Kauli hii ya CHADEMA ina athari yoyote kwa yanayoendelea?

Oh my God sijui watu wengine uelewa wao wa hoja ni upi? Sasa kuna hoja gani ya kujadili la huyu anayejiita jakay...labda kama anataka advice on how to come up with what people call hoja...hata kama in the back of your mind alln you ever think is how to stain CDM, it would have been good if you come up with something sensible...unfortunately, that you are unable to come up with and you will never be able to do so; because in reality, you are running away from the truth...and where you are supposed to point your fingers at...where for you and people like you...that would hurt because it will affect you and those of the likes of yours...the truth hurts...but you must face it if you want to be free...the truth shall make you free
 
TAMKO LA KIKAO CHA KAMATI KUU YA CHADEMA KUHUSU HALI YA TAIFA



TAMKO LA KIKAO CHA KAMATI KUU YA CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA) KUHUSU HALI YA TAIFA.


Kamati Kuu ya CHADEMA katika kikao chake cha kawaida kilichofanyika tarehe 29-30 Januari 2011 jijini Dar es Salaam chini ya Mwenyekiti wa Taifa Mheshimiwa Freeman Aikael Mbowe (Mb), pamoja na mambo mengine, imepokea, kujadili na kutolea maazimio Taarifa ya Hali ya Siasa na Taifa kwa ujumla. Maazimio haya yapo katika maeneo matano yafuatayo.

3. Matatizo ya Nishati ya Umeme na Gesi na Malipo kwa Kampuni Hewa ya Dowans

Kamati Kuu imesikitishwa na kupanda holela kwa bei za nishati muhimu za umeme na gesi, pamoja na kushindwa kwa serikali ya CCM katika kuwekeza kikamilifu katika sekta ya nishati hapa nchini. Aidha, Kamati Kuu imesikitishwa na kufadhaishwa sana na uamuzi wa CCM na serikali yake kuridhia kuilipa Kampuni hewa ya Dowans fedha za walipa kodi wa Tanzania zipatazo Shilingi bilioni 94, pamoja na kwamba Kampuni hii ilikwishaharamishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa niaba ya wananchi.

Kamati Kuu imetambua kuwa sakata la Dowans ni mwendelezo wa vitendo vya kifisadi ndani ya CCM na serikali yake ambavyo vimeligharimu taifa hili kwa miongo mitano iliyopita. Hivyo basi:

  1. Kamati Kuu imewahimiza wana CHADEMA, wabunge na wananchi kwa ujumla kuendelea kupinga kwa nguvu zote malipo ya Dowans
  2. Kamati Kuu imewaelekeza viongozi pamoja na wabunge wa CHADEMA kuendelea kuwahamasisha wananchi kupinga kwa njia mbalimbali za kisiasa na kisheria malipo ya Dowans na ufisadi mwingine hapa nchini
  3. Kamati Kuu imewapongeza na kuwashukuru wanaharakati wa taasisi za kiraia kwa ujasiri na moyo wao wa kizalendo kwa uamuzi wao wa kufungua kesi mahakamani ya kupinga malipo ya Dowans
  4. Kamati Kuu imeiasa Serikali ya CCM kutokuona aibu kutekeleza sera za CHADEMA zilizofanyiwa utafiti kuhusu namna ya kujenga na kuimarisha sekta ya nishati ya umeme na gesi hapa nchini ili nchi yetu iondokane na tatizo la kudumu la umeme.
  5. Kamati Kuu imeiagiza Secretariat yake kuanza maandalizi ya maandamano ya nchi nzima ya kupinga ongezeko la bei ya umeme, gesi na kuilipa Dowans. Na tarehe 24/02/2011 itakuwa siku ya kuanza maandamano kwenye Jiji la Mwanza na miji mingine kadiri ratiba itakavyotolewa.

7. Kuhusu mpango mkakati wa chama 2011-2016.

Kamati Kuu ilijadili na kupitisha mapendekezo ya mpango kazi wa chama kwenye Baraza kuu la chama .Pia ilijadili na kupitisha mpango kazi wa mwaka 2011-2012.

Tamko hili limetolewa leo tarehe 31/01/2011.

Dk Willibrod Peter Slaa
Katibu Mkuu




6773768.jpg

Hujafafanua hoja yako vizuri. Una maana walikuwa wanachambua mabomu ya machozi ya kuwashughulikia CHADEMA 24/2/2011 haya mengine yakalipuka au?
 
Sioni uhusiano wowote kati ya mabomu kulipuka na mipango ya maandamano ya CHADEMA kupinga ongezeko la bei ya umeme. Ila kama una ushahidi sio vibaya ukautoa hadharani ili wengine tuujue. Kuhusu chanzo cha milipuko nadhani wanajeshi, hasa wataalamu wa milipuko, wanaweza kutujulisha kwa ufasaha zaidi.
 



Pengine ingekuwa vizuri tukajua chama kikuu cha upinzani kimetoa tamko gani kuhusu matatizo yanayotukabili kama Nishati,elimu (kidato cha nne - matokeo ) na swala la udini unaohubiriwa na wanapropaganda sikuhizi.

Yafuatayo ni matamko ya kamati kuu kuhusiana na matatizo hayo.




