Kauli Potofu za viongozi

Bowbow

JF-Expert Member
Oct 20, 2007
541
31
Hongereni kwa jitihada waja JF

Nimetaka kuleta hii mada ya kauli potofu za viongozi waandamizi na jinsi walivyoudanganya Umma na hatimaye kuumbuliwa na ukweli.

Ningeomba tuweke kauli zote(nukuu halisi ya kiongozi) zenye Utaka kuanzia Sakata za Buzwagi, BoT, Balali,n.k

Unamtaja kwa jina unaquote kauli yake(nukuu halisi)na jinsi alivyoumbuliwa. lengo ni kufikisha ujumbe kwa wananchi wengi zaidi kwa kuonesha jinsi viongozi wetu wanavyojitahidi kutudanganya. Naamini viombo vingi vya habari vinachukua habari hapaJF tutakuwa tumewarahisishia kazi.

Karibuni
 
Naanza na Samweli Sitta

"Kuanzia sasa, nitakuwa makini sana kwa siku za usoni kuhusu taarifa za intaneti maana zinatuvuruga"

Aliyasema hayo bungeni tarehe 2007-06-30 muda mfupi baada ya Bw. Zitto Kabwe (CHADEMA-Kigoma Kaskazini) kuzungumzia tuhuma za ubadhirifu wa fedha Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Sasa sio taarifa za internet tena Sitta aambiwe aombe radhi wabunge na Umaa kwa kutoa matamshi yenye utata
 
Naanza na Samweli Sitta

"Kuanzia sasa, nitakuwa makini sana kwa siku za usoni kuhusu taarifa za intaneti maana zinatuvuruga"

Aliyasema hayo bungeni tarehe 2007-06-30 muda mfupi baada ya Bw. Zitto Kabwe (CHADEMA-Kigoma Kaskazini) kuzungumzia tuhuma za ubadhirifu wa fedha Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Sasa sio taarifa za internet tena Sitta aambiwe aombe radhi wabunge na Umaa kwa kutoa matamshi yenye utata

Asante Bow,
Ila hapo nahisi umekosea kidogo nukuu, aliye ongea ni Dr.Slaa kama nakumbuka vyema.,
 
Akiongea D. Balali (aliyekuwa gavana wa BOT)na waandishi wa habari DSM
''Tuhuma zote ni za uzushi, hao wanaona wivu kwa vile sikuwapitishia mikopo yao''
 
Akiongea D. Balali (aliyekuwa gavana wa BOT)na waandishi wa habari DSM
''Tuhuma zote ni za uzushi, hao wanaona wivu kwa vile sikuwapitishia mikopo yao''

Rwabugiri,

Nimecheka kweli -haya ndo aliyosema Dr. Balali? ukirelate na aliyosema JK jana na report ya wakaguzi- inachekesha mno!
 
JK akiongea na Waumini wa Kilutheri, wakati wa kusimikwa kwa askofu Alex Malasusa,
"Hoja ya mahakama ya kadhi haikuanzishwa na sisiemu, ilianzishwa na Mrema akiwa mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi"
Wahojaji wakamngæ'ang'ania Kikwete kwamba, "Mbona iko katika ilani ya sisiemu"? Kama sio yenu mliiweka ya nini?
 
1.Sam sitta
Akiongoe ktk kipindi maalumu cha TV, alisema akionyesha makabrasha aliyosema ya Dr. Slaa kuwa nikiwa nasoma haya makabrasha ili nijiridhishe kabla ya kuruhusu hoja ya Slaa ijadiliwe bungeni nimegundua maelezo mengi ni yakubuni na hayana ukweli wowote na nimeviagiza vyombo vya sheria viyafanyie kazi kwani huu ni uongo na ni pollice case.

2.Mhe Mzindakaya alisema ktk bunge kuwa watu wengine wanazusha tu mambo yao ya uwongo na pale BOT hakuna tatizo lolote na huu ni uzushi kutoka kwenye mitandao.

.Hitimisho je viongozi hao bado wanaona habari za Bot zilikuwa ni uzushi? na hapa naomba vyombo vya habari vifanye kazi ya kuwahoji viongozi wote waliosema ni habari za kubuni ili watoe maoni yao tena na hili litakuwa fundisho kwa wabunge kutorukia hoja ambazo hawana uhakika nazo na pia yajengwe mazingira yakuwawezesha ama kuhojiwa hata na vyombo vya habari ni kwanini walilidanganya bunge huku wakijua kuwa kusema uwongo ni kosa na hili litakuwa somo zuri kwao na kuwakumbusha ni mambo gani yaliyowapeleka bungeni. na pia ombi kwa Dr Slaa,zitto,Hamad Rashidi na wengine wanaoweza kuhoji wamhoji Spika ktk mjadala wa Bot kuna idadi ya wabunge waliolidanganya bunge ni hatua gani wanastahili kuchukuliwa ili iwe mwisho na mwanzo mzuri wa kupunguza ama kumaliza itikadi za kisiasa pale Bungeni.
 
ninachojiuliza mie kwanini huyo spika na hao waliokuwa wanatetea kwa nguvu zoote kuwa hamna tatizo lolote BOT kwanini wasijiuzulu??au waandishi wetu ndipo wangetafuta chance ya kuwahoji upya watu kama kina sitta tuone watavyojingata meno if not ndimi zao..mikubwa mizimaaaa haina hata aibu...!!
mijitu mizima ovyooooo
 
Watanzania ni wanyonge kifikra na wamekosa uzalendo wa nchi yao, ndiyo maana wameruhusu baadhi ya watu kufanya ubadhirifu by Balali alipokuwa anaongea na waandishi wa habari


"Taarifa iliyotolewa kwenye intaneti ni uongo mtupu tena haina jina halisi la mwandishi," alisema Bw. Balali kwenye mkutano huo ambao ajenda kuu ilikuwa hali ya uchumi nchini


"Hatulindi mali zetu na ukienda kwenye madini utakuta watu wamejichimbia," alisema Bw. Balali

"Niko comfortable (nimetulia) kabisa na moyo wangu ni mweupe na ninafanya kazi nzuri kama kawaida," alisema Bw. Balali na kuongeza kuwa amefurahi kutekelezwa kwa maombi yake kwa Rais ya kupewa wasaidizi ili aboreshe kazi yake ikiwamo ya kuwa karibu na waandishi kwa ufafanuzi wa mambo mbalimbali ya uchumi.

Hayo ni baadhi ya maneno ya "mshi miwa" Balali
 
Sikia hii na majibu yake

Rais mstaafu wewe ni kiongozi madhubuti na shupavu tangu zamani na hata sasa kwani kwa jinsi hawa jamaa wanavyoendelea kukuandama ungekuwa si shupavu ungekuwa umeshaanguka.
Asante sana kwa kututumikia Watanzania,`` alisema Dk. Maliki

Naye Mkapa akajibu,
``Naona Dk. Maliki anataka kuniingiza kwenye mijadala ya kisiasa, hakuna namna, mimi nimestaafu,``
Mzee huyu alionekana Dodoma kwenye maswala ya chama sisiem Je amestaafu siasa gani?


Ushupuvu wake ni upi? wa kujenga mafisadi?

Umadhubuti upi na aliwatumikia wananchi wapi?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom