Ayubu Massau
Member
- Apr 24, 2015
- 16
- 43
KAULI MBIU YETU YA TANZANIA YA VIWANDA IMEJIFUNZA NINI KUTOKA CHINA.
SEHEMU YA KWANZA
Ndugu ,
Watanzania na Wanabodi
Huu Ni Mwaka Mpya Wa 2018, Ambao Ndio Umeanza Ukiwa Mbichi Kabisa , Lakini Mwaka Huu Unasogeza Mbele Na Kutuelekeza Tukiwa Tumebakiwa Na Miaka Takribani 7, Kukamilisha Dira Ya Maendeleo Ya Taifa Mwaka 2000-2025.
Katika Dira Hii Inatuelekeza Tanzania Kufikia Uchumi Wa Kati Na Kutoka Kundi La Nchi Maskini Duniani Ifikiapo 2025.
Kichecheo kikubwa cha kutupeleka uchumi wa kati , kwa kuboreka hali ya uchumi wa taifa na Tanzania ya viwanda, kama inavyohubiriwa katika sehemu mbalimbali za nchi, jambo ambalo ni zuri na la kutia faraja na matumaini.
Neno, Tanzania ya viwanda limeanza kupata umaarufu ,wakati wa Kampeni za Uchaguzi mkuu mwaka 2015, ni sera nzuri sana na yenye kutia matumaini kwa wale wote wanaofahamu umuhimu wa viwanda katika ukuaji wa uchumi, katika taifa lolote lile.
Bahati mbaya au nzuri , wahusika wanaotakiwa kutupa Mwongozo wa Tanzania ya viwanda hawajaitoa hadharani ,ili kila mtanzania na wawekezaji toka nje wajue dira yetu katika Tanzania ya viwanda ikoje , japo dondoo tu ambazo zingekuwa Mwongozo ni aina gani za viwanda vinavyotakiwa na malighafi zake zinapatikana wapi.
Kwa kuwa sijapata wala kusikia dondoo za Tanzania ya viwanda , kuanzia sera zake, mpango kazi wake hadi Utekelezaji wake na uhusika wa watanzania moja kwa moja , mimi nitajaribu kuangazia Mapinduzi ya viwanda nchini china ,iliyopata uhuru mwaka 1949 na kuwa Jamhuri ya watu wa china chini ya Uongozi wa rais Mao Tse Tung ( Mao Ze Dong),ni miaka 12 mbele ya uhuru wa Tanganyika ( Tanzania bara) .
Sera Na Mikakati Ya Mapinduzi Ya Viwanda Nchini China.
Mapinduzi ya viwanda china ya sasa yalianza miaka 36 iliyopita , wataalam wa uchumi ,wana Sayansi na wana zuoni mbalimbali huyatazama kama Mapinduzi yenye kasi ya ajabu , tangu Mapinduzi ya viwanda nchi za ulaya miaka 250s iliyopita.
Mapinduzi haya ya viwanda nchini china ,hayakuja hivihivi kwa kutamka tu ,bali mojawapo ya sababu kuu ya Mapinduzi haya ni china kugundua wao ni taifa lenye watu wengi duniani,hivyo wana rasilimali watu na nguvu kazi kubwa zaidi ya kuzalisha malighafi zitakazoweza kutumika viwandani.
China waligundua , chini ya Asilimia 10 ya wakazi wote duniani wameshafanya Mapinduzi ya viwanda na nchi hizi nyingi zilikuwa nchi za ulaya na marekani. China wakagundua kama wao wakifanikiwa katika Mapinduzi ya viwanda itaongeza Asilimia zipatazo 20 katika Mapinduzi ya viwanda duniani na hivyo dunia kuingia katika utawala mpya wa teknolojia na viwanda.
