jeviounipers
Member
- Jan 5, 2011
- 68
- 26
Mh. Mbowe kayasema haya leo mara baada ya kumalizika kwa mkutano mkuu maalumu wa kanda ya Nyasa katika ukumbi wa Igimbi mkoani Mbeya.
Mwandishi: Nini kauli yako juu ya kupotea kwa msaidizi wako Ben Saanane?
Mh. Mbowe: Mambo mengine yanapokua katika masuala ya kiuchunguzi sio kila jambo litasemwa hadharani wakati wote, na tunatambua jambo hili lina hatari, linahusu maisha ya mtu, sasa sio kila wakati kusema kuyarahisha.
Unaweza ukasema kumbe kwa kusema sana unawaruhusu na watesi wake pengine waweze kumtoa roho. Kwa hiyo kuna mambo mengine ni sensitive, siyo mambo ya kuzungumza rahisi sana. Tunafanya kazi kwa njia mbalimbali kama chama cha siasa na tunakuwa waangalifu sana kuhusiana na tuseme nini kwa wakati gani na kwa taratibu gani lakini kwamba chama kinafuatilia suala hili,
Kinawasiliana na vyombo mbalimbali. Chama kina vyombo vyake vingine vya ndani ambavyo vinafanya jambo hili lichunguzwe kwa makini.
Tuko hivyo na tunawahakikishia Wote kwamba muda muafaka ukifika tutaweza kutoa taarifa za kina tumekwamia wapi na nini kifanyike cha ziada.
Mwandishi: Mbona kama mwenyekiti umekua kimya sana kuhusu jambo hili kuliko kawaida yako, kulikoni?
Mh. Mbowe: Ah, sasa inategemea, hiyo ni tafsiri, kwa sababu chama ni taasisi sio mwenyekiti
Na mimi nilikua niko safari kwa muda mrefu. Nilikua ziara ya Ulaya wakati jambo hili likiendelea kwa muda wa wiki mbili na nusu. Nimerejea tu kama siku tano zilizopita na nikaja moja kwa moja kwenye ziara jana na juzi usiku. Lakini tunamaliza sasa jukumu hili la kwenda kwenye ziara tunaporejea majumbani kwa likizo hii ya krismasi tutapata mambo ya kujadiliana zaidi.
Lakini chama kama chama Kilikuwa kinawasiliana sana na familia wakati mimi niko safari.
Mwandishi: Nini kauli yako juu ya kupotea kwa msaidizi wako Ben Saanane?
Mh. Mbowe: Mambo mengine yanapokua katika masuala ya kiuchunguzi sio kila jambo litasemwa hadharani wakati wote, na tunatambua jambo hili lina hatari, linahusu maisha ya mtu, sasa sio kila wakati kusema kuyarahisha.
Unaweza ukasema kumbe kwa kusema sana unawaruhusu na watesi wake pengine waweze kumtoa roho. Kwa hiyo kuna mambo mengine ni sensitive, siyo mambo ya kuzungumza rahisi sana. Tunafanya kazi kwa njia mbalimbali kama chama cha siasa na tunakuwa waangalifu sana kuhusiana na tuseme nini kwa wakati gani na kwa taratibu gani lakini kwamba chama kinafuatilia suala hili,
Kinawasiliana na vyombo mbalimbali. Chama kina vyombo vyake vingine vya ndani ambavyo vinafanya jambo hili lichunguzwe kwa makini.
Tuko hivyo na tunawahakikishia Wote kwamba muda muafaka ukifika tutaweza kutoa taarifa za kina tumekwamia wapi na nini kifanyike cha ziada.
Mwandishi: Mbona kama mwenyekiti umekua kimya sana kuhusu jambo hili kuliko kawaida yako, kulikoni?
Mh. Mbowe: Ah, sasa inategemea, hiyo ni tafsiri, kwa sababu chama ni taasisi sio mwenyekiti
Na mimi nilikua niko safari kwa muda mrefu. Nilikua ziara ya Ulaya wakati jambo hili likiendelea kwa muda wa wiki mbili na nusu. Nimerejea tu kama siku tano zilizopita na nikaja moja kwa moja kwenye ziara jana na juzi usiku. Lakini tunamaliza sasa jukumu hili la kwenda kwenye ziara tunaporejea majumbani kwa likizo hii ya krismasi tutapata mambo ya kujadiliana zaidi.
Lakini chama kama chama Kilikuwa kinawasiliana sana na familia wakati mimi niko safari.