Kauli ya Magufuli kuwa Kabudi na Lukuvi hawatagombea Urais haikuwa ya ghafla, ilipangwa siku nyingi na ndio mwanzo wa mgogoro ndani ya CCM

Hapana Mkuu. Hata Mkapa ambaye alikuwa ni rafiki mKubwa wa Magufuli, labda aliona mapungufu fulani ndani ya Magufuli hivyo hakumpa support yote ili kwenye mio za uraisi. Labda pia Mkapa hakutaka kugombana na Kikwete. Ndio maana Magufuli alisema wazi siku zote - hakuna anaemdai katika kuwa kwake raisi, ni juhudi zake peke yake.

Na labda kwa hasira ya Mkapa kutokuwa nae kwenye harakati a kumrithi Kikwete, Magufuli alipokuwa rahisi alikuwa hasikilizi chochote Mkapa alichomshauri. Na wala alikuwa ham-consult. Watu walianza kumlaumu Mkapa kuwa mtu wako Magufuli haambiliki, uwe unamshauri. Mkapa aliweka bayana kwamba hata yeye Magufuli hataki kabisa kumsikiliza, japo ni kweli yeye ndio aliyemfanya afike alipofika.

Ilifikia wakati Mkapa alikasirika akawa hahudhurii function yeyote ya kitaifa.Aliamua kukaa kando kabisa na mambo ya serikali, kama amesusa. Watu wenye busara wakamwambia Magufuli kwamba umeenda mbali sana na Mkapa, mwombe msamaha, huwezi kusahau mlikotoka. Nadhani katika maisha yake Magufuli ya uraisi, ni ushauri huo tu aliowahi kupokea, maana ni kweli alimalizana na Mkapa na Mkapa akawa anashiriki dhifa za kitaifa baada ya hapo.
Magufuli kawekwa na Mkapa, usiwe mbishi.

 
Magufuli kawekwa na Mkapa, usiwe mbishi.
Mkapa alimwekaje Magufuli kwenye uraisi wakati unajua kila kilichotokea? Kumwambia akachukue form za uraisi? Magufuli kuwa raisi ni juhudi yake na Kikwete wala hakuwa na mpango nae kwenye list yake ya mfukoni. Bila mgongane kati ya Membe mtu wa Kikwete na Lowassa Magufuli asingekuwa raisi
 
Kwa jinsi navyoona kuna uwezekano mkubwa Rais ajaye akawa ni Mwanamama. La hasha Rais atatokea Zanzibar, iwapo rais atatokea CCM.

Kuhusu Rais kutokea Zanzibar, ni suala la Legacy. Ukiangalia mfumo wa uongozi na utawala anaotumia Magufuli unaendana na maono ya mzee Nyerere.

Wakati Nyerere anang'atuka alituachia Mzee Mwinyi wa Zanzibar. Hivyo bila shaka na huyu mtawala atatuachia Mzanzibar Mwengine.

Ikishindikana na kukawa na vita kali kati ya vijana wafuatao CCM, Makamba, Jafo, Mwigulu, Kigwangala, Bashe, na Ndugai. Basi maajabu ya mwanamama kupitishwa na mkutano mkuu wa CCM kwa shinikizo la Mwenyekiti wao.

Above all, Tunaweza kuwa na Rais ambaye hatokani na Baraza la mawaziri kwa mara ya kwanza. Mheshimiwa anaweza kuamka na kuleta jina la mfukoni. Hapa tunaweza kuletewa Mkuu wa mkoa au Katibu wa wizara kama mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM.

Kama hujanielewa. Ki ufupi namaanisha Magufuli hasomeki.
Ngoja Dotto wa Wizara ya Fedha mtoto wa dada yake Magufuli aje awe raisi ajae ndio tutaelewa maana ya kunyooshwa!
 
Ina maana hao wajanja waliomwondoa Sokoine kimaajabu April 1984 walishajua mapema kwamba Nyerere alikuwa na mpango wa kung'atuka Novemba 1985?
Yes, Nyerere alifanya liwe wazi sana kwamba alitarajia Sokoine awe mrithi wake. Tatizo Sokoine alikuwa mkali saa, na ni kweli kuna wakati altaka kuwaweka ndani mawaziri kwa makosa ya uhujumu uchumi.

