Katoka sultani mwarabu waingia usultani wa mtu mweusi zanzibar

Mbunge

Senior Member
Aug 7, 2008
104
10
HALI ilivyo ni kuwa upo uwezekano mkubwa chini ya CCM Zanzibar isiyo na mwelekeo wala visheni ya kule visiwa vinavyokotakiwa kuwa baada ya 2015....sasa wanazua jambo juu ya jambo.

Nalo sio jingine ila lile la uwezekano wa kuwa na the Karume aristocracy in Zanzibar. Hivi tunahitaji tena uongozi wa kina Karume kweli visiwani. Na akingia Hali hii basi itakuja Hali ya Wajukuu wa Mzee Abedi nao kuwa maraisi na vitukuu wao na hili ndio sera ya serikali ya mapinduzi.

Wazanzibari wenzangu, ndugu zangu, wandani wangu haiwezekani kuwa na demokrasia ya kweli visiwani kwa sababu kwanza kuna kitu haramu ambacho kiko katika katiba. Nacho sio kingine ila ni kile kinachoitwa Baraza la Mapinduzi.

Bila baraza hilo kufutwa kikatiba sio rahisi kwa ujinga tuliokuwa nao Zanzibari kuhimili vishindo vya kushinikizwa na bara na viongozi wa visiwani wasiokuwa na sifa wala uwezo wa uongozi kuwa ndio viongozi wetu. Hili linafanyika wakati nusu ya Wazanzibari wenye uwezo wa uongozi mara 10 ya uwezo wa kina Karume wanatengwa kisiasa chini ya huruma, ulinzi na rehema ya CCM bara.
 
Kiongozi akiingia madarakani,watu wanataka kuona utendaji kazi wake. Kama ameingia kwa Demokrasia au kwa Mapinduzi;kama ana matatizo yoyote kama ana ugonjwa wa moyo,au matatizo yoyote ya mahusiano,watu hawajui hayo. Wao wanategemea mambo fulani kutoka kwa Rais wao,kutoka kwa mtu yeyote anayeitwa "Rais''. Kama akishindwa kutekeleza kwa sababu yoyote,watu watakuwa disappointed. If there is a problem,the President must step down.


''Some[Presidents] are well prepared, some are not; some
have enormous advantages, others have few; some seek the office, others
have it thrust on them. Often, however, expectations of performance are
uniform''
 
Mkuu si wanasema ana haki ya kuchukua fomu?
Kwa hiyo akigombea na akapitishwa na wajumbe wa halmashauri kuu watakuwa wameamua wao wajumbe.
 
Kwa maoni ya wa-zenj huu Usultani mweusi unafanyika kwa baraka ya Muungano, kwani chama tawala ndio wanachagua nani anewafaa kua kibaraka chao na kumtumia kwa remote control. Sasa wanaamini kua madam CCM inataka itawale daima, katu uchaguzi huru hautofanyika. Be prepare next generation kua na raisi wa zenj chotara wa ki-arabu.
 
HALI ilivyo ni kuwa upo uwezekano mkubwa chini ya CCM Zanzibar isiyo na mwelekeo wala visheni ya kule visiwa vinavyokotakiwa kuwa baada ya 2015....sasa wanazua jambo juu ya jambo.

Nalo sio jingine ila lile la uwezekano wa kuwa na the Karume aristocracy in Zanzibar. Hivi tunahitaji tena uongozi wa kina Karume kweli visiwani. Na akingia Hali hii basi itakuja Hali ya Wajukuu wa Mzee Abedi nao kuwa maraisi na vitukuu wao na hili ndio sera ya serikali ya mapinduzi.

Wazanzibari wenzangu, ndugu zangu, wandani wangu haiwezekani kuwa na demokrasia ya kweli visiwani kwa sababu kwanza kuna kitu haramu ambacho kiko katika katiba. Nacho sio kingine ila ni kile kinachoitwa Baraza la Mapinduzi.

Bila baraza hilo kufutwa kikatiba sio rahisi kwa ujinga tuliokuwa nao Zanzibari kuhimili vishindo vya kushinikizwa na bara na viongozi wa visiwani wasiokuwa na sifa wala uwezo wa uongozi kuwa ndio viongozi wetu. Hili linafanyika wakati nusu ya Wazanzibari wenye uwezo wa uongozi mara 10 ya uwezo wa kina Karume wanatengwa kisiasa chini ya huruma, ulinzi na rehema ya CCM bara

Mbunge,

Hakika umezungumza mambo takriban matatu katika bandiko lako.

