Kauli ya Kinana inaonyesha CCM imechoka amani

nahavache

JF-Expert Member
Apr 3, 2009
871
246
Kinana: Hatuungi rasimu ya katiba kwa 100%. Hii ni kauli ya Kinana kama ilivyoandikwa na magazeti mengi ikiwemo lile la Nipashe. In fact, ameitisha kikao cha CC kujadili rasimu hii na kutoa msimamo.

Kwa kauli kama hii, ina maana kuwa ama anakataa maoni ya wananchi kwa asilimia 100 ambao ndio waliyatoa na yakafanyiwa uchambuzi na kuwekwa kwenye summary ikatoka hii rasimu, au ana maana kuwa wajumbe wa kuandika rasimu hii walitoa yao moyoni wakaandika bila kufuata maoni ya wananchi. Mimi sidhani kuwa wajumbe wa katiba walitoa yao kichwani, hapana bali walifanya uchambuzi wa yale ambayo ni maoni ya wananchi. Hivyo, kauli ya Kinana kuwa kwa asilimia 100 % CCM inaipinga rasimu hii maana yake kubwa ni kuwa CCM haitaki maoni ya wananchi na hivyo inataka mambo yaendeshwe kama anavyojua yeye Kinana na sio maoni ya wananchi. Hii ni dharau kubwa na udikiteta wa hali ya juu.
CCM hasa Kinana anajua kuwa kwa rasimu hii, wananchi wanakuwa washirika wakubwa katika kujiamulia mambo yao ndio maana wana uwezo wa kumpumzisha mbunge ambaye hafanyi yale waliyomtuma bungeni. Hii inajuikana kabisa kuwa, wabunge wa CCM wengi kwa sababu mara nyingi bungeni wameonekana kuwa hawawakilishi wanachi bali wanawakilisha chama. Hii rasimu inaongeza uwajibikaji wa wabunge kwa sababu, mbunge anaweza akafukuzwa chama na akaendelea kuwa mbunge. Ina maana kuwa watu kama Filikunjombe hawataogopa tena kuikosoa serekali wakihofia kufukuzwa chama. Hivyo ni dhahiri kuwa kuna uwezekano mkubwa wa wabunge wa CCM wakawa mwiba kwa CCM yenyewe kwa manufaa ya wananchi.
Kauli ya Kinana inaonyesha dhahiri kuwa CCM inataka kuendeleza udikiteta na hivyo isipopingwa vikali, inaweza ikaleta machafuko nchini. Kumbuka, wajumbe pale ambao wanaegemea upande wa CCM ni kama 80 % ya wajumbe wote ikiwa ni pamoja na mwenyekiti, mwenyekiti msaidizi na katibu. Na bado ushaihidi uliotolewa na Tundu Lissu bungeni unaonyesha ukaribu wa tume kwa mwenyekiti wa CCM. Bado Kinana anasema haikubali kwa 100%.

Waacheni wananchi waamue! Tumechoka kuamuliwa na watu wachache
 
  • Thanks
Reactions: mij
Watanzania tumejichelewesha wenyewe,CCM haiko tayari kuliendeleza taifa...hata hii katiba ni unafiki tupu,ccm haina dhamira ya dhati..
 
Hukumwelewa Kinana vizuri, kwa jinsi nilivyomsikia akisema ni kuwa hawapingani na rasimu ya katiba lakini yako maeneo ambayo hawayaungi mkono. Hakuwa tayari kuyasema maeneo hayo huku akisisitiza kuwa ni mapema mno kwani wanaendelea kuisoma rasimu hiyo. Ndipo alipoahidi kuwa ataitisha kikao cha Kamati kuu wajadili rasimu hiyo. Kila chama cha siasa, NGO, Taasisi za kidini, Taasisi za Elimu ya juu, wakulima, vyama vya wafanyakazi wote wana haki ya kuanza kuijadili rasimu hiyo. Sioni tatizo kwa CCM kuanza kujipanga mapema kupitia rasimu na kuangalia ni kwa namna gani watatoa mchango wao, vyama vingine vya siasa kama CDM,CUF,NCCR n.k navyo vikutane haraka iwezekanavyo ili vitoe misimamo yao kuhusu ni kipi wanadahani kina mapungufu kwenye rasimu hii. Misimamo yao ya mapema itatoa mwongozo kwa wajumbe wa mabaraza ya katiba (japo yanalalamikiwa kupatikana kwa njia isiyo halali) kujua ni mambo gani kwenye rasimu hii wayape kipaumbele kuyajadili.
 