Sokoine hata alikuwa na wazo kwamba ikiwa serikali iligharamia elimu hadi chuo kikuu, basi ukimaliza chuo kikuu usipewe vyeti bali upangiwe kazi na serikali, kwa kuwa watu wakipewa vyeti wengine walikuwa wanaenda nje au private sector kfanya kazi, na Sokoine alichukizwa sana na hilo na kuona ni kuiibia serikali. Wakati huo kuanzia form four hadi chuo kikuu, ukimaliza ulipangiwa kazi na serikali.
 
Yes, Nyerere alifanya liwe wazi sana kwamba alitarajia Sokoine awe mrithi wake. Tatizo Sokoine alikuwa mkali saa, na ni kweli kuna wakati altaka kuwaweka ndani mawaziri kwa makosa ya uhujumu uchumi.

Sokoine hata alikuwa na wazo kwamba ikiwa serikali iligharamia elimu hadi chuo kikuu, basi ukimaliza chuo kikuu usipewe vyeti bali upangiwe kazi na serikali, kwa kuwa watu wakipewa vyeti wengine walikuwa wanaenda nje au private sector kfanya kazi, na Sokoine alichukizwa sana na hilo na kuona ni kuiibia serikali. Wakati huo kuanzia form four hadi chuo kikuu, ukimaliza ulipangiwa kazi na serikali.
Kama ingefanyika hivyo wale ambao wangefanya kazi kwenye sekta binafsi wangetoka nchi gani?
 
Yes, Nyerere alifanya liwe wazi sana kwamba alitarajia Sokoine awe mrithi wake. Tatizo Sokoine alikuwa mkali saa, na ni kweli kuna wakati altaka kuwaweka ndani mawaziri kwa makosa ya uhujumu uchumi.

Sokoine hata alikuwa na wazo kwamba ikiwa serikali iligharamia elimu hadi chuo kikuu, basi ukimaliza chuo kikuu usipewe vyeti bali upangiwe kazi na serikali, kwa kuwa watu wakipewa vyeti wengine walikuwa wanaenda nje au private sector kfanya kazi, na Sokoine alichukizwa sana na hilo na kuona ni kuiibia serikali. Wakati huo kuanzia form four hadi chuo kikuu, ukimaliza ulipangiwa kazi na serikali.
Msingi wa kukuza uchumi huwezi kuepuka private sector.

Private sector inatoa ajira kwa Watanzania kama wana sifa.

10% ya michango ya NSSF inatoka waajiri (Private sector) 10% kwa waajiriwa wa (Private sector kupitia mishahara) ndio msingi wa michango ya NSSF.

18% ya manunuzi ya bidhaa na huduma yanayofanywa na private sector yanaingia serikalini kama VAT. Hayo ni makato ya Opex (operating cost)

30% ya net profit ya kampuni binafsi inakatwa kama corporate tax.

Usoshalist hauna maana ya kila kitu kufanywa na public sector au kila mtu aliesomeshwa kwa mkopo wa elimu ambao ataurudisha baada ya kuajiriwa.

Sidhani kama Sokoine alikuwa short sighted kiasi hicho.

Ila kwa sasa; kama JPM anataka kukuza tax base; TIC na TIB Bank zifanye kazi kimkakati ili kukuza private sector inayozalisha bidhaa na huduma ambazo kwa asilimia kubwa tuna import.

Na uzalishaji uwe na excess ili tuki-export tuwe na surplus ya balance of trade and balance of payment.

Imetosha ku-operate kwenye deficit on balance of trade and balance of payment.

Time is now
 
Siku Magufuli alipotamka hadharani kwamba Kabudi na Lukuvi hawatagombea Urais kwa sababu ya umri wao mkubwa, wengine walicheka wakiichukulia kama ni kauli ya ghafla. La hasha, hii ilikuwa ni kauli ya kimkakati ambayo Magufuli alikuwa ameitafakari na kupanga kuisema kabla hata ya kuingia Uchaguzi Mkuu.

Ni kauli ambayo iliwashangaza sana Kabudi na Lukuvi, kuwashitua, kuwakatisha tamaa na hatimae kuwaudhi sana. Ilibidi tu wajichekeshe mbele za watu.

