Kauli ya Kakobe "Magufuli atubu", yaibua mambo! Je asili halisi ya Rais Magufuli ni Msukuma, Mhaya au Muha wa Kakonko?

Luck Star,
Ni kweli neno WALWA kwa kisukuma ni POMBE in Kiswahili na MAGUFULI ina maana ya KUFULI kwa Kiswahili na wingi wa KUFULI ni MAGUFULI......!!
Kwenye Kiswahili wingi wa kufuli si magufuuli.Wingi wa kufuli ni kufuli.
Umoja Wingi
Kufuli Kufuli
Kwa mfano somo sentensi hizi mbili hapa chini;
Umoja: Juma amenunua kufuli moja.
Wingi: Kesho Ana atanunua kufuli mbili kwa ajili ya milango miwili.
 
Nyamalagala,
You've said it all...!!!Naweza kuyaamini maneno yako kwa 99.99%....!!!!
Iliyobaki ni kujua huyu Baba wa Magufuli aliyeko Bukililo huko Kigoma asili yake ni wapi..??? Nina hakika trace back ya Mzazi wa Magufuli aliiyeko Bukililo atatuvusha mipaka kuingia aiidha RWANDA au BURUNDI.....!!!!
Hapa ndiipo hoja ya kwanini Magufuli alipoiingiia Ikulu tu nchi ya kwanza kuitembelea ni RWANDA...!!!!Kuna tetesi kwamba mfumo wa Utawala wa Magufuli ni Kagame style.....!!!
Lakinii pia kuna tetesi za hata ulinzi wa Magufuli una support ya mashushu kutoka kwa Kagame.......!!!!!
Ni wakti wa Watz kuamka na kuhoji uhalali wa URAIA(Kabila na asilii ya Mtu anayeomba nafasii yoyote ya uongozii kuanzia Balozii wa Mtaa mpaka Urais wa nchi yetu), otherwise tutaendelea kutawaliwa na Intarahamwe mpaka khiyama....!!!!!
Mmmh!
 
Wanabodi,

Hii ni thread ya swali lililotokana na ile kauli ya Kakobe kumtaka rais "Magufuli Atubu", yaibua mambo!. Kumeibuka watu wanaohoji asili halisi ya rais wetu Mhe. Dr. John Pombe Magufuli, baada ya member fulani humu kuibuka na hoja kuwa Magufuli sii Msukuma wa Chato, bali ni Muha wa Kakonko anakotoka Kakobe, sasa ukweli ni upi?. Jee rais wetu Magufuli ni Msukuma wa Chato, Mhaya wa Wazilankande au ni Muha wa Kakonko?. Japo ni bandiko kuhusu ukweli wa asili ya rais Magufuli, pia tutamuangazia kidogo Askofu Kakobe na hoja yake kumtaka rais Magufuli atubu, kama alichofanya ni kitu sahihi au laa!.

Declaration of Interest
Naomba kuanza na declaration of interest kuwa mimi Paskali Mayalla ni mwandishi wa habari wa kujitegemea, na kanuni kwanza ya kuu ya tasnia ya habari ni seek the truth, and tell nothing but the truth!. Kwa kabila ni Msukuma, na kwa vile tayari kuna hoja za ukabila na Usukumanaization, naomba kudeclare my interest kuwa mimi sio mkabila, na hili sio bandiko la kuhusu ukabila, bali ni bandiko la kuhoji ukweli wa kabila halisi la kiongozi wetu, kwa nia njema kabisa ya kuwa na info, kwa Imani kuwa hakuna ubaya wowote kwa raia wowote wa Tanzania, kufahamu kabila halisi na asili ya kiongozi wetu ili kwa kwa vile rais wetu amejinasibu kuwa ni wa kabila la Wasukuma, hixi kauli za kusema rais Magufuli sio Msukuma bali ni kabila Fulani, hii ikitokea kuwa ni ni kweli sii Msukuma kama anavyojisibu, then this has nothing do to with ukabila, but has something to do with uadilifu.