Kinana: Hatuungi rasimu ya katiba kwa 100%. Hii ni kauli ya Kinana kama ilivyoandikwa na magazeti mengi ikiwemo lile la Nipashe. In fact, ameitisha kikao cha CC kujadili rasimu hii na kutoa msimamo. Kwa kauli kama hii, ina maana kuwa ama anakataa maoni ya wananchi kwa asilimia 100 ambao ndio waliyatoa na yakafanyiwa uchambuzi na kuwekwa kwenye summary ikatoka hii rasimu, au ana maana kuwa wajumbe wa kuandika rasimu hii walitoa yao moyoni wakaandika bila kufuata maoni ya wananchi. Mimi sidhani kuwa wajumbe wa katiba walitoa yao kichwani, hapana bali walifanya uchambuzi wa yale ambayo ni maoni ya wananchi. Hivyo, kauli ya Kinana kuwa kwa asilimia 100 % CCM inaipinga rasimu hii maana yake kubwa ni kuwa CCM haitaki maoni ya wananchi na hivyo inataka mambo yaendeshwe kama anavyojua yeye Kinana na sio maoni ya wananchi. Hii ni dharau kubwa na udikiteta wa hali ya juu. CCM hasa Kinana anajua kuwa kwa rasimu hii, wananchi wanakuwa washirika wakubwa katika kujiamulia mambo yao ndio maana wana uwezo wa kumpumzisha mbunge ambaye hafanyi yale waliyomtuma bungeni. Hii inajuikana kabisa kuwa, wabunge wa CCM wengi kwa sababu mara nyingi bungeni wameonekana kuwa hawawakilishi wanachi bali wanawakilisha chama. Hii rasimu inaongeza uwajibikaji wa wabunge kwa sababu, mbunge anaweza akafukuzwa chama na akaendelea kuwa mbunge. Ina maana kuwa watu kama Filikunjombe hawataogopa tena kuikosoa serekali wakihofia kufukuzwa chama. Hivyo ni dhahiri kuwa kuna uwezekano mkubwa wa wabunge wa CCM wakawa mwiba kwa CCM yenyewe kwa manufaa ya wananchi. Kauli ya Kinana inaonyesha dhahiri kuwa CCM inataka kuendeleza udikiteta na hivyo isipopingwa vikali, inaweza ikaleta machafuko nchini. Kumbuka, wajumbe pale ambao wanaegemea upande wa CCM ni kama 80 % ya wajumbe wote ikiwa ni pamoja na mwenyekiti, mwenyekiti msaidizi na katibu. Na bado ushaihidi uliotolewa na Tundu Lissu bungeni unaonyesha ukaribu wa tume kwa mwenyekiti wa CCM. Bado Kinana anasema haikubali kwa 100%. Waacheni wananchi waamue! Tumechoka kuamuliwa na watu wachache
Mwanga kama hana wa kumuwangia anawangia wanawe! Huyu ni ADUI no1 wa Taifa letu!
 
Watu makini hufanya maamuzi yao kwa pamoja sio kukurupuka kila mtu anasema lake huyu anaitisha press conference Kinondoni huyu yupo Dodoma huyu anaongea kwenye jukwa Arusha.

Hongera Kinana kwa kuonesha ukomavu.
 