Matatizo ya Nishati ya Umeme na Gesi na Malipo kwa Kampuni Hewa ya Dowans

Kamati Kuu imesikitishwa na kupanda holela kwa bei za nishati muhimu za umeme na gesi, pamoja na kushindwa kwa serikali ya CCM katika kuwekeza kikamilifu katika sekta ya nishati hapa nchini. Aidha, Kamati Kuu imesikitishwa na kufadhaishwa sana na uamuzi wa CCM na serikali yake kuridhia kuilipa Kampuni hewa ya Dowans fedha za walipa kodi wa Tanzania zipatazo Shilingi bilioni 94, pamoja na kwamba Kampuni hii ilikwishaharamishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa niaba ya wananchi.
Kamati Kuu imetambua kuwa sakata la Dowans ni mwendelezo wa vitendo vya kifisadi ndani ya CCM na serikali yake ambavyo vimeligharimu taifa hili kwa miongo mitano iliyopita. Hivyo basi:

  1. Kamati Kuu imewahimiza wana CHADEMA, wabunge na wananchi kwa ujumla kuendelea kupinga kwa nguvu zote malipo ya Dowans
  2. Kamati Kuu imewaelekeza viongozi pamoja na wabunge wa CHADEMA kuendelea kuwahamasisha wananchi kupinga kwa njia mbalimbali za kisiasa na kisheria malipo ya Dowans na ufisadi mwingine hapa nchini
  3. Kamati Kuu imewapongeza na kuwashukuru wanaharakati wa taasisi za kiraia kwa ujasiri na moyo wao wa kizalendo kwa uamuzi wao wa kufungua kesi mahakamani ya kupinga malipo ya Dowans
  4. Kamati Kuu imeiasa Serikali ya CCM kutokuona aibu kutekeleza sera za CHADEMA zilizofanyiwa utafiti kuhusu namna ya kujenga na kuimarisha sekta ya nishati ya umeme na gesi hapa nchini ili nchi yetu iondokane na tatizo la kudumu la umeme.
  5. Kamati Kuu imeiagiza Secretariat yake kuanza maandalizi ya maandamano ya nchi nzima ya kupinga ongezeko la bei ya umeme, gesi na kuilipa Dowans. Na tarehe 24/02/2011 itakuwa siku ya kuanza maandamano kwenye Jiji la Mwanza na miji mingine kadiri ratiba itakavyotolewa.
Matokeo ya Kidato cha Nne

Kamati Kuu imeyapokea kwa masikitiko makubwa matokeo ya Kidato cha Nne yanayoonyesha kuwa nusu ya watahaniwa wote wamefeli Mtihani huo. Aidha, Kamati Kuu imezingatia na kusikitishwa na taarifa kuwa ni asilimia 11.5 tu ya watahiniwa ndio waliopata daraja la I hadi la III. Ndio kusema kuwa karibu asilimia 90 ya vijana wote waliomaliza kidato cha nne mwaka 2010 hawawezi kuendelea na elimu yeyote ya juu na itakuwa ni vigumu sana kwa vijana hawa kupata aina yeyote ya ajira ya uhakika.
Aidha, Kamati Kuu imezingatia kuwa matokeo mabaya ya Kidato cha Nne yamesababishwa na sera dhaifu za serikali ya CCM zenye kulenga kughilibu wananchi kwa ajili ya mafanikio ya kisiasa kwa kukazania wingi wa majengo ya shule badala ya ubora wa walimu na ubora wa shule. Kutokana na hali hii:

  1. Kamati Kuu imeyatangaza matokeo ya Kidato cha Nne ya mwaka 2010 kuwa ni Janga la Kitaifa
  2. Kamati Kuu imeitaka Serikali ya CCM isione aibu kutekeleza sera za elimu za CHADEMA zilizoanishwa katika ilani yake ya mwaka 2010, ikiwemo sera ya kutoa elimu bure na kuboresha maslahi na mazingira ya kazi ya walimu ambazo zilielezwa na wataalamu wa elimu kwamba ndio sera sahihi za kufufua ubora wa elimu ya nchi yetu
  3. Kamati Kuu imeunda timu maalumu ya wataalamu wa elimu kwa ajili ya kutafiti kwa kina sababu za matokeo mabaya ya Kidato cha Nne na kutoa mapendekezo yake kwa Kamati Kuu katika kikao chake kitakachofanyika kabla ya Mwezi Mei 2011.
Kuhusu propaganda za udini hapa nchini

Kamati Kuu imesikitishwa na propaganda zinaendelezwa na viongozi wa juu wa Chama cha Mapinduzi, hususani Rais Kikwete, kuhusu kuwepo kwa mfarakano wa kidini hapa nchini. Kamati Kuu imezingatia kuwa wananchi wa Tanzania wameendelea kuishi kwa amani, upendo na mshikamano mkubwa bila kujali tofauti zao za kidini. Kamati Kuu imezingatia kuwa Viongozi wa juu wa CCM, na hasa Rais Kikwete, ameamua kuficha udhaifu wake wa kiuongozi chini ya zulia la udini ili wananchi waache kujadili mambo ya msingi ya Taifa hili, ikiwemo kushindwa kwa CCM kutekeleza ahadi ambazo imekuwa ikizitoa katika miongo mitano iliyopita. Hivyo basi:

  1. Kamati Kuu imewahimiza wananchi wa dini zote hapa nchini kuendelea kuishi kwa amani na mshikamano na kushirikiana katika shughuli mbalimbali za kiuchumi na kijamii bila kujali tofauti zao za dini, ukabila wala itikadi ya siasa
  2. Kamati Kuu imewataka viongozi wa juu wa CCM na hasa Rais Kikwete kuacha kuchochea mgawanyiko wa dini hapa nchini kama njia ya kuficha udhaifu wake wa uongozi
  3. Kamati Kuu imewahimiza viongozi wa dini zote hapa nchini kuendelea kukemea maovu yeyote katika jamii bila woga wala upendeleo kwani hilo ni jukumu lao la msingi.
 
Back
Top Bottom