Ukuaji wa uchumi na Mapinduzi ya viwanda nchini china ,ulizishangaza nchi nyingi duniani hasa mataifa ya ulaya na marekani wakiwemo wana uchumi wakubwa duniani, walijiuliza maswali mengi ya kinadharia yasiyo na Majibu , Moja ya swali hilo ni “ inakuwaje nchi yenye watu wapatao bilioni 1.4 kutoka kwenye kilimo kisicho na manufaa na kuwa nchi ya viwanda” wakati nchi nyingi ndogondogo Zenye watu wachache na eneo dogo zimeshindwa kufanya Mapinduzi ya viwanda japo zina mazingira mazuri na yenye kushawishi ukuaji wa uchumi.
Kutokana na ukuaji wa china kiuchumi na Mapinduzi ya viwanda kuwashangaza wana uchumi wengi duniani ( nitaeleza sera na mikakati china iliyotumia katika mwendelezo wa makala hii mbele), wengi walikuwa na maoni tofauti , lakini maoni hayo yaliegemea pande kuu mbili,
Moja “ wapo aliyoina china kama serikali kubwa sana ,ambayo haiko imara na ingesambaratika kwa sababu haikuwa na demokrasia ya kimagharibi,hakuna haki za binadamu,hakuna uhuru wa kuzungumza,hakuna utawala wa sheria,hakuna mifumo ya kimagharibi katika utawala,hakuna masoko mazuri yaliyopangiliwa,hakuna benki binafsi, hakuna ulinzi wa maandiko ya wataalam/wasomi(intellectual properties), hakuna uwezo wa kufanya ugunduzi zaidi ya kukopi na kuiba teknolojia ya nchi za magharibi na biashara za siri, haimiliki vitu vingi dhidi ya nchi ya magharibi ambazo zimemiliki kwa karne nyingi” kwa mtazamo huu wachambuzi wengi wa uchumi baada ya uhuru 1949, waliiona china kama taifa litakaloporomoka muda wowote kama ilivyokuwa huko nyuma.
Kundi la pili, lilikuwa na mtazamo huu kuhusu china “kundi hili liliona ukuaji wa china na Mapinduzi ya viwanda umetokana na historia yake ya vizazi na vizazi na kuhusisha na Tawala zake za kifalme huko nyuma, kwa Mujibu wa historia, china ilikuwa taifa tajiri na kubwa na taifa la kwanza kustaaribika kwa kuwa na mifumo iliyoeleweka kuanzia miaka ya 200K.K hadi 1800K.K, kundi hili linafikiri ilikuwa ni suala la muda tu china kurudisha hadhi yake tukufu ya kutawala tena dunia” maono ya kundi hili la pili yanapata mkazo na msisitizo kupitia Kauli ya mfalme wa Kifaransa enzi hizo (King Napeleon Bonaparte) alivyosema, nanukuu “Let china sleep for a while, when the dragon awakes, she will shake the world” Mwisho wa kunukuu.
Japokuwa ,Makundi hayo mawili yalikuwa na mitazamo yao katika maono,lakini yanachagizwa na u sirias katika Uchambuzi wa kiuchumi, badala ya kutegemea katika Upande wa historia na mawazo ya kufikirika, wachumi waliendelea Kujiuliza hili swali “inakuwaje nchi isiyo kuwa na biashara zinazoeleweka na Ufanyaji tafiti /ugunduzi kuwa na uwezo wa kukua kiuchumi na kufikia digit mbili kwa mwaka, Mfululizo kwa miongo mingi na kufanya mabadiliko yenyewe kwa muda mfupi, kutoka uchumi wa kilimo kisicho na tija hadi kuwa ngome ya Mapinduzi ya viwanda”
Wana uchumi wakubwa ,duniani waliendelea Kujiuliza, kama ni suala la utamaduni na mahusiano ya jamii za kale zilizoanza kustaarabika mapema, Je Kwanini, nchi kama Misri,Ugiriki na Dola la Ottoman wameshindwa kufikia hatua hiyo?. Swali hili limekuwa gumu sana kupata Ufumbuzi juu ya Mapinduzi makubwa ya viwanda nchini china.
Andiko ,hili linajaribu tu kutuelewesha wenzetu china walipotoka na walivyofanikiwa katika Mapinduzi ya viwanda ,kama sisi tunavyoimba Tanzania ya viwanda.