Hukumwelewa Kinana vizuri, kwa jinsi nilivyomsikia akisema ni kuwa hawapingani na rasimu ya katiba lakini yako maeneo ambayo hawayaungi mkono. Hakuwa tayari kuyasema maeneo hayo huku akisisitiza kuwa ni mapema mno kwani wanaendelea kuisoma rasimu hiyo. Ndipo alipoahidi kuwa ataitisha kikao cha Kamati kuu wajadili rasimu hiyo. Kila chama cha siasa, NGO, Taasisi za kidini, Taasisi za Elimu ya juu, wakulima, vyama vya wafanyakazi wote wana haki ya kuanza kuijadili rasimu hiyo. Sioni tatizo kwa CCM kuanza kujipanga mapema kupitia rasimu na kuangalia ni kwa namna gani watatoa mchango wao, vyama vingine vya siasa kama CDM,CUF,NCCR n.k navyo vikutane haraka iwezekanavyo ili vitoe misimamo yao kuhusu ni kipi wanadahani kina mapungufu kwenye rasimu hii. Misimamo yao ya mapema itatoa mwongozo kwa wajumbe wa mabaraza ya katiba (japo yanalalamikiwa kupatikana kwa njia isiyo halali) kujua ni mambo gani kwenye rasimu hii wayape kipaumbele kuyajadili.

Unajua maana ya neno asilimia 100%??? Hivi wakiitisha kikao cha CCM wanaenda kuangalia nini katika rasimu hii? Simple logic ni kuwa wanaaenda kuangalia masilahi ya chama na wala sio masilahi ya wananchi kwa sababu wananchi wameshatoa maoni yao na wataendelea kutoa maoni kupitia mabaraza
 
Hongera warioba, hongera kwa kazi nzuri, kama ccm wanasema kazi yako siyo nzuri lakini watanzania tunakubali sana kazi yako. Usikubali kuyumbishwa na watu wachache, fanya kazi yako ili vizazi vya miaka hamsini ijayo vikukumbuke kwa mema utakayo kuwa umeifanyia nchi kwa kuleta katiba yenye tija kwa watanzania. Ubarikiwe sana warioba.
 
Kinana anaogopa Maamuzi MAGUMU yaliyojitokeza! Anataka yawe MEPESI, lakini tutakutana kwenye kura za maoni.
 
Ndugu NAHAVACHE, Uongo na unafiki wako umezidi, hakuna hata tone la dharau wala hayo unayoyasema, wewe ni mchochezi na ni mmoja wa lile kundi ninalotaka nchi isitawalike, Hutaweza na ujue fikira zako ni duni sana, kabebe mizigo bandarini, ndio kazi inayokufaa kwani umeshindwa kutumia ubongo uliopewa na mwenyezi Muungu. Hiyo Article uliyo inuku iko hapo chini kwa wana JF wote kuisoma. NAHAVACHE ni MCHOCHEZI HUYOOOOOOOOOOOO
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesema hakiungi mkono rasimu ya katiba mpya iliyozinduliwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba Jumatatu wiki hii kwa asilimia mia moja.

Chama hicho kimesema kuwa wiki ijayo kitatoa msimamo wake kuhusu rasimu ya hiyo iliyoandaliwa na tume hiyo iliyoongozwa Jaji Joseph Warioba.

Kauli hiyo ya chama tawala ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu wake, Abdulrahman Kinana, baada ya kuulizwa na waandishi wa habari kuhusu msimamo wa chama chake juu ya rasimu mpya.

Kinana alisema uamuzi wa kutangaza msimamo wa chama utatokana na kikao cha Kamati Kuu (CC), kitakachokutana Jumatatu ijayo chini ya mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete.

"Kwa sasa hatuungi mkono rasimu hii kwa asilimia 100 wala kuipinga mpaka hapo tutakapokaa CC wiki ijayo na kuamua msimamo wetu ni upi katika hili," alisema Kinana.

Alisema kila jambo ndani ya chama hicho huamuliwa kwa pamoja kupitia vikao na kwamba huo ndio utaratibu wao.

Miongoni mwa mambo ya msingi ambayo Tume ya Mabadiliko ya Katiba imeyapendekeza katika rasimu hiyo ni mfumo wa Muungano wa serikali tatu za Tanzania Bara, Zanzibar na Shirikisho.

