Kauli huumba! Je, ni kweli Magufuli ni dikiteta? Kama ni kweli, ni kosa la nani kati yake na aliyetoa kauli hii?

Paskali ndugu yangu. Una uelewa wa mambo kiupana sana tena sana. Kwa kutambua hilo, naomba nikuulize kwanza maana ya dikteta ni nini? Hili neno liko kwenye kamusi zetu? Je, haiwezi kuwa rungu la wakubwa ambalo linatumika kusambaratisha umoja wa vinchi vidogo kama haka ka kwetu?

Ni kweli sisi tunaongozwa na dikteta? Kwa dalili au vipimo vipi? Ukiwa Baba wa familia na ukaamka na kumkuta mtoto wako hapo nyumbani hajaenda shule na anachezea midoli au anaumba ng'ombe wa udongo na angalau ukatata kufahamu kwa nini hajaenda shule na akakujibu hataki utafanyaje?

Nafahamu ni lazima utatumia nguvu kwa kuwa kama mzazi utakuwa unafahamu umhimu wa shule. Hapo hujawa dikteta? Ni dhahiri utakuwa dikteta japo dhamira yako itakuwa sahihi na ya kumuokoa mwanao ili asipate madhila huko mbeleni. Lakini pia kuna mifano mingi sana hapa ninaweza kuitoa ikiwemo ya viongozi waliopachikwa majina ya udikteta na mpaka wakaondoshwa madarakani na wengine kuuwawa kama wanyama. Tanzania hatuna dikteta wala hatujampata wa kufanana nae. Mwalimu pia aliwahi kuitwa dikteta na hao hao wanaojaribu kupenyeza hii kitu sasa.

Hakika si watu wema kwetu. Wana mbinu lukuki za kutuvuta mashati. Ukitaka mkeo akuheshimu ni lazima asiwe na uwezo wa kujipatia kipato chake Paskali. Akiwa na kazi yake na akajitosheleza wewe hutoweza kumwambia akupikie ugali usiku wa manane na kama huamini jaribu utakuja unioe mrejesho. Hizi ni propaganda kama demokrasia nk.

Tuziepuke tujenge nchi yetu. Tuna kiongizi mfia nchi tumuungee mkono. Hii ni bahati hatutaiona kirahisi naamini hivyo. Nyerere aliitwa dikteta lakini angalau yeye hakuwahi kukubali hayo na yawezekana hakuwa dikteta bali ni mzazi alietaka mtoto asichezee maboksi siku ya shule badala yake aende shule akasome ili kutengeneza maisha yake ya baadae.

Tusikubali msemo wa "wenzetu" UK au USA. Hao si wenzetu maana wana utamaduni tofauti na sisi na hawatakuja kuwa wenzetu milele.

Watakusifia ukishindwa na kamwe hawatakupenda ukiwa na dalili za kushinda. Ukijiweza maana yake hawatakunyonya tena.
Watu kama wewe ni wamezaji wa kila kitu mnachoambiwa. Makengeza hayawaruhusu kuona kwa Uhuru. Nchi yetu inahitaji kuboreshwa na kusogezwa mbele na siyo kuharibiwa kwa kigezo butu cha uzalendo.
 
Wanabodi,

Kuna hoja kuwa kauli huumba. Yaani ukitoa kauli fulani, kauli hiyo inakuwa na nguvu za kuumba, hivyo huko mbele inakuja kukiumba kitu hicho kilichosemwa au kilichozungumzwa.

Hili likitokea, kosa ni la nani kati ya kilichotokea na aliyekiumba kwa kauli?.

Kama ni kweli kauli huwa zinaumba, kuna hii kauli kuwa Tanzania itatawaliwa na dikiteta, na kama rais Magufuli kweli ni dikiteta, then sio kosa lake kuwa dikiteta, kwa sababu huo udikiteta hakujiumbia yeye, bali uliumbwa kwa kauli kuwa tutatawaliwa na rais dikiteta!.

