ajali sehemu hiyo!
Kauli hii ya Mwigulu ni ya kizembe haistahili hata kutolewa na mtu ambaye anajiita msomi na kupewa daraka la kuwa waziri. Ni kauli ya kizembe kwa sababu inatetea uzembe wa TANROADS dhidi ya maisha ya Watanzania na mali zao. Najiuliza;
- Mwigulu anajuaje kama mwendo wa Fuso ulikuwa kasi? Ukiwa dereva hata kama uko mwendo wa 50km/hr ukakutana na shimo mara nyingi instinct ya kwanza ni kulikwepa. Na hata akimshitaki dereva wa Fuso kwa mwendo kasi, ni uthibitisho gani anao kwamba alienda mwendo kasi, na mwendo kasi wa kiasi gani?
- Kusema mbona magari mengine hayakupata ajali hiyo sehemu, je Mwigulu anataka kutuambia kwamba kila gari lililopita hiyo sehemu ya shimo lilipita kukiwa na gari nyingine upande wa pili? Anataka kusema kwamba hata kama kusingekuwa na basi upande wa pili Fuso ingepata ajali?
- Mwigulu anasema dereva wa Fuso alipaswa kupunguza mwendo kwenye hili shimo - je Mwigulu bado anatutarajia Watanzania tuelewe na kukumbuka kila shimo lililopo katika barabara za TANROADS ili tupunguze mwendo kila tunapokaribia sehemu yenye shimo?
- Kama Mwigulu ni msomi wa kweli basi anajua theory ya cause-effect; anachotaka kusema ni kwamba kama pasingekuwa na shimo na dereva wa Fuso akawa na spidi ile ile aliyokuwa nayo katika ajali hii, pangetokea ajali? Kwa hiyo nini kimesababisha ajali hapa, spidi au shimo?
Refer:
TANROADS wanapaswa kushtakiwa kwa ajali na vifo vinavyotokana na ubovu wa barabara