Mfumo wa Muungano ni moja ya mambo ambayo serikali ya CCM imekuwa ikiyachukulia maamuzi kwa uangalifu mkubwa kwa kuwa ni sera ya chama hicho.

Hadi sasa sera ya CCM kuhusu Muungano ni mfumo wa serikali mbili za Muungano na ya Zanzibar.

Mapema miaka ya 90 suala la Muungano liliitikisa serikali ya awamu ya pili ya Alhaji Ali Hassan Mwinyi, ilijikuta katika mtikisiko mkubwa, baada ya kuridhia kuundwa kwa serikali ya Tanganyika ndani ya Muungano.

Uamuzi huo ulitokana na shinikizo la kundi la wabunge 55 maarufu kwa jina la G55 ambalo lilikuwa linapinga uamuzi wa Zanzibar kuamua kujiunga na Jumuiya ya Kimataifa ya Kiislamu (OIC) kinyume cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Baada ya Bunge kupitisha hoja hiyo na serikali kuridhia, Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere, aliingilia kati kwenye kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM na kuwaambia wabunge wakiokuwa wakishinikiza kuundwa kwa serikali ya Tanganyika kusitisha hoja hiyo au kujitoa ndani ya CCM.

Mwalimu aliongeza kuwa viongozi wa kitaifa walioshauri vibaya Rais Mwinyi wawakibike au wawajibishwe.

Aidha, alitaka CCM kwenda kwa wanachama kuwauliza maoni yao kuhusu mfumo wa Muungano wanaoupendekeza kwa maelezo kuwa sera hiyo haiwezi kubadilishwa bila kuwauliza wanachama.
Kufuatia uamuzi huo, NEC ilituma wajumbe katika maeneo mbalimbali ya nchi kukusanya maoni na wanachama wengi walisema wanataka mfumo wa serikali mbili uendelee.

Baada ya hapo aliyekuwa Waziri Mkuu na makamu wa kwanza wa Rais, John Malecela, aliondolewa katika nafasi hiyo na baadaye NEC ilimuondoa Hayati Horace Kolimba, katika nafasi ya ukatibu mkuu wa CCM.

Wakati wa uongozi wa awamu ya tatu wa Rais Benjamin Mkapa suala la mfumo wa Muungano liliibuka upya, lakini Mkapa alitumia nguvu kuzima mawazo ya kutaka serikali mbili.

Hata alipounda Tume ya kukusanya maoni chini ya uenyekiti wa Jaji Robert Kisanga kupitia utaratibu wa waraka maalum wa White Paper wa marekebisho ya katiba, Mkapa alikataa mapendekezo ya tume hiyo ya kupendekeza mfumo wa serikali tatu, akiwatolea lugha kali wajumbe wa tume kuwa hawakupewa adidu ya kutoa mapendekezo bali kukusanya maoni kuhusu Muungano.

Siala la mfumo wa Muungano huenda likazua mjadala mkubwa ndani ya CC kabla ya kutoa msimamo wa chama hicho.

TAMWA YALILIA HAKI

Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (Tamwa) kimewataka wajumbe wa Mabaraza ya Katiba kupigania kuondolewa kwa mapengo kuhusu haki za wanawake na watoto yaliyopo katika Rasimu ya Katiba ili kuleta haki, usawa na maendeleo nchini.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari jana na Mkurugenzi Mtendaji wa Tamwa, Valerie Msoka, mchango wa wananchi ndiyo nguvu ya pamoja inayohitajika kuondoa unyanyasaji wa kijinsia na sheria kandamizi kwa mwanamke na mtoto wa kike.

Alisema Tamwa inaipongeza Tume ya Mabadiliko ya Katiba kutoa rasimu, lakini rasimu hiyo haijaweka bayana misingi itakayomlinda mwanamke na mtoto wa kike dhidi ya vitendo vya ukatili vikiwamo ubakaji, ndoa za umri mdogo na ukeketaji wa watoto wa kike.