Sikiliza kwa makini clip hii, kisha ujibu maswali yafuatayo

Jee ni kweli Tanzania tuko under dictatorship?,
Kama ni kweli, jee kosa ni la nani?,
Ni la dikiteta aliyepo ambaye hakujiumba, bali aliumbwa, au ni kosa la kauli yenye nguvu, iliyotuumbia huo udikiteta?.

Magufuli ni Dikiteta!, Tanzania Ilihitaji Dikiteta, Tumempata ...
Jumatatu Njema.

Paskali

Bwana Paskali wewe wasema. Katika hiyo presentation yako kuhusu Bwana Mkubwa ulimuumba vizuri sana na kwa kutumia jina lake pasipo kificho. Mwalimu alikuwa akiongea kwa ujumla tu pasipo kutaja majina. Wewe ulikwenda mbali zaidi kwani ulitoa na sifa zake na umuhimu wa kuwa na dikteta katika kipindi hiki. Hivyo, Paskali, you stand accused!
 
Aisee kweli Mkuu Kivyako? Duh kweli tuna kazi kubwa sana mbele yetu
Ulishaambiwa sio kiongozi ni nyapala wa barabara ndio pekee analojua!!!....mambo uchumi uzalishaji kilimo biashara export import yeye haelewiii!!! Visasi kashfa nguvu mabavu bila busara.....ndio anaona sifa!!!
 
Wanabodi,

[]Kuna hoja kuwa kauli huumba.[]
...
Kama ni kweli kauli huwa zinaumba, kuna hii kauli kuwa Tanzania itatawaliwa na dikiteta, na kama rais Magufuli kweli ni dikiteta, then sio kosa lake kuwa dikiteta, kwa sababu huo udikiteta hakujiumbia yeye, bali uliumbwa kwa kauli kuwa tutatawaliwa na rais dikiteta!.

Sikiliza kwa makini clip hii, kisha ujibu maswali yafuatayo

Jee ni kweli Tanzania tuko under dictatorship?,
Kama ni kweli, jee kosa ni la nani?, ...

Paskali


Paskaki, kuna methali nitatumia kujenga hoja yangu kujibu maswali yako kwamba Tanzania ni nchi ya Kimodkrasia kikatiba na kiutekelezaji wa hiyo Katiba. Na pia Rais Magufuli si dikteta.

Wahenga walinena:
1) Ukimchekea nyani utavuna mabua.
2) Samaki mkunje angali mbichi.
3) Asiyesikia la mkuu huvunjika guu.

Paskali, nimeisikiliza kwa makini hiyo clip ya Baba wa Taifa, marehemu Mwl. Nyerere. Yako maudhui mawili makuu:
1) Nafasi yetu kutokutimiza wajibu wetu ipasavyo. Kwa kipindi kirefu, tangu kupata uhuru, shughuli za umma zimekuwa zikifanywa pasipo ufanisi - ni mlolongo wa urasmu, umangimeza, rushwa, ubadhirifu, ufisadi nk kinyume na Katiba, Sheria, Kanuni na Taratibu tulizijiwekea. Uozo ulioibuliwa na Serikali iliyoko madarakani kwa sasa ni ushahidi tosha. Kwa sababu hiiyo tumevuna mabua kwa kuwa tumekuwa tukichejeana, kufichana maovu na kukumbatia waovu

2) Hilo aliliona Baba wa Taifa na kuwaasa viongozi kutokuwa waoga kuilinda na kuisimamia Katiba, Sheria, Kanuni na Taratibu husika. Akatoa tahadhari kwamba atapatikana Rais mwenye uthubutu na utashi wa kisiasa, kwa lugha kali akimlinganisha na dikteta. Hatukuchukua hatua za kumkunja samaki angali mbichi.

Rais Magufuli, ameielewa falsafa hiyo ya Mwl Nyerere na anaitekeleza, bila kupepesa macho au kumung'unya maneno kwa kaulimbiu yake ya Hapa kazitu, mithili ya Marehemu Moringe Sokoine. Pia anasisitiza utii wa sheria bila shurti. Hakika, asiyesikia la mkuu atavunjika guu.[/B] Dikteta, hapana.

Tukumbuke kwamba ni wanyama tu hushurutisha kufanya anachotaka Bwana wao wafanye, ikiwezekana kwa mijeredi. Tusisubiri kupigwa mijeledi, tijitume kutimiza wajibu wetu kwa weledi na ufanisi, kadiri ya uwezo wetu. Naamini hakuna atakayetusimamia, na kulazimika kutumia nguvu (sheria). Pia tumbuke kwamba ni tabia na hulka ya binadamu kulipiza kisasi akitendewa visivyo. Mtawala atatumia sheria, taratibu na kanuni zilizowekwa kuadhibu.
 
Mkuu Paskali, hiyo clip yako hapo Mwalimu Nyerere alikuwa ana state facts, hakuwa anafanya unabiii au kuchuria, he was merely stating the known facts.

Magufuli ni dikteta, na hilo ni tatizo la John Magufuli. NUKTA.
...
Tunaomkosoa Magufuli, wengi tuna point kwenye hizo facts za Mwl. Nyerere tu. Wengi hatumkosoi kwa kumchukia bali kwa kuonyesha na kuianisha bayana madhaifu yake, ila kiburi chake kimemfanya ashindwe kusikia na kujirekebisha.
Unaweza kuthibitisha hicho kiburi?

..
Nami nitumie 'facts' tu kama ulivyofanya. 'Fact' kwamba unatumia lugha chafu dhidi ya Rais ni wazi kwamba, tukiendekeza tabia hiyo, mwishowe tutatiana vidole machoni. Ukimkosoa mtu tumia maneno na lugha staha, na ngazi ya Rais, uwe ni uthibitisho usio na mashaka.

Lugha yaliyotumia haitumiwi hata na wavuta bangi au vichaa, labda wenye chuki pitiliza. Dawa ya chuki ni kutenda siyo maneno.
 
Nami nitumie 'facts' tu kama ulivyofanya. 'Fact' kwamba unatumia lugha chafu dhidi ya Rais ni wazi kwamba, tukiendekeza tabia hiyo, mwishowe tutatiana vidole machoni. Ukimkosoa mtu tumia maneno na lugha staha, na ngazi ya Rais, uwe ni uthibitisho usio na mashaka.

Lugha yaliyotumia haitumiwi hata na wavuta bangi au vichaa, labda wenye chuki pitiliza. Dawa ya chuki ni kutenda siyo maneno.

Asante Mwengeso kwa kunikosoa.

Basi naomba pia unisaidie lugha nzuri na neno zuri la kutumia badala ya neno kiburi nililotumia hapo ulikoweka rangi nyekundu.
 
Asante Mwengeso kwa kunikosoa.

Basi naomba pia unisaidie lugha nzuri na neno zuri la kutumia badala ya neno kiburi nililotumia hapo ulikoweka rangi nyekundu.

Hakuna lugha nzuri ila kuna lugha ya staha. Lugha staha ina kauli (statement) sahihi zenye uthibitisho.

Katika bandiko lako la kwanza umeandika ila kiburi chake kimemfanya ashindwe kusikia na kujirekebisha. Hiyo ni kauli yako.

a statement (kauli) is a definite or clear expression of something in speech or writing. "Do you agree with this statement?" Synonyms: decleration, expression of views/facts, affirmation, assertion, announcement, utterance, communication, proclamation, presentation, expounding, account, testmony, evidence, bulletin, etc).

Kwa tafsiri ya Kiswahili kauli/taarifa ni ufafanuzi halisi au uwazi wa kitu katika matamshi au maandishi. "Je, unakubaliana na kauli/taarifa hii?" Maonesho: kiapo, kujieleza kwa maoni/ukweli, uthibitisho, tamko, mawasiliano, uwasililishaji, kutafakari, ushahidi, nk.

Je, kauli yako ina staha?
 
Hujitambui wewe kelb. Ukiandika upupu na kuposti huku lazima upewe za uso. Huo ujinga wako una bahati wameunga na hii ni thread yenye maudhui mengine.

Usitegemee kuandika upumbavu halafu unyamaziwe.

Nenda kawe dikteta kwa hao ng'ombe wako unaowachunga.
Wewe nimegundua tatizo lako ni shule.
Unajua maana ya Dictator ?

Unajua kuwa huyo mwenyekiti wako wa chama kazi yake mojawapo ni ku-Dictate Sera za chama chake ?

Tatizo lako badala ya kuisoma hoja kwa kuitafakari, unakimbilia kudhihaki hoja za watu kwa kutukana badala ya kujibu hoja.

Ungeniuliza
Kwanini unasema wenyeviti wa vyama ni Ma-dictator ningekufafanulia.
Usifikiri kuwa unajua kilakitu humu kuna watu wenye fani tofauti ndugu.
We unaona kunipa za uso ndio jibu la mijadala.
Lakini sikulaumu sana kwakuwa sijui umilelewa katika malezi gani na umestarabikaje.
Inawezekana katika jamii uliyokulia mmejifunza kutukana watu badala ya kuomba ufafanuzi kwenye masuala msiyoyaelewa.
 
Wanabodi,

Kuna hoja kuwa kauli huumba. Yaani ukitoa kauli fulani, kauli hiyo inakuwa na nguvu za kuumba, hivyo huko mbele inakuja kukiumba kitu hicho kilichosemwa au kilichozungumzwa.

Hili likitokea, kosa ni la nani kati ya kilichotokea na aliyekiumba kwa kauli?.

Kama ni kweli kauli huwa zinaumba, kuna hii kauli kuwa Tanzania itatawaliwa na dikiteta, na kama rais Magufuli kweli ni dikiteta, then sio kosa lake kuwa dikiteta, kwa sababu huo udikiteta hakujiumbia yeye, bali uliumbwa kwa kauli kuwa tutatawaliwa na rais dikiteta!.

Sikiliza kwa makini clip hii, kisha ujibu maswali yafuatayo

Jee ni kweli Tanzania tuko under dictatorship?,
Kama ni kweli, jee kosa ni la nani?,
Ni la dikiteta aliyepo ambaye hakujiumba, bali aliumbwa, au ni kosa la kauli yenye nguvu, iliyotuumbia huo udikiteta?.

Magufuli ni Dikiteta!, Tanzania Ilihitaji Dikiteta, Tumempata ...
Udikiteta ni Dhana Tuu or ni Real?. "Lets Call A Spade A Spade ...
If you can't beat them, join them! He is the worst dictator. Let's ..
Mwito Kwa Wana JamiiForums Kuhusu Ukosoaji wa Rais Magufuli ..

Rais Magufuli, Waliomchagua Wanajuta!, Wasiomchagua Wanamshangilia ...
Utumbuaji Majipu wa Rais Magufuli: Is It A Right Thing, At The ...
Kama sio udikteta, Mhe. Rais futilia mbali utawala wa sheria ...
Jumatatu Njema.


Paskali

Pascal.

Umeandika kama mtu semi-literate asiyeweza kusikiliza kitu kwa mantiki.

Nyerere hakusema kwamba Tanzania itatawaliwa na dikteta.

Nyerere alisema mkiwa na woga mtatawaliwa na dikteta.

Kwa maana nyingine aliwaasa Watanzania wasiwe na woga ili wasije kutawaliwa na dikteta.

Kama kauli ya Nyerere inaumba chochote, inachoumba ni muamko wa wananchi kukataa kutawaliwa na dikteta, si utawala wa kidikteta.

Wananchi wakishindwa kuwa na muamko wa kupinga udikteta, hilo ni tatizo lao, si tatizo kwamba hawajausiwa na Nyerere kukataa udikteta.

Utasemaje kauli ya Nyerere imeumba udikteta?
 
Hakuna lugha nzuri ila kuna lugha ya staha. Lugha staha ina kauli (statement) sahihi zenye uthibitisho.

Katika bandiko lako la kwanza umeandika ila kiburi chake kimemfanya ashindwe kusikia na kujirekebisha. Hiyo ni kauli yako.

a statement (kauli) is a definite or clear expression of something in speech or writing. "Do you agree with this statement?" Synonyms: decleration, expression of views/facts, affirmation, assertion, announcement, utterance, communication, proclamation, presentation, expounding, account, testmony, evidence, bulletin, etc).