Turudi kwenye mada kuu
Jee Rais Magufuli ni Msukuma, Muhaya au Muha wa Kakonko?.
Siku za nyuma kuna member mwingine humu aliwahi kuibuka na kudai kuwa rais Magufuli sii Msikuma bali ni Muhaya, akaibuka hadi na jina lake halisi la Kihaya kuwa anaitwa Katto, tulipomuomba atufafanulie ukweli huu, aliingia mitini, sasa leo huyu Gungele naye anaibuka na yake kuwa rais Magufuli ni Muha wa Kakonko anakotoka Kakobe!, nimemuomba athibitishe, wakati tukisubiri uthibitisho huu, ndipo ninauliza, kuna ubaya wowote, Watanzania tukafahamisha kwa ukweli asili usio na chenga zozote jee rais wetu Dr. John Pombe Magufuli asili yake kabisa ni Kabila gani?.

Ili kupata majibu yakweli ya ya ukweli huu, tunaomba members wowote wa jf, wenye data za ukweli na uhakika kuhusu rais wetu watuletee kwa kuyajibu haya maswali simple
  1. Jee alizaliwa lini na wapi?.
  2. Wazazi wake halisi ni nani?.
  3. Asili ya wazazi hao ni wapi?.
  4. Ni kweli aliwahi kuitwa Katto?.
  5. Ilikuwaje akaibukia Chato?.
  6. etc, etc
NB. Hii tabia ya baadhi ya viongozi kubadili makabila na kutumia makabila mengine, haikuanza leo, ilianza tangu Enzi za Baba wa Taifa, watu walisema humu, hata Mkapa naye akasemwa ni wa kule..., Edward Lowassa inafahamika kwa wengi kuwa ni Mmeru, ila wazazi wake ndio walihamia Monduli, akazaliwa Monduli, akakulia Monduli, akalelewa Kimasai na kukua na morani wa kule, kwa kupitia hatua zote ikiwemo initiations, hivyo sasa yeye kweli ni Mmasai.

Hitimisho.
Rais Magufuli ni rais wetu, tumemchagua kwa kura zetu, yeye sio malaika bali ni binadamu tuu kama sisi, na hivyo kuweza kufanya makosa na hata dhambi, ila hakuna binadamu mwenye mamlaka ya kumhukumu binadamu mwingiwe kuwa ni mdhambi, ila sisi kama raia wema wa taifa letu, rais wetu anapofanya makosa ya wazi, tuko huru kumkosoa kwa heshima na staha, na kumueleza makosa yake au mapungufu yake ili ajirekebishe lakini sio kumhukumu kuwa ni mdhambi, na katika kuijua asili yake, kuna baadhi ya mambo ni mambo yake ya binafsi, na hatupaswi kuyaulizia ili tusiingilie his right to privacy, lakini kuijua asili yake, dini yake, kabila lake na jinsi anavyoendesha familia yake, jambo ni mambo binafsi, lakini sisi as taxpayers, we have the right to know details, his public as well as his private conduct haswa katika determination ya truthfulness ambayo ni ethical issue ni sifa kuu muhimu kabisa kuliko sifa zote za kiongozi wa nchi.
Jumatano Njema ya Kufungia Mwaka.
Paskali.
Rejea
Sumu ya Siasa za Udini, Ukanda na Ukabila, "Is It Real? au ni Dhana Tuu?."
Tuhuma za udini, ukanda na ukabila katika teuzi, kama wote wana sifa, kuna tatizo gani?.
Tuhuma Za Ukabila: Wasukuma Sii Miongoni Mwa Makabila Yenye Ukabila, Tatizo Ndio Walio Wengi!
Mtazamo: Kanda ya Kaskazini, CCM imechokwa mpaka basi!
Wito Kwa Bunge Letu Tukufu: Mkithibisha Hii Nepotism ya Ajabu na Zile Boeing ni TT, Then Hatufai!.
https://www.jamiiforums.com/threads...edeye-ni-bomu.570208/page-8n-hatufai.1246099/
Update 1
Haya ni baadhi ya majibu ambayo ambayo ni very objective na yana coherence, na kwakutumia uzoefu wangu wangu wa miaka 27 ya uandishi wa habari, naamini haya yasemwayo ni kweli kwa msingi tuu wa hearsay na third party contributions, confirmation itapatikana kutoka kwa ndugu wa karibu, wana ukoo, next of kin or from the horses mouth.