Aliongeza kuwa rasimu imeeleza haki za mtoto wa kike, lakini haijaweka bayana vipengele vya kumlinda ili kumwezesha kupata huduma za jamii ikiwa ni pamoja na elimu itakayomuwezesha kudai, kutetea na kumlinda dhidi ya ukatili wa kijinsia.

"Kuna ukimya pia kuhusu umri wa kuolewa, jambo ambalo linapelekea mtoto wa kike chini ya miaka 18 kuolewa kwa ridhaa ya wazazi au walezi wake," alisema Msoka.

Msoka alisema Rasimu hiyo imebainisha kuwapo kwa haki sawa katika nafasi za uongozi wa bunge, lakini kumekuwa na ukimya katika ngazi nyingine za uongozi kama vile katika vyama vya siasa, mawaziri, serikali za mitaa, mabalozi na makatibu wakuu.

Alisema kwa kufanya hivyo kutapelekea ushiriki sawa wa wanawake katika nyanja zote za uongozi.

Alisema rasimu hiyo inatoa haki ya mwanamke ya huduma ya juu ya afya inapopatikana, lakini haijabainisha haki za uzazi salama wala kuiwajibisha serikali kuwekeza katika afya ya uzazi pamoja na kumlinda mwanamke katika jukumu zima la uzazi.

"Ingawa Rasimu imezungumzia kuheshimiwa kwa mikataba ya kimataifa kuhusu haki za binadamu, imeshindwa kuweka bayana utekelezwaji wa Kitaifa wa mikataba ambayo Tanzania imetia saini," alisema Msoka.

Aliongeza kuwa katika kuleta mabadiliko yatakayoleta maendeleo nchini, fursa ya mabaraza ya kuiangalia rasimu ya katiba ni fursa ambayo itahakikisha kuondolewa kwa mapungufu yaliyopo ili kuwapo na usawa na haki kwa Watanzania wote.





CHANZO: NIPASHE



































 
Kinana anajjua alifanyalo kwa bulk huitaji kukurupuka. Mi binafsi naupenda mungano wa serikari moja tu zaidi ya hall malalamiko hhayataisha
 
Kinana: Hatuungi rasimu ya katiba kwa 100%. Hii ni kauli ya Kinana kama ilivyoandikwa na magazeti mengi ikiwemo lile la Nipashe. In fact, ameitisha kikao cha CC kujadili rasimu hii na kutoa msimamo.

Kwa kauli kama hii, ina maana kuwa ama anakataa maoni ya wananchi kwa asilimia 100 ambao ndio waliyatoa na yakafanyiwa uchambuzi na kuwekwa kwenye summary ikatoka hii rasimu, au ana maana kuwa wajumbe wa kuandika rasimu hii walitoa yao moyoni wakaandika bila kufuata maoni ya wananchi. Mimi sidhani kuwa wajumbe wa katiba walitoa yao kichwani, hapana bali walifanya uchambuzi wa yale ambayo ni maoni ya wananchi. Hivyo, kauli ya Kinana kuwa kwa asilimia 100 % CCM inaipinga rasimu hii maana yake kubwa ni kuwa CCM haitaki maoni ya wananchi na hivyo inataka mambo yaendeshwe kama anavyojua yeye Kinana na sio maoni ya wananchi. Hii ni dharau kubwa na udikiteta wa hali ya juu.
CCM hasa Kinana anajua kuwa kwa rasimu hii, wananchi wanakuwa washirika wakubwa katika kujiamulia mambo yao ndio maana wana uwezo wa kumpumzisha mbunge ambaye hafanyi yale waliyomtuma bungeni. Hii inajuikana kabisa kuwa, wabunge wa CCM wengi kwa sababu mara nyingi bungeni wameonekana kuwa hawawakilishi wanachi bali wanawakilisha chama. Hii rasimu inaongeza uwajibikaji wa wabunge kwa sababu, mbunge anaweza akafukuzwa chama na akaendelea kuwa mbunge. Ina maana kuwa watu kama Filikunjombe hawataogopa tena kuikosoa serekali wakihofia kufukuzwa chama. Hivyo ni dhahiri kuwa kuna uwezekano mkubwa wa wabunge wa CCM wakawa mwiba kwa CCM yenyewe kwa manufaa ya wananchi.
Kauli ya Kinana inaonyesha dhahiri kuwa CCM inataka kuendeleza udikiteta na hivyo isipopingwa vikali, inaweza ikaleta machafuko nchini. Kumbuka, wajumbe pale ambao wanaegemea upande wa CCM ni kama 80 % ya wajumbe wote ikiwa ni pamoja na mwenyekiti, mwenyekiti msaidizi na katibu. Na bado ushaihidi uliotolewa na Tundu Lissu bungeni unaonyesha ukaribu wa tume kwa mwenyekiti wa CCM. Bado Kinana anasema haikubali kwa 100%.

