Kauli mbiu kuelekea Simba v Al Ahly | "Total war - Point of no return"

Utopologist

JF-Expert Member
Feb 17, 2021
987
2,487
“Mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika kati yetu Simba na Al Ahly kutoka nchini Misri itapigwa saa 10:00 jioni siku ya Jumanne Februari 23, 2021. Ni mechi kubwa sana kwa Simba, Tanzania na Afrika Mashariki.”- Haji Manara
.
🖋️ “Mabingwa wa Afrika ambao wametoka kushiriki ubingwa wa dunia wamefanikiwa kushika nafasi ya tatu watakuwa nchini kuwakabili mabingwa mara nyingi zaidi wa Afrika Mashariki. Rekodi hizo zitaufanya mchezo kuwa wa kipekee.”- Haji Manara
.
🖋️ “Mara ya mwisho tulikutana hapa Dar tukawafunga goli 1-0 kwenye mechi tuliyosema YES WE CAN na tukaweza. Al Ahly mara zote tukicheza Tanzania tunawafunga.”- Haji Manara
.
🖋️ “Tunao uwezo wa kuwafunga tena, tunao uwezo wa kushinda mechi hiyo. Dhamira hiyo ipo kwa kila Mwanasimba kuanzia wachezaji, benchi la ufundi, viongozi, wanachama na mashabiki wote.”- Haji Manara
.
🖋️ “Al Ahly sio timu nyepesi. Tunaposema tunaweza kuwafunga tunajua ukubwa wao, lakini Simba hupenda mechi kubwa kama hizi.”- Haji Manara
.
🖋️“Tumejiandaa kiakili na tunakwenda kwenye mchezo huu hakuna jambo lingine ila ushindi ili kukaribia lengo letu la nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika.”- Haji Manara
.
🖋️ “Mechi ya mwisho tuliita WAR IN DAR, mechi ya jasho na damu ndani ya dakika 90 na sasa tunasema TOTAL WAR : POINT OF NO RETURN hii sasa ni vita kamili ya ndani ya uwanja.”- Haji Manara.
.
🖋️“Malengo yetu ni makubwa, tunataka kuleta heshima kwa Afrika Mashariki. Tunawakilisha zaidi ya watu 150 milioni, wote hao wanategemea timu moja Simba SC. Tunaenda kutetea Simba, Tanzania na Afrika Mashariki yote.”- Haji Manara. #NguvuMoja
.
🖋️“CAF wametwambia wanaruhusu watu 30,000 pekee. Kwa timu kubwa kama Simba SC na Al Ahly kiingilio cha Mzunguko - Tsh. 3,000 ukibaki nyumbani Usimba wako ni wa mashaka. 15,000 - VIP B, 30,000 - VIP A . Viingilio hivi mwisho Jumatatu usiku. Ikiingia Jumanne Mzunguko - Tsh. 5,000, VIP B - 20,000 na VIP A - Tsh. 40,000.”- Haji Manara
 
Wakati wengine wakijipanga namna ya kupambana na kumshinda bingwa wa Afrika na mshindi wa tatu wa vilabu duniani, Kuna wengine wanajipanga kujitoa kwenye ligi endapo hawatapendelewa na refa kuifunga team ya Mtibwa Sugar toka hapo Turiani Morogoro....

Soka la bongo linaenda kwa kasi sana miaka hii...
 
Sina mengi ya kuwaambia wanautelembwe wote maandalizi ya Hamsa yanahanzia kwa mkapa, yahani hiyo jumanne hamtoki hata muingie na nguruwe uwanjani waarabu lazima wawatoboe tu Hakuna namna ya utelembwe kupona siku hiyo
 
Kumtumia maneno sentensi mbili imeharibu ingebaki tu total war au wangeweka Point of no return

Point of no return ingetosha sana
Kusema kweli hizo kauli zingefaa kutumika kama ingekuwa ni mechi ya mwisho ya group stage ambayo ni lazima tushinde au mechi ya marudiano robo au nusu fainali ambapo ushindi ni lazima ili kuendelea mbele

Total war au point of no return katika mchezo wa pili group stage naona kama ni extreme kidogo
 
Kusema kweli hizo kauli zingefaa kutumika kama ingekuwa ni mechi ya mwisho ya group stage ambayo ni lazima tushinde au mechi ya marudiano robo au nusu fainali ambapo ushindi ni lazima ili kuendelea mbele

Total war au point of no return katika mchezo wa pili group stage naona kama ni extreme kidogo
Hamna jinsi tunaitaji point tatu na hatutaki iwe mechi ya kawaida kwetu sababu tuko nyumbani na tunacheza na bingwa wa afrika unategemea nini sio mechi ya kiboya
 
Kusema kweli hizo kauli zingefaa kutumika kama ingekuwa ni mechi ya mwisho ya group stage ambayo ni lazima tushinde au mechi ya marudiano robo au nusu fainali ambapo ushindi ni lazima ili kuendelea mbele

Total war au point of no return katika mchezo wa pili group stage naona kama ni extreme kidogo
You are right kiongozi. Nadhani labda mechi hizo tutatumia lugha kali zaidi... "time of killing" hahaha
 
Back
Top Bottom