Magufuli ameitoa kauli hiyo akiwa amesoma wazi nia za Kabudi na Lukuvi kutaka kuwa Marais wajao. Ukiangalia kwa makini, Kabudi na Lukuvi wamekuwa waaminifu sana kwa Magufuli, wakiwa nyuma yake kwa 100%, wakimpamba kila wanapopata nafasi, na lengo lao ilikuwa kupata kuungwa mkono na Magufuli ili kuwa Rais awamu ifuatayo. Kuna wakati mtu kama Kabudi anajitoa kabisa maarifa na akili (wisdom and intelligence) ili mradi tu ajiweke upande wa Magufuli na Magufuli amuone ndio Waziri anaefaa kuwa Rais ajaye.

Sasa kwa kauli hii Magufuli amefanya kosa kubwa sana. Ametangaza vita na mgogoro ndani ya CCM katika suala la Rais atakaemrithi. Magufuli ameshaanza kumpigia debe "kijana" anaetaka amrithi, kijana ambae Magufuli ataweza kumtawala (kum-influence) kirahisi wakati amemaliza awamu hii. Na watu wanajua ili Magufuli awe na "mrithi" wa kumtawala, lazima awe ni kijana wake mtiifu kabisa kama vile Makonda, au kijana wa kutoka kanda ya ziwa.

Sasa ndani ya CCM kuna watu wameanza kuliona hilo na hawataki kabisa! Kuna watu wanaona Lukuvi au Kabudi ndio Mawaziri "wenye hekima na busara" wanaofaa kumrithi Magufuli.

Magufuli amekuwa na haraka mno kuanzisha vita ya wa Rais ajae, akidhani kuwakatisha tamaa mapema Kabudi na Lukuvi itasaidia kuwaondoa uwanja wa mapambano. Magufuli alipaswa ajifunze toka kwa Kikwete, ambaye alijua kabisa Mwandosya alitaka kuwa kumrithi kiti cha Urais, na Kikwete akajifanya kumuunga mkono Mwandosya hadi dakika za mwisho kabisa ndio akatoa majina yake mfukoni. Mwandosya akawa amepigwa knock out kwa " sucker punch" hakuamini betrayal ya Kikwete! Sidhani hata kama hata wanasalimiana hadi leo. Kikwete mtoto wa mjini, Magufuli mtu wa kuja, ndio tofauti zao.

Sasa athari za Magufuli kuonyesha karata zake mapema ni kwamba ile support aliyopata toka kwa Kabudi na Lukuvi katika awamu ya kwanza hataipata tena! Hilo ndilo kosa kubwa Magufuli amefanya. Sasa Kabudi na Lukuvi hawatampta tena ile 100% waliyompa huko nyuma. Kibaya sana kinachoweza kutokea ni kwamba wataunda makundi yao ndani ya CCM ya kuwa support, lengo likiwa kupanda mbegu ndani ya watu wa CCM kwamba Magufuli ni kiongozi asie na hekima hata kumuunga mkono juu ya chaguo lake la Rais ajae itakuwa ni kosa kubwa!

Kwangu mimi, Hotuba ya Kabudi aliyotoa kwa wafanya kazi wa mambo ya ndani ina kila namna ya viashiria kwamba ameanza mapambano na kujitofautisha ili watu waone anaweza kuwa Rais wa namna gani!

Yajayo ndani ya CCM yatafurahisha sana. Mpambano ndio kwanza unaanza!
Mnaongea nini nyie mnazungumzia mende!! Lukuvi na Kabudi?ni akina nani nchi hawa ni kama Ndanda na Majimaji acheni dharau kwa nchi hii, ongea kuhusu, Jaffo, Mbarawa, Hussein Mwinyi (uhakika kbsa), Majaliwa kwa mbali na Mama Samia, Bashiru acheni Utopolo
 
Kabudi is very very intelligent. Anajua kujishusha ili akwezwe. Hivyo hiyo yote ni strategy. Nimewahi kuwa na Kabudi. He is very calculating. Hivi unaona mtu kama Kabudi kusema yeye ni mtu wa jalalani inaendana na profiling yake ya kuwa presumptuous, flamboyant, cocky na pompous? Anasema hivyo ili kujijenga. Ni strategy ili kumpa confidence Magufuli kuwa ni kitwana wake na pia kuwafanya watu waone ni mnyenyekevu sana. Ndio maana nikasema Kabudi anaweza kujitoa akili na maarifa (wisdom and intelligence) kwa muda mfupi ili kutimiza lengo la muda mrefu.
Kabudi yuko pompous sana, ana kariri kwingi kuliko kuelewa.
 