Waacheni wananchi waamue! Tumechoka kuamuliwa na watu wachache
Hili andiko nalipinga bila ya kuwa na shaka mimi mwenyewe nilimsikiliza kinana hakusema hivyo wandishi siku hizi wamepotoka,kinana aliongelea pande mbili kuwa hawataunga mkono wala kukataa kwa vile bado hawajaisoma pindi wakiisoma watatoa msimamo wa chama.
 
Hukumwelewa Kinana vizuri, kwa jinsi nilivyomsikia akisema ni kuwa hawapingani na rasimu ya katiba lakini yako maeneo ambayo hawayaungi mkono. Hakuwa tayari kuyasema maeneo hayo huku akisisitiza kuwa ni mapema mno kwani wanaendelea kuisoma rasimu hiyo. Ndipo alipoahidi kuwa ataitisha kikao cha Kamati kuu wajadili rasimu hiyo. Kila chama cha siasa, NGO, Taasisi za kidini, Taasisi za Elimu ya juu, wakulima, vyama vya wafanyakazi wote wana haki ya kuanza kuijadili rasimu hiyo. Sioni tatizo kwa CCM kuanza kujipanga mapema kupitia rasimu na kuangalia ni kwa namna gani watatoa mchango wao, vyama vingine vya siasa kama CDM,CUF,NCCR n.k navyo vikutane haraka iwezekanavyo ili vitoe misimamo yao kuhusu ni kipi wanadahani kina mapungufu kwenye rasimu hii. Misimamo yao ya mapema itatoa mwongozo kwa wajumbe wa mabaraza ya katiba (japo yanalalamikiwa kupatikana kwa njia isiyo halali) kujua ni mambo gani kwenye rasimu hii wayape kipaumbele kuyajadili.

Sasa yeye hayaungi mkono kama nani. Maana rasimu ni maoni ya wananchi, Kazi ya tume ilikuwa kuyachambua na kuyaweka katika utaratibu wa Kikatiba. Huyo amejichokea atafute pa kukimbilia, tumeonewa kiasi cha kutosha, tumepuuzwa kiasi cha kutosha, tumenyanyaswa kiasi cha kutosha, unyonge wetu ndio uliotufanya tuonewe, tunyanyaswe na kupuuzwa................(Mwl. J.K. Nyerere), Nia ya mabadiliko tunayo, sababu ya mabadiliko tunayo uwezo wa wa mabadiliko tunao. PEEEPOOOOOOOOOZ!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! POWERRRRRRRRRRRRRRRRRRRRRR
Tafakari
 
Kinana: Hatuungi rasimu ya katiba kwa 100%. Hii ni kauli ya Kinana kama ilivyoandikwa na magazeti mengi ikiwemo lile la Nipashe. In fact, ameitisha kikao cha CC kujadili rasimu hii na kutoa msimamo.

Kwa kauli kama hii, ina maana kuwa ama anakataa maoni ya wananchi kwa asilimia 100 ambao ndio waliyatoa na yakafanyiwa uchambuzi na kuwekwa kwenye summary ikatoka hii rasimu, au ana maana kuwa wajumbe wa kuandika rasimu hii walitoa yao moyoni wakaandika bila kufuata maoni ya wananchi. Mimi sidhani kuwa wajumbe wa katiba walitoa yao kichwani, hapana bali walifanya uchambuzi wa yale ambayo ni maoni ya wananchi. Hivyo, kauli ya Kinana kuwa kwa asilimia 100 % CCM inaipinga rasimu hii maana yake kubwa ni kuwa CCM haitaki maoni ya wananchi na hivyo inataka mambo yaendeshwe kama anavyojua yeye Kinana na sio maoni ya wananchi. Hii ni dharau kubwa na udikiteta wa hali ya juu.
CCM hasa Kinana anajua kuwa kwa rasimu hii, wananchi wanakuwa washirika wakubwa katika kujiamulia mambo yao ndio maana wana uwezo wa kumpumzisha mbunge ambaye hafanyi yale waliyomtuma bungeni. Hii inajuikana kabisa kuwa, wabunge wa CCM wengi kwa sababu mara nyingi bungeni wameonekana kuwa hawawakilishi wanachi bali wanawakilisha chama. Hii rasimu inaongeza uwajibikaji wa wabunge kwa sababu, mbunge anaweza akafukuzwa chama na akaendelea kuwa mbunge. Ina maana kuwa watu kama Filikunjombe hawataogopa tena kuikosoa serekali wakihofia kufukuzwa chama. Hivyo ni dhahiri kuwa kuna uwezekano mkubwa wa wabunge wa CCM wakawa mwiba kwa CCM yenyewe kwa manufaa ya wananchi.
Kauli ya Kinana inaonyesha dhahiri kuwa CCM inataka kuendeleza udikiteta na hivyo isipopingwa vikali, inaweza ikaleta machafuko nchini. Kumbuka, wajumbe pale ambao wanaegemea upande wa CCM ni kama 80 % ya wajumbe wote ikiwa ni pamoja na mwenyekiti, mwenyekiti msaidizi na katibu. Na bado ushaihidi uliotolewa na Tundu Lissu bungeni unaonyesha ukaribu wa tume kwa mwenyekiti wa CCM. Bado Kinana anasema haikubali kwa 100%.

Waacheni wananchi waamue! Tumechoka kuamuliwa na watu wachache

Nahisi umesoma tu title ta gazeti la Nipashe then umekuja JF moja kwa moja bila kusoma kwa undani iyo habari. Next time usiishie kusoma title bali check habari kwa umakini. Hiyo ni title ya kuuzia gazeti, ukienda ndani zaidi amesema kuna vipengele wanaunga mkono na vingine hapana kama suala la Muungano.

Pili CCM,CDM, CUF ni taasisi kamili usitegemee viongozi wa hivyo vyama watatoa kauli bila kuitisha vikao vyao vya ndani na kupata msimamo wa pamoja. So soon kila chama tegemea kitakuja na msimamo wake.Suala la CCM kuitisha kikao chake kisikutishe, vyama vingine navyo vitafuata, sasa wako busy kupitia iyo rasimu na kuja na msimamo wa vyama vyao.
 
awe amesema au hajasema, KInana ananini cha kujivunia katika kuchangia umoja na mshikamano wa taifa kama si zaidi ni propaganda na uchakachuaji wa kura, watanzania tuamke, hawa jamaa wanafanya haya mambo kwa manufaa yao na jamaa zao,
 
1. CCM Hatuungi mkono rasimu kwa asilimia 100 na

2. kwa asilimia 100 CCM inaipinga rasimu.

Ni mambo mawili tofauti, ni maneno yapi kayatumia kati ya hayo mawili.
 
kinacowakera ccm ni mgombea binafsi,wanajua akiruhusiwa mgombea binafsi lowassa atajitoa ccm,filikunjombe na sitta watafatia,hawa wataondoka na umati wa wanachama..mgombea binafsi ndio kifo cha ccm.Trust me on this.
 
Back
Top Bottom