Kauli ya Chagulani dhidi Manyerere (Council Mwanza) ni sahihi kwa afya ya CHADEMA?

Chagulani namfahamu vizuri sana, ni rafiki yangu tokea tupo chuoni. Jamaa ANAJAZBA NA MAAMUZI YA HARAKA!
 
Hebu mliopo huko Rock city tupeni uhalisia halisi wa hili jambo kwa pande zote mbili bila upendeleo ili isije ikawa tunapoteza carolite zetu kujadili vitu humu kwa ajili self politcal interests za watu.
 
Uko wapi ukomavu wa kidemokrasia ikiwa tutaenedelea kuwabeba watu wenye personal interest kama Manyerere,lazima awajibishwe ili CDM isimamie dahana ya utawala bora kivitendo ikiwa ni kujipambanua hakun kilindana
 
Chadema mnashindwa kusimamia Jiji la Mwanza kweli mtaweza kulisimamia taifa letu la Tanzania.

Meya wa Mwanza ni Chadema.

Mbunge wa Mwanza ni Chadema.

Madiwani wengi wa Mwanza ni Chadema.

Halmashauri ya Jiji la Mwanza ipo chini ya Chadema.

Miradi yote ya Jiji la Mwanza inapitishwa na madiwani wa Chadema.

Leo hii Chadema hawapatani wenyewe kwa wenyewe, cha kuchekesha wakiulizwa tatizo nini wanasema ni CCM.

Chadema bado sana kwenye masuala ya kiutawala.
 
Ukweli kuwa tatizo linaweza kuwa ni CCM bado uko pale pale; HUJUMA, mbunge wetu amekatwa mapanga umesikia kesi hiyo ikiunguruma??? hakuna, tunajua ni hujuma. Mwanza haitayumba hata iweje, CCM haitakikani hata iwe giza au mwanga, engough is enough 50years +???? bado tu Chama kinataka utawala kwa lipi zuri wamefanya???? lipi nauliza???

Unasahau kuwa watendaji wote bado ni CCM, hujuma ni hoja kubwa na ya msingi hapa, mapato ya jiji yanashuka vipi? wakati watendaji ni wale wale wa CCM, Hujuma huioni???
 
This is a clear evidence that Chadema has a long way to go and 2015 is very near for this journey!
 
Hapa ndio naanza kuyaamini maneno ya mtu wa shoka Wassira.
 
Kimsingi Chagulani hajatumia busara hata kidogo na hakuma sababu ya msingi ya kumtetea Chagulani.

Kwanza huyu jamaa (Chagulani) kuanzia mwanzo wa mchakato wa uchaguzi wa meya 2010 alitangaza nia ya kugombea umeya lakini ilishindikana kwa hiyo bado ana chuki binafsi na meya wa sasa (Manyerere)!

Pili, kwenye mchakato wa kumpata meya 2010 huyu Adam Chagulani na diwani wa Kitangiri Matata na diwani mwingine wa CHADEMA viti maalum walipewa hela kutoka CCM ili wampigie mgombea wa CCM kura badala ya mgombea wa CHADEMA lakini busara za viongozi wa CHADEMA taifa ndo zilisaidia. Kwa hiyo zile pesa za CCM bado zinamsumbua Chagulani kwa sababu hawakuzirudisha mpaka leo.

Tatu, ninaamini kuwa Chagulani ameongezwa hela na wana CCM ili kukivuruga CHADEMA Mwanza kwa sababu Chagulani na Matata wameanza bifu za ajabu ajabu dhidi ya meya na Wenje bila sababu za msingi! Kama meya ana matatizo au mapungufu na meya ni wa Chama chake (Chagulani) kwa nini asitumie vikao halali vya chama kwanza kumpinga meya kuliko kukurupuka?

Naamini Chagulani ameingizwa mkenge na CCM na asipoangalia atapotea kwenye ramani ya siasa na kuhusu kutokuwa na imani na meya hatofanikiwa kamwe na hata akifanikiwa yeye hawezi kupata umeya kamwe kwa tabia zake hizi!
 
Chadema mnashindwa kusimamia Jiji la Mwanza kweli mtaweza kulisimamia taifa letu la Tanzania.

Meya wa Mwanza ni Chadema.

Mbunge wa Mwanza ni Chadema.

Madiwani wengi wa Mwanza ni Chadema.

Halmashauri ya Jiji la Mwanza ipo chini ya Chadema.

Miradi yote ya Jiji la Mwanza inapitishwa na madiwani wa Chadema.