Kwa tafsiri ya Kiswahili kauli/taarifa ni ufafanuzi halisi au uwazi wa kitu katika matamshi au maandishi. "Je, unakubaliana na kauli/taarifa hii?" Maonesho: kiapo, kujieleza kwa maoni/ukweli, uthibitisho, tamko, mawasiliano, uwasililishaji, kutafakari, ushahidi, nk.

Je, kauli yako ina staha?

Asante Mwengeso. Kwanza ni kweli yale ni maoni yangu.

Niseme hivi.......mathalan imetokea mimi nimeona shida au kasoro fulani kwa Mkuu wetu, nachunguza na kujiuliza je chanzo cha tatizo alilo nalo ni nini? Nagundua kuwa chanzo ni tabia yake (attitude); na tabia ni wasifu wa kila mwenye nayo iwe mbaya au njema. Lakini pia tabia ni kielelezo/taswira, ni sehemu ya huyo mwenye nayo iwe ni mbaya au njema. Na moja ya tabia niliyoiona kwa kuangalia matendo, mwenendo na maneno yake ni kiburi (pride) kwa sababu:-

Pride is an inwardly directed emotion that carries two antithetical meanings. With a negative connotation pride refers to a foolishly and irrationally corrupt sense of one's personal value, status or accomplishments, used synonymously with hubris.

Hivyo kwa heshima na taadhima naomba nisaidie hapo how best I can put it.
 
Wanabodi,

Kuna hoja kuwa kauli huumba. Yaani ukitoa kauli fulani, kauli hiyo inakuwa na nguvu za kuumba, hivyo huko mbele inakuja kukiumba kitu hicho kilichosemwa au kilichozungumzwa.

Hili likitokea, kosa ni la nani kati ya kilichotokea na aliyekiumba kwa kauli?.

Kama ni kweli kauli huwa zinaumba, kuna hii kauli kuwa Tanzania itatawaliwa na dikiteta, na kama rais Magufuli kweli ni dikiteta, then sio kosa lake kuwa dikiteta, kwa sababu huo udikiteta hakujiumbia yeye, bali uliumbwa kwa kauli kuwa tutatawaliwa na rais dikiteta!.

Sikiliza kwa makini clip hii, kisha ujibu maswali yafuatayo

Jee ni kweli Tanzania tuko under dictatorship?,
Kama ni kweli, jee kosa ni la nani?,
Ni la dikiteta aliyepo ambaye hakujiumba, bali aliumbwa, au ni kosa la kauli yenye nguvu, iliyotuumbia huo udikiteta?.

Magufuli ni Dikiteta!, Tanzania Ilihitaji Dikiteta, Tumempata ...
Udikiteta ni Dhana Tuu or ni Real?. "Lets Call A Spade A Spade ...
If you can't beat them, join them! He is the worst dictator. Let's ..
Mwito Kwa Wana JamiiForums Kuhusu Ukosoaji wa Rais Magufuli ..

Rais Magufuli, Waliomchagua Wanajuta!, Wasiomchagua Wanamshangilia ...
Utumbuaji Majipu wa Rais Magufuli: Is It A Right Thing, At The ...
Kama sio udikteta, Mhe. Rais futilia mbali utawala wa sheria ...
Jumatatu Njema.


Paskali

Ilipotamkwa kauli ya udicteta ilishakwepo,hivyo alipotamkwa dicteta alikuwa wa hivyo,maana yake ndivyo alivyo.siyo suala la kuumba
 
Asante Mwengeso. Kwanza ni kweli yale ni maoni yangu.

Niseme hivi.......mimi naona shida kwa Mkuu wetu, nachunguza na kujiuliza je chanzo cha tatizo alilo nalo ni nini? Nagundua kuwa chanzo ni tabia yake (attitude); na tabia ni wasifu wa kila mwenye nayo iwe mbaya au njema. Lakini pia tabia ni kielelezo/taswira, ni sehemu ya huyo mwenye nayo iwe ni mbaya au njema. Na moja ya tabia niliyoiona kwa kuangalia matendo, mwenendo na maneno yake ni kiburi (pride) kwa sababu:-

Pride is an inwardly directed emotion that carries two antithetical meanings. With a negative connotation pride refers to a foolishly and irrationally corrupt sense of one's personal value, status or accomplishments, used synonymously with hubris.

