Mkapa ni mmoja wa marais wenye msimamo ambao Tanzania imewahi kuwapata. Ni katika kipindi chake ndiyo Tanzania imeshuhudia mapinduzi makubwa ya kiuchumi hasa katika kuuza na kubinafsisha mashirika ya uma. Kuna mazuri na mabaya anayotuhumiwa kuyafanya wakati wa utawala wake, hata hivyo unapokuwa kiongozi huwezi kumridhisha kila mtu kwani maadui hawatakosena kwa njia moja ama nyingine.
Ndiyo maana viongozi wetu wastaafu bado wanapatiwa huduma zote muhimu ikiwemo ya kulinda maisha yao kutokana na maadui mbalimbali wanaojulikana na wasiojulikana. Kitendo cha Mkapa kutamka wazi kuwa anaogopa kusema ni maamuzi gani magumu aliwahi kuyatoa kwani "bado nataka kuishi" ni ishara mbaya kwa usalama wa viongozi wetu ambao wanatoa maamuzi kwa niaba ya watanzia wote siyo kikundi cha wa watu wachache.
Kwa maana hiyo basi sisi kama Taifa hatuna budi kuwalinda viongozi wetu kwa kutumia kila uwezo tulionao ili kuwafanya wasihofie maisha yao kwa sababu tu walichukua maamuzi magumu kwa faida ya nchi yetu kabla na baada ya kustaafu. Vinginevyo tutakuwa na viongozi "dummy" na hata puppet wakiangalia zaidi kulinda maisha yao kuliko kutumia taifa kwa moyo wa dhati bila hofu toka kwa mtu yeyote.
Nchi kama Tanzania inahitaji viongozi watakaokuwa tayari kutoa maamuzi magumu kwa faida ya watanzania bila woga, tukifikia hapo nina hakika kuwa Tanzania itasonga mbele. Utamaduni wa woga tuliona watanzania (wananchi na viongozi wetu) ni sababu kuu ya Taifa letu kuwa nyuma kimaendeleo, kwani hatuna uthubutu wa kufanya mambo kwa kuangalia masilahi watanzania walio wengi hata kama yatawauzi wachache wenye nguvu badala ya kufanya kwa kuangalia usalama na kiulaji binafsi.
My take: Watanzania tuwe na ujasiri, kwani hata baba wa taifa kwenye sherehe za CCM kitaifa 1988 pale Tabora Ali Hassan Mwinyi Stadium, alisema "Taifa lolote litakalokosa wananchi walio tayari kujitolea basi, taifa hilo lisahau kupata maendeleo". Kama mtanzania unaona huwezi kujitolea iwe maisha, nguvu, akili zako basi unakuwa umekosa sifa za kuongoza wengine kuelekea kwenye maendeleo. Viongozi wetu wanatakiwa kuwa ni watu waliojitolea zaidi ili kufanikisha lengo hilo, vinginevyo tutakuwa tunatumikia woga na vitisho toka kwa wahalifu wachache.
Kama mtu huwezi kutoa maamuzi magumu kwa hofu yoyote ukiwa kama kiongozi, Inakuwa ni jambo la busara zaidi kama utafuta mawazo ya kuomba "UONGOZI"- Kwani uongozi ni ujasiri ukiwa mwoga kila siku unaowaongoza watadhurika
http://www.globalpublishers.info/video/bado-nataka-kuishi-mkapa source GPL
Ndiyo maana viongozi wetu wastaafu bado wanapatiwa huduma zote muhimu ikiwemo ya kulinda maisha yao kutokana na maadui mbalimbali wanaojulikana na wasiojulikana. Kitendo cha Mkapa kutamka wazi kuwa anaogopa kusema ni maamuzi gani magumu aliwahi kuyatoa kwani "bado nataka kuishi" ni ishara mbaya kwa usalama wa viongozi wetu ambao wanatoa maamuzi kwa niaba ya watanzia wote siyo kikundi cha wa watu wachache.
Kwa maana hiyo basi sisi kama Taifa hatuna budi kuwalinda viongozi wetu kwa kutumia kila uwezo tulionao ili kuwafanya wasihofie maisha yao kwa sababu tu walichukua maamuzi magumu kwa faida ya nchi yetu kabla na baada ya kustaafu. Vinginevyo tutakuwa na viongozi "dummy" na hata puppet wakiangalia zaidi kulinda maisha yao kuliko kutumia taifa kwa moyo wa dhati bila hofu toka kwa mtu yeyote.
Nchi kama Tanzania inahitaji viongozi watakaokuwa tayari kutoa maamuzi magumu kwa faida ya watanzania bila woga, tukifikia hapo nina hakika kuwa Tanzania itasonga mbele. Utamaduni wa woga tuliona watanzania (wananchi na viongozi wetu) ni sababu kuu ya Taifa letu kuwa nyuma kimaendeleo, kwani hatuna uthubutu wa kufanya mambo kwa kuangalia masilahi watanzania walio wengi hata kama yatawauzi wachache wenye nguvu badala ya kufanya kwa kuangalia usalama na kiulaji binafsi.
My take: Watanzania tuwe na ujasiri, kwani hata baba wa taifa kwenye sherehe za CCM kitaifa 1988 pale Tabora Ali Hassan Mwinyi Stadium, alisema "Taifa lolote litakalokosa wananchi walio tayari kujitolea basi, taifa hilo lisahau kupata maendeleo". Kama mtanzania unaona huwezi kujitolea iwe maisha, nguvu, akili zako basi unakuwa umekosa sifa za kuongoza wengine kuelekea kwenye maendeleo. Viongozi wetu wanatakiwa kuwa ni watu waliojitolea zaidi ili kufanikisha lengo hilo, vinginevyo tutakuwa tunatumikia woga na vitisho toka kwa wahalifu wachache.
Kama mtu huwezi kutoa maamuzi magumu kwa hofu yoyote ukiwa kama kiongozi, Inakuwa ni jambo la busara zaidi kama utafuta mawazo ya kuomba "UONGOZI"- Kwani uongozi ni ujasiri ukiwa mwoga kila siku unaowaongoza watadhurika
http://www.globalpublishers.info/video/bado-nataka-kuishi-mkapa source GPL