Leo hii Chadema hawapatani wenyewe kwa wenyewe, cha kuchekesha wakiulizwa tatizo nini wanasema ni CCM.

Chadema bado sana kwenye masuala ya kiutawala.

mbona nyie wenye dhamana maeneo mengi nchini mmeshindwa kwa miaka 50? Ama kweli nyie wadini hamuoni kundule.
 
Wewe Ghost Rider inaonekana uko Mwanza, tunaomba utupe representation yako binafsi, Utendaji huyu Manyerere unauonaje????
 
Mi nadhani hoja ya msingi hapo ni madhaifu ya huyo meya na jinsi anavyokigharimu chama katika siasa za kanda ya ziwa!!!

Ni sahihi kumpigia kura ya kutokuwa na imani anatuchelewesha sana, pia alionyesha kutokuwa na uwezo toka mwanzo na akawapa waandishi wa habari ya kusema.

Hilo la makundi sijui ila naona kuna hoja za msingi tu katika kuzingatia usimamizi na kuonyesha uongozi wa manispaa, huyo meya wa saiv kashindwa sana kwa kweli.
Nikisimama kutoka kwenye maelezo yako, maoni yangu ni kwamba watanzania tuwe makini sana, hawa viongozi wa CHADEMA ni binaadamu na wanaweza kukosea kama wanavyofanya viongozi wa Magamba, tunachotakiwa kusimamia ni Mabadiriko na Uwajibikaji, kama kiongozi haridhishi katika utendaji wake sioni sababu ya kumtetea eti kwa vile ni CHADEMA, hizi ni tabia typical kabisa za CCM.

Mtu analalamikiwa kwamba anawazingua kwenye uendeshaji wa vikao vya halmashauri anaiubuka mtu na kuulizia juu ya afya ya chama, nani amesema kwamba vikao vya Halmashauri ni vikao vya CHAMA.

CHADEMA msiwe wepesi wa kusahau, Hakuna mtu analichukia jina la CCM wala rangi za Kijani na Njano, watu wanachukia uongozi wao Mbovu, hata nyie mkituletea uongozi mbovu tutawapitisha katika tanuru lile lile hata nyie sio mama yetu.

Uongozi wa CHADEMA mkoa unatakiwa kumuwajibisha huyu Manyerere haraka kama anauzembe, you have to walk the talk.
 
Kimsingi Chagulani hajatumia busara hata kidogo na hakuma sababu ya msingi ya kumtetea Chagulani!

Nadhani katumia jukwaa husika kwani issue ni juu ya uwezo wa kutawala jiji, Kuzungumzia kwenye chama siyo mahali pake.

Vinginevyo hatuna sababu ya kulalamika juu ya wabunge wa CCM wanaposhindwa kuzungumzia madudu ya serikali kisa ni ya chama chao. Yaani kila baya ya serikali wabunge wakalisemee kwenye vikao vya CCM? ndo demokrasia tunayoitaka?

Juu ya ukweli wa hoja zake hapo ndo awajibishwe kama inaonekana amehongwa kama wanavyosema watu lkn platform aliyotumia ni sahihi.
 
Leo tulikuwa kwenye mkutano wa hadhara Igoma, mkutano ulioitishwa na diwani Igoma (CHADEMA) Mh. Adam Chagulani kuelezea juu ya mchakato wa kukusanya kura za kutokuwa na imani na meya wa jiji la Mwanza Mh. Manyerere.

Kwa mujibu wa maelezo ya Chagulani juu sababu ya kutokuwa na imani na meya nimegundua kuwa Chagulani hana jipya na anatumiwa sana na CCM. Amezungumza siri nyingi sana za CHADEMA bila aibu mbele umati wa watu waliokuepo kwenye ule mkutano na kila mtu ametoka pale akilalamika na kumlaumu Chagulani. Na amemshutumu sana Mh. Wenje - mbunge wa Nyamagana (CHADEMA) bila kufuata taratibu za kichama. Kiujumla ni kwamba Chagulani hana jipya, hana ushirikiano na mahusiano mazuri na viongozi wa CHADEMA Mwanza!

Hata asiponyang'anywa kadi ni wazi kuwa 2015 hana chake tena Igoma.

- JACADUOGO (Mwenyekiti wa WANARORYA WOTE popote walipo)!
 
Mwacheni afanye upumbafu aone ujira wake!
Ccm inamtumia kama pepeta, kuivaa kazi, kuivua kazi.
 
Njaaa dhiki inaua watz,,, anatukana wakunga wakati uzazi ungalipo..... watz hakuna mzalendo atayetufikisha kokote,
 
Back
Top Bottom