Hivyo kwa heshima na taadhima naomba nisaidie hapo how best I can put it.

Tafsiri na ufafanuzi wako kuhusu tabia ni sahihi kabisa. Hitimisho lako ndilo lenye kukosa staha, unampo mtuhumu mtu pasipo na ushahidi, na hasa kiongozi wa nchi ambaye anawakilisha Taifa, ukiwemo wewe.

Unaandika mimi naona shida kwa Mkuu wetu, nachunguza na kujiuliza je chanzo cha tatizo alilo nalo ni nini? Nagundua kuwa chanzo ni tabia yake (attitude)... Na moja ya tabia niliyoiona kwa kuangalia matendo, mwenendo na maneno yake ni kiburi (pride) kwa sababu.... Unaendelea kutoa tafsiri ya neno pride kwa kiingereza na kuacha kauli yako ikielea.

Kutuhumu au kusifia tabia ya mtu ni lazima kuwepo vigezo vya kupima au kuelezea sifa hizo. Na ni vizuri katika tafsiri yako ya kiingereza ya neno pride umegusia hivyo vigezo (maneno mazito mlalo kwenye bandiko lako). Tafadhali, tusaidie (mimi na wanaJF) pride ya huyo mtu kwa matendo, mwenendo na maneno yake
 
Pascal Mayalla,

Kama ni udikteta basi aliuumba huyo Julius Nyerere na siku chache baada ya hiyo clip wapo majasiri waliomfuata na kumweleza wazi "Mwalimu wewe ndiye uliyetufundisha kuwaheshimu wakubwa". Watanzania wamezoeshwa kuwa watu wa kuogopaogopa yangu Julius Nyerere ambaye naye katawala hivyohivyo tangu 1961 hadi 1985 huku watu wakiwa waogawaoga.

Hiyo clip aliisema mwaka 1993 ambapo alishaona amebaki peke yake katika mapambano ya kuikataa Tanganyika yaliyoongozwa na serikali wakati huo. Nyerere aliona watu wanaogopa lakini akasahau kwamba yeye ni mdau mkubwa wa kuwafanya watu wogope na hadi kesho mtanzania ni mtu wa kuogopaogopa.

HUku makazini ukitokea kujua sheria kila mtu anakuogopa akidhani wewe ni USALAMA WA TAIFA. USALAMA WA TAIFA ni taasisi iliyotakiwa kupendwa na kila mmoja kwani ni usalama wa Paschal Mayala, wewe na mimi. Lakini inapofikia mimi na wewe tunapoogopa USALAMA WA TAIFA basi tusiishie kwa Rais wa sasa bali tuanzie kwa Rais aliyeufanya tukauogopa.

Taifa ni taifa. Ni jamii ya watu. Ukiingiza jambo kwenye psychology ya taifa hata kama ni dogo usitarajie liondoke lote chini ya miaka hata sabini. Ukumbuke mtawala unapofanya hata jambo la kipumbavu wapo watu wanaofaidika na jambo hilo na watakuwa washabiki wako na wataambukiza hata wajukuu ule ushabiki ili waendelee kufaidi.

Hakuna dikteta duniani ambaye hakutumia USALAMA WA TAIFA lake. Hakuna dikteta duniani ambaye hakupata washabiki na wapiga debe tena kw amiaka kadhaa inayofuata.

Watanzania tumepandikizwa woga kiasi kwamba ukianza kudai haki tena za rafiki yako aliyegandamizwa utaona yeye mwenyewe anaanza kukuonya kwamba unaleta jambo la hatari. Haajali kwamba haki unayompigania ni yake!

Kumbuka chama alichokuwamo Nyerere ndiyo bado kiko madarakani. Kama kuna misingi ya udikteta ilianzishwa enzi za Julius Nyerere chama hicho kitaendelea kutamba na silaha hiyo.