Itaendelea......
SEHEMU YA KWANZA
Ndugu ,
Watanzania na Wanabodi
Huu Ni Mwaka Mpya Wa 2018, Ambao Ndio Umeanza Ukiwa Mbichi Kabisa , Lakini Mwaka Huu Unasogeza Mbele Na Kutuelekeza Tukiwa Tumebakiwa Na Miaka Takribani 7, Kukamilisha Dira Ya Maendeleo Ya Taifa Mwaka 2000-2025.
Katika Dira Hii Inatuelekeza Tanzania Kufikia Uchumi Wa Kati Na Kutoka Kundi La Nchi Maskini Duniani Ifikiapo 2025.
Kichecheo kikubwa cha kutupeleka uchumi wa kati , kwa kuboreka hali ya uchumi wa taifa na Tanzania ya viwanda, kama inavyohubiriwa katika sehemu mbalimbali za nchi, jambo ambalo ni zuri na la kutia faraja na matumaini.
Neno, Tanzania ya viwanda limeanza kupata umaarufu ,wakati wa Kampeni za Uchaguzi mkuu mwaka 2015, ni sera nzuri sana na yenye kutia matumaini kwa wale wote wanaofahamu umuhimu wa viwanda katika ukuaji wa uchumi, katika taifa lolote lile.
Bahati mbaya au nzuri , wahusika wanaotakiwa kutupa Mwongozo wa Tanzania ya viwanda hawajaitoa hadharani ,ili kila mtanzania na wawekezaji toka nje wajue dira yetu katika Tanzania ya viwanda ikoje , japo dondoo tu ambazo zingekuwa Mwongozo ni aina gani za viwanda vinavyotakiwa na malighafi zake zinapatikana wapi.
Kwa kuwa sijapata wala kusikia dondoo za Tanzania ya viwanda , kuanzia sera zake, mpango kazi wake hadi Utekelezaji wake na uhusika wa watanzania moja kwa moja , mimi nitajaribu kuangazia Mapinduzi ya viwanda nchini china ,iliyopata uhuru mwaka 1949 na kuwa Jamhuri ya watu wa china chini ya Uongozi wa rais Mao Tse Tung ( Mao Ze Dong),ni miaka 12 mbele ya uhuru wa Tanganyika ( Tanzania bara) .
Sera Na Mikakati Ya Mapinduzi Ya Viwanda Nchini China.
Mapinduzi ya viwanda china ya sasa yalianza miaka 36 iliyopita , wataalam wa uchumi ,wana Sayansi na wana zuoni mbalimbali huyatazama kama Mapinduzi yenye kasi ya ajabu , tangu Mapinduzi ya viwanda nchi za ulaya miaka 250s iliyopita.
Mapinduzi haya ya viwanda nchini china ,hayakuja hivihivi kwa kutamka tu ,bali mojawapo ya sababu kuu ya Mapinduzi haya ni china kugundua wao ni taifa lenye watu wengi duniani,hivyo wana rasilimali watu na nguvu kazi kubwa zaidi ya kuzalisha malighafi zitakazoweza kutumika viwandani.
China waligundua , chini ya Asilimia 10 ya wakazi wote duniani wameshafanya Mapinduzi ya viwanda na nchi hizi nyingi zilikuwa nchi za ulaya na marekani. China wakagundua kama wao wakifanikiwa katika Mapinduzi ya viwanda itaongeza Asilimia zipatazo 20 katika Mapinduzi ya viwanda duniani na hivyo dunia kuingia katika utawala mpya wa teknolojia na viwanda.
Ukuaji wa uchumi na Mapinduzi ya viwanda nchini china ,ulizishangaza nchi nyingi duniani hasa mataifa ya ulaya na marekani wakiwemo wana uchumi wakubwa duniani, walijiuliza maswali mengi ya kinadharia yasiyo na Majibu , Moja ya swali hilo ni “ inakuwaje nchi yenye watu wapatao bilioni 1.4 kutoka kwenye kilimo kisicho na manufaa na kuwa nchi ya viwanda” wakati nchi nyingi ndogondogo Zenye watu wachache na eneo dogo zimeshindwa kufanya Mapinduzi ya viwanda japo zina mazingira mazuri na yenye kushawishi ukuaji wa uchumi.