nionavyo mimi hao watu wawili ndio wagombea wao wanaowaandaa,mwenyekiti aliongea vile hadharani ili kuwaepusha na mashilawadu (wasifuatwefuatwe)

naona ile kauli kama mkakati kabambe kabisa

time will tell
 
Mnaongea nini nyie mnazungumzia mende!! Lukuvi na Kabudi?ni akina nani nchi hawa ni kama Ndanda na Majimaji acheni dharau kwa nchi hii, ongea kuhusu, Jaffo, Mbarawa, Hussein Mwinyi (uhakika kbsa), Majaliwa kwa mbali na Mama Samia, Bashiru acheni Utopolo
Wewe lazima unatoka Zanzibar
 
Kauli hii ya Magufuli imeweza, kwa makusudi au kwa bahati tu, kuwapumbaza Watanzania wengi kutoka kwenye hoja ya kuangalia taasisi ya urais na mabadiliko ya kimfumo inayoyahitaji, kama vile mabadiliko ya katiba kupunguza nguvu za urais, kwa rais yeyote ajaye, na kuwapeleka kwenye viroja vya kujadili nani atakuwa rais.

Mwalimu JK Nyerere, katika mkutano wa waandishi wa habari kujadili sifa za rais atakayetufaa, mwaka 1995, Kilimanjaro Hotel, aliulizwa na muandishi wa habari maoni yake kuhusu Augustine Mrema. Mgombea wa NCCR Mageuzi aliyekuwa akiwika sana wakati huo.

Mwalimu Nyerere, kwa busara zake, alikataa kuongelea watu. Alisema hajaja pale kwenye mkutano kuongelea mtu. Na kama waandishi walifikiri kaja kuongelea mtu, angefungasha virago na kuondoka zake.

Mwalimu alisema alienda pale kuzungumzia sifa za mgombea safi.

Alielewa tofauti ya kujadili mtu na kuujadili urais kimfumo. Alielewa tofauti ya kumjadili mtu na kujadili sifa za rais anayefaa.

Siasa za Afrika zinajikita kwenye kuangalia watu, badala ya kuangalia mifumo.

Mpaka leo wengi hatujajifunza somo alilofundisha Mwalimu Nyerere Kilimanjaro Hotel mwaka 1995.

 
Kauli hii ya Magufuli imeweza, kwa makusudi au kwa bahati tu, kuwapumbaza Watanzania wengi kutoka kwenye hoja ya kuangalia taasisi ya urais na mabadiliko ya kimfumo inayoyahitaji, kama vile mabadiliko ya katiba kupunguza nguvu za urais, kwa rais yeyote ajaye, na kuwapeleka kwenye viroja vya kujadili nani atakuwa rais.

Mwalimu JK Nyerere, katika mkutano wa waandishi wa habari kujadili sifa za rais atakayetufaa, mwaka 1995, Kilimanjaro Hotel, aliulizwa na muandishi wa habari maoni yake kuhusu Augustine Mrema. Mgombea wa NCCR Mageuzi aliyekuwa akiwika sana wakati huo.

Mwalimu Nyerere, kwa busara zake, alikataa kuongelea watu. Alisema hajaja pale kwenye mkutano kuongelea mtu. Na kama waandishi walifikiri kaja kuongelea mtu, angefungasha virago na kuondoka zake.

Mwalimu alisema alienda pale kuzungumzia sifa za mgombea safi.

Alielewa tofauti ya kujadili mtu na kuujadili urais kimfumo. Alielewa tofauti ya kumjadili mtu na kujadili sifa za rais anayefaa.

Siasa za Afrika zinajikita kwenye kuangalia watu, badala ya kuangalia mifumo.

Mpaka leo wengi hatujajifunza somo alilofundisha Mwalimu Nyerere Kilimanjaro Hotel mwaka 1995.


MKuu umeongea pointi nzuri sana! Nyerere angekuwapo Magufuli asingekuwa raisi, au angekuwa raisi wa awamu moja tu - anachapa kazi sana, lakini hana sifa za kuwa raisi
 
Back
Top Bottom