Sasa hiyo clip ya MWalimu ni fundisho kwake yeye mwenyewe maana wakati huo alibaki mwenyewe kuipigania Tanganyika isije kwani RAsi Ali Hassan Mwinyi na serikali yake yote na bunge zima walishakubali Tanganyika ije. Sasa katika mazingira kama hayo ni mtanzania gani ambaye angepiga hilo. Hapa ndipo Julius Nyerere alipokosea yaani kutoandaa mazingira ya watanzania kuishughulikia serikali inapofanya madudu kama ilivyomfanyia.

Yeye Julius Nyerere alikuwa anafaidi ulinzi kama Rais mstaafu. Hivyo watu wasiojulikana wasingeweza kumfikia kiurahisi na kumfyatulia risasi.

Sisi anaoutusema eti tunaogopa si kwamba tunaogopa kusema na tuna akili kama zake Julius Nyerere. Ila tunaogopa kupigwa risasi 32 kama Tundu Lissu, kupotea kama Ben Saa Nane, kuvamiwa kama Ulimboka.

Hii ndiyo comment yangu kuhusu udikteta. Sisi kama wnanchi hatukuutengeneza bali tawala ziliutengeneza tangu 1961 hadi leo. Hivyo unapaswa uwasifie vyama vya upinzani kwamba wamejitoa mhanga maisha yao.

Si unaona hata kwenye fani yenu ya uandishi wa habari mnavyopigana vikumbo kujipendekeza kwa serikali.

Ngoja niisikilize tena kwa sikio la rohoni labda nitaelewa!
Ukisoma historia utagundua hakuna jipya katika hii dunia.
Pascal.

Umeandika kama mtu semi-literate asiyeweza kusikiliza kitu kwa mantiki.

Nyerere hakusema kwamba Tanzania itatawaliwa na dikteta.

Nyerere alisema mkiwa na woga mtatawaliwa na dikteta.

Kwa maana nyingine aliwaasa Watanzania wasiwe na woga ili wasije kutawaliwa na dikteta.

Kama kauli ya Nyerere inaumba chochote, inachoumba ni muamko wa wananchi kukataa kutawaliwa na dikteta, si utawala wa kidikteta.

Wananchi wakishindwa kuwa na muamko wa kupinga udikteta, hilo ni tatizo lao, si tatizo kwamba hawajausiwa na Nyerere kukataa udikteta.

Utasemaje kauli ya Nyerere imeumba udikteta?
Mkuu Paskali, hiyo clip yako hapo Mwalimu Nyerere alikuwa ana state facts, hakuwa anafanya unabiii au kuchuria, he was merely stating the known facts.

Magufuli ni dikteta, na hilo ni tatizo la John Magufuli. NUKTA.

Upande wa pili kuna tatizo la mfumo (system) ambao ni dhaifu na butu haukufanya kazi ya vetting thoroughly. Hakuna namna Magufuli angeshika hata nafasi ya 10 kati ya wagombea 11, kwa sababu track record yake Wizara "alizotawala" ilikuwa mbaya na chafu. Hizo takwimu za kukariri ambazo zilimpa umaarufu zilipaswa kupitishwa kwenye tanuru ili dhahabu ijulikane na makinikia yajulikane.

Ukitaka kujua ubaya wake sikiliza kauli zake anapotafuta sympathy au ego-satisfaction hasa kwa kutumia zile cheap and stereo-typed popular slogans zake za uzalendo, upendo, tumbua nk nk. Ule ni unafiki wa kiwango cha Hollywood. Unafiki na chuki ni tabia zake Magufuli asisingiziwe mtu mwingine awaye yote. Anatakiwa akubali huo udhaifu kisha ajirekebishe (ni process) sio kusema aombewe. Udikteta wake alianzia kwenye familia yake na maisha yake yote amekuwa uchwara, hata kwenye Wizara alizotumikia.

Tunaomkosoa Magufuli, wengi tuna point kwenye hizo facts za Mwl. Nyerere tu. Wengi hatumkosoi kwa kumchukia bali kwa kuonyesha na kuianisha bayana madhaifu yake, ila kiburi chake kimemfanya ashindwe kusikia na kujirekebisha.
Mkuu Pascal Mayalla Kuna Nissan Nyeupe siku hizi na pia kuna watu wasiojulikana wanatoa bastola hata mbele ya Polisi na bado hawajulikani! Kweli Maneno huumba!

Cc:
Pascal Mayalla,
 
Wewe nimegundua tatizo lako ni shule.
Unajua maana ya Dictator ?

Unajua kuwa huyo mwenyekiti wako wa chama kazi yake mojawapo ni ku-Dictate Sera za chama chake ?

Tatizo lako badala ya kuisoma hoja kwa kuitafakari, unakimbilia kudhihaki hoja za watu kwa kutukana badala ya kujibu hoja.

Ungeniuliza
Kwanini unasema wenyeviti wa vyama ni Ma-dictator ningekufafanulia.
Usifikiri kuwa unajua kilakitu humu kuna watu wenye fani tofauti ndugu.
We unaona kunipa za uso ndio jibu la mijadala.
Lakini sikulaumu sana kwakuwa sijui umilelewa katika malezi gani na umestarabikaje.
Inawezekana katika jamii uliyokulia mmejifunza kutukana watu badala ya kuomba ufafanuzi kwenye masuala msiyoyaelewa.
Crap. Don't got time for whining beyotches
 
Paskali: unachokiona leo, ni matokeo ya kazi iliyofanyika hapo kabla. So Udicteta wa leo haukuanza leo, pita wizara zote alipopitia huyu jamaa utaona harufu kali ya udicteta. unakumbuka Samaki wale, Nyumba za serikali, Makanikia, Konoike nk. Nani yupo nyuma yake.
 
Crap. Don't got time for whining beyotches
We kuwa tu mtumwa wa lugha za kigeni.
Tunajadiliana kwa Kiswahili wewe unajibu kwa kiingereza tena kwa kutukana.
Kama unaona nilichokiandika hakika maana we kaa kimya tu sio lazima utukane na kujionesha jinsi ulivyo.

Sipendi watukanaji.
 
Mkuu Paskali, hiyo clip yako hapo Mwalimu Nyerere alikuwa ana state facts, hakuwa anafanya unabiii au kuchuria, he was merely stating the known facts.

Magufuli ni dikteta, na hilo ni tatizo la John Magufuli. NUKTA.

Upande wa pili kuna tatizo la mfumo (system) ambao ni dhaifu na butu haukufanya kazi ya vetting thoroughly. Hakuna namna Magufuli angeshika hata nafasi ya 10 kati ya wagombea 11, kwa sababu track record yake Wizara "alizotawala" ilikuwa mbaya na chafu. Hizo takwimu za kukariri ambazo zilimpa umaarufu zilipaswa kupitishwa kwenye tanuru ili dhahabu ijulikane na makinikia yajulikane.

Ukitaka kujua ubaya wake sikiliza kauli zake anapotafuta sympathy au ego-satisfaction hasa kwa kutumia zile cheap and stereo-typed popular slogans zake za uzalendo, upendo, tumbua nk nk. Ule ni unafiki wa kiwango cha Hollywood. Unafiki na chuki ni tabia zake Magufuli asisingiziwe mtu mwingine awaye yote. Anatakiwa akubali huo udhaifu kisha ajirekebishe (ni process) sio kusema aombewe. Udikteta wake alianzia kwenye familia yake na maisha yake yote amekuwa uchwara, hata kwenye Wizara alizotumikia.

Tunaomkosoa Magufuli, wengi tuna point kwenye hizo facts za Mwl. Nyerere tu. Wengi hatumkosoi kwa kumchukia bali kwa kuonyesha na kuianisha bayana madhaifu yake, ila kiburi chake kimemfanya ashindwe kusikia na kujirekebisha.

Mbali na kuwa umetumia denials as a defensive mechanism kwa kutumia maneno kama "Hatumchukii" n.k, Kwa mtu mwenye akili post yako imejaa chuki binafsi kwa Magufuli binafsi na si kwa kuangalia utendaji wake.

- Hakuna hata sehemu moja umediscuss utendaji wake bali kufanya Character assassination kwa kumpa sifa mbaya ambazo nina uhakika hana.
 
Back
Top Bottom