Kauli tata za Rais Magufuli: Wabunge wa Kagera mko wapi?

Baija Bolobi

JF-Expert Member
Feb 25, 2009
1,093
1,726
Ni siku takribani nne tangu Mkuu wa nchi awasute, awakejeli na kuwadharau watu wa mkoa wa Kagera.

Ule haukuwa utani kwa sababu Mkuu yule si mtani wa watu wa Kagera. Zaidi sana, maneno yale yanafanana sana maneno aliyoyasema huko Wilayani Misenyi. Ukitilia maanani kuwa imemchukua miezi mitatu kwenda Kagera kuwapa pole ya tetemeko, ni wazi kuwa Mkuu alimaanisha alichokisema siku hiyo, yaani "Kagera nao wamezidi - Ukimwi, Mnyauko, Tetemeko, katerero, Kiterangoma, n.k". Haya si maneno ya kuwaambia watu walio katika shida, ukiacha mbali kitendo cha serikali kukusanya misaada kwa kutumia shida zao, kisha kuzitumia kwa kazi nyingine.

Najiuliza yafuatayo:
- Wabunge wa Mkoa wa Kagera wanamwakilisha nani?
- Je, wana msimamo gani juu ya kauli hizi za Mkuu wa nchi dhidi ya wananchi waliowachagua wao?
- Wao wakiwa wananchi wa Kagera, nao ni sehemu ya majanga hayo ya "kujitakia"?

Bila kusubiri majibu yao kwa maswali hayo, nawashauri yafuatayo:
- Wamtake Mkuu wa nchi hadharani, aombe radhi na maisha yasonge mbele, akikataa,
- Wajiuzuru kuonyesha kutoridhishwa na kauli za udhalilishaji kwa wananchi waliowachagua,
- Mbali na wabunge, viongozi wote wa kijamii mkoani Kagera walaani kauli hizi
- Wateule wote wa Rais watokao Kagera mahali popote, wajiuzuru kupinga udhalilishaji huu
- Madheheb yote ya dini, yaitishe sala maalum kumwomba Mungu awafanyie wepesi wana Kagera ili waepushe na majanga haya ambayo Mkuu amesema yamezidi kwa Kagera

--/Baija
 
Wale wala hawajitambui na sijuhi ni kwanini huwa wanashinda ubunge kwani kusema kweli, wale si 'wenzetu' hata kidogo. Na hawawezi kuungana kwani wao wenyewe hawathaminiani pia, kila mmoja anajiona yeye anaweza.

Mwangalie Jasson Rweikiza, hivi huyu ni mtu anayeweza kuitwa mwakilishi wa watu kweli? Ni lini uliwahi kumwona akishughurika na matatizo ya watu kama si wakati wa chaguzi, very hopeless. Yuko busy na shule zake St. Anne Marie dar na Sunshine kibaha, yuko busy na shule yake ya Rweikiza kyetema.

Hawa watu wa hivi ni kupoteza mda bure na hawezi kuwa na msaada, ni afadhari kidogo Mama Tibaijuka na Dr. Diodorus, hawa wengine tumekula garasa. Si Lwakatare na wala si yule wa Karagwe ama Biharamulo, wote ni majokeri
 
Iv wewe umetoka wap et wajiuzulu ubunge acha utan bas hii njaa mtaani huioni had unawashauli wenzako wajiuluzulu njaa ni kitu kingine wewe
 
Rweye,

Nakubaliana na wewe kuhusu Rweikiza na shule zake ingawa umeiacha Brilliant.

Kwa Rwakatale ukweli utakuwa hujamtendea haki kabisa. Huyu ndiye alisimama hadharani mbele ya rais kudai misaada iliyochangwa kwaajili ya waathirika na alisema wazi kama serikali imeamua kujibinafsishia misaada badi ni bora hata iwapunguzie kodi za vifaa vya ujenzi. Feel pity for him!
 
Sio tu ukimwi (Juliana) ambao kwa sehemu kubwa uliingia nchini kupitia Kanyigo (Ziwa magharibi), kuna vita vya Kagera vilivyogharimu maisha ya maelfu ya watu, ajali ya MV. Bukoba yote haya ni majanga makuu ya kitaifa yaliyopitia mkoa wa Kagera (Bukoba).

Hili ni swali ambalo wengi tunajiuliza why through west lake region nafikiri huenda tatizo la JPM yeye kaibukia behind the microphone na sisi wengine siku zote tunawaza tu kwa sauti.
 
Mbunge wa Wahaya yaani watu wa Kagera ni mmoja tu...waliobaki ni wabunge wa wakurugenzi ...MAGARASA
 
Mimi nashangaa mtu unanyooshea wenzako vidole, kama kauli ya kiongozi wetu imekugusa, tumia fursa hii ndani ya jamvi sema upo tayali kujenga nyumba ngapi?

Kuandika ni simple sana.

Sawa alivyosema hatojenga sasa kama umeguswa tengua kauli tuone ubavu wako.
 
Back
Top Bottom