Kutokana na ukuaji wa china kiuchumi na Mapinduzi ya viwanda kuwashangaza wana uchumi wengi duniani ( nitaeleza sera na mikakati china iliyotumia katika mwendelezo wa makala hii mbele), wengi walikuwa na maoni tofauti , lakini maoni hayo yaliegemea pande kuu mbili,
Moja “ wapo aliyoina china kama serikali kubwa sana ,ambayo haiko imara na ingesambaratika kwa sababu haikuwa na demokrasia ya kimagharibi,hakuna haki za binadamu,hakuna uhuru wa kuzungumza,hakuna utawala wa sheria,hakuna mifumo ya kimagharibi katika utawala,hakuna masoko mazuri yaliyopangiliwa,hakuna benki binafsi, hakuna ulinzi wa maandiko ya wataalam/wasomi(intellectual properties), hakuna uwezo wa kufanya ugunduzi zaidi ya kukopi na kuiba teknolojia ya nchi za magharibi na biashara za siri, haimiliki vitu vingi dhidi ya nchi ya magharibi ambazo zimemiliki kwa karne nyingi” kwa mtazamo huu wachambuzi wengi wa uchumi baada ya uhuru 1949, waliiona china kama taifa litakaloporomoka muda wowote kama ilivyokuwa huko nyuma.
Kundi la pili, lilikuwa na mtazamo huu kuhusu china “kundi hili liliona ukuaji wa china na Mapinduzi ya viwanda umetokana na historia yake ya vizazi na vizazi na kuhusisha na Tawala zake za kifalme huko nyuma, kwa Mujibu wa historia, china ilikuwa taifa tajiri na kubwa na taifa la kwanza kustaaribika kwa kuwa na mifumo iliyoeleweka kuanzia miaka ya 200K.K hadi 1800K.K, kundi hili linafikiri ilikuwa ni suala la muda tu china kurudisha hadhi yake tukufu ya kutawala tena dunia” maono ya kundi hili la pili yanapata mkazo na msisitizo kupitia Kauli ya mfalme wa Kifaransa enzi hizo (King Napeleon Bonaparte) alivyosema, nanukuu “Let china sleep for a while, when the dragon awakes, she will shake the world” Mwisho wa kunukuu.
Japokuwa ,Makundi hayo mawili yalikuwa na mitazamo yao katika maono,lakini yanachagizwa na u sirias katika Uchambuzi wa kiuchumi, badala ya kutegemea katika Upande wa historia na mawazo ya kufikirika, wachumi waliendelea Kujiuliza hili swali “inakuwaje nchi isiyo kuwa na biashara zinazoeleweka na Ufanyaji tafiti /ugunduzi kuwa na uwezo wa kukua kiuchumi na kufikia digit mbili kwa mwaka, Mfululizo kwa miongo mingi na kufanya mabadiliko yenyewe kwa muda mfupi, kutoka uchumi wa kilimo kisicho na tija hadi kuwa ngome ya Mapinduzi ya viwanda”
Wana uchumi wakubwa ,duniani waliendelea Kujiuliza, kama ni suala la utamaduni na mahusiano ya jamii za kale zilizoanza kustaarabika mapema, Je Kwanini, nchi kama Misri,Ugiriki na Dola la Ottoman wameshindwa kufikia hatua hiyo?. Swali hili limekuwa gumu sana kupata Ufumbuzi juu ya Mapinduzi makubwa ya viwanda nchini china.
Andiko ,hili linajaribu tu kutuelewesha wenzetu china walipotoka na walivyofanikiwa katika Mapinduzi ya viwanda ,kama sisi tunavyoimba Tanzania ya viwanda.
Itaendelea......