Zanzibar hatuna tatizo kabisaaaa na akina Karume kugombea na hata kuchaguliwa kuwa viongozi kama WATAKUWA NA SIFA NA UWEZO WA KUONGOZA. Hakika Zanzibar tunataka kiongozi aliye shupavu, mwenye uwezo na sifa zote sahihi za uongozi na awe aliyechaguliwa na Wazanzibari wenyewe. Hatuna ubaguzi kwa hilo.

Demokrasia ya kweli Zanzibar itapatikana tu kama Katiba ya Zanzibar ifanyiwe marekebisho makubwa ingawa mimi ningependa iandikwe upya ili kukidhi mahitaji na matakwa ya jamii kwa sasa. hapo ndio tutakuwa wazi kabisa katika kulichambua BMZ na muundo mzima wa Serikali, Balaza la Wawakilishi na mfumo mzima wa mahakama.

Vile vile Znz itakuwa huru kuchagua viongozi wake bila kuingiliwa na Bara. hapo tutapata kiongozi safi, mwenye uwezo, aliye na sifa na aliye chaguo la wazanzibar.

Kinyume cha hapo tutaendelea kuchaguliwa viongozi na Bara.

Nasriyah.
 
Some people are just previliged and have more resources than others. Mfano tuchukulie Marekani. Bush mdogo won the presidency in large part because of his families position. He had the resources and political connects. On the other hand you might have someone like Obama who had no large capital, resources or political connections Bush had but he had other advantages which are natural charisma, a good campaign team and fund raising skills. My point being, mtu yoyote anaye taka chochote hato sita kutumia the resources they have. Wakina Karume ni kama Bush, their biggest resource is their name. So you can't blame themfor trying to use it. Kinacho takiwa ni mtu makini na mwenye uwezo wa kuongoza. So let's judge the Karumes according to their talents and skills and not by their name.
 
usishangae sana kuhusu usultan ndugu yangu kwani hata mkikwepa la Karume basi ujue la Mwishi ambaye ni waziri wa ulinzi hamuwezi kulikwepa, akishindwa kupata Karume Balozi basi jiandaeni na Mwinyi waziri mtoto wa Mzee Ali Hassani Mwinyi hii ndio Tanzania ya watu wachache kuhodhi madaraka kwa kisingizio cha kulinda serikali ya mapinduzi ya Zanzibar au kwa kulinda amani ya Tanzania wakati watu wakijenga nyumba wanazungusha kuta sasa amani ipo wapi? waende Canada waone maaana ya amani hakuna maukuta makubwa yanayozunguka nyumba ukiona kuta ujue hakuna amani
 
pia la msingi la kuangalia hapa ni je huyo karume balozi ana elimu gani? anao uwezo wa kuongoza? je keshaifanyia nini Zanzibar katika maisha yake? je ni mtu mpenda maendeleo ya wana zanzibar au ni mtu anayetafuta u rais ili tu awe kwenye kumbukumbu za historia kuwa alishawahi kuwa rais wa Zanzibar? nyie wazanzibar ndo mnamjua tuambieni ili tuunganishe nguvu za kumpinga kama hafai na kumuunga mkono kama anafaa, jina au ukoo sio tatizo ni uwezo wa kiongozi tunaoungalia
 
watanzania inabidi sasa tujifunze kupambanua mambo tusifanye au kujenga hoja kwenye mtandao bila ushahidi au kufanya research kuhusu hilo jambo.
wazanzibar mnao lalamika kuhusu karume balozi je mlifanya research mkagundua kuwa hafai kiuongozi? au tu ni kwa kuwa yeye amezaliwa na mzee karuma, na kwa kuwa babake alishawahi kuwa rais na kakake pia basi yeye hana haki ya kuwa rais? nani kasema hilo? imeandikwa wapi kwenye katiba ya Jamuhuri ya muungano wa Tanzania au hata kwenye katiba ya marekani? hajaona marekani bushi baba na bushi mwana? na hamkuona Clinton mume na kidogo clinton mke naye awe rais? ni kwa kuwa katiba inampa kila mmoja haki sawa ya kugombea kuwa rais na kuchagua rais ampendaye
 
Demokrasia ni pamoja na kuwa na