Kwa wenye karama ya upambanuzi, jamaa ana mama ila biological father hajulikani.
 
Mi sijaona kosa la kakobe, magufuli ni binadamu kama wewe na mimi, na binadamu tunatenda dhambi kwa hiyo ni lazima tutubu!!

Na mimi nasema magufuli anatakiwa atubu!!
Watanzania sasa tumesahau kuwa ili tuishi kwa amani inatupasa kuepuka maswala ya udini na ukabila!
Kumtaka Raisi wa nchi atubu kiuhalisia ni kumuambia yeye mwenyewe na mahakama wasihukumu, wafungwa waachiwe huru, aamuru kodi isitozwe, achukue mali zake agawane na maskini n.k. yote anayotakiwa kufanya yeye kama Mkristo.
Je, mnataka Raisi aongoze nchi kidini?
Watanzania hamuoni kuwa mnamuandama Magufuli tu?
Je, Maraisi waliopita mlisha washauri watubu dhambi zao hata baada ya kumaliza mda wao madarakani?
Ni nani alietuloga akili zetu Watanzania?
Kabla hamjamuandama Raisi mfikirie kwanza Tanzania kuna dini nyingi sana na makundi ya aina nyingi ambayo yana haki kimsingi.
Kama wewe una udini na ukabila hutanielewa.
 
Hata akitubu Mungu hawez msamehe mtu mkatili km yeye ,ye aendelee tu atapata kile kinachomstahili
Katika kusoma maandiko matakatifu sijaona mahali panaposema ukifanya dhambi hii hauta samehewa, ninavyofahamu kuna maandiko yanayosema hakuna dhambi isiyo sameheka kwa Mungu.
 
Katika kusoma maandiko matakatifu sijaona mahali panaposema ukifanya dhambi hii hauta samehewa, ninavyofahamu kuna maandiko yanayosema hakuna dhambi isiyo sameheka kwa Mungu.
Dhambi ya kukufuru hautosamehewa imeandikwa kwa biblia
 
Utawajua tu,watoro wa kipindi cha jografia...hivi kweli paskali hujui muingiliano wa watu katika eneo la biharamulo,geita,kibondo,na kahama?au umeandika tu.!
 
Ofisi ya Uhamiaji Mkoa wa Dar-Es-Salaam, imemwandikia barua Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), Askofu Zachary Kakobe, kumwita kwa ajili ya mahojiano.

Barua hiyo yenye Kumbukumbu Na. BA: 120/231/02/82 ya tarehe 5.4.2018, imemtaka Askofu Kakobe kufika katika ofisi hiyo, Jumatatu 9.4.2018 saa 4 asubuhi, na kuonana na Afisa Uhamiaji wa Mkoa wa Dar-Es-Salaam, ili kuhojiwa juu ya uraia wake.

Alipoulizwa kwa njia ya simu, Askofu Kakobe amethibitisha kupokea barua hiyo, na kusema kifupi tu kwamba, atakwenda kwenye mahojiano hayo.
Msikute Kakobe ameponzwa na baadhi ya hoja za kwenye bandiko hili.

P
 
Kazi ipo
IMG-20180408-WA0003.jpg
 
38 Reactions
Reply
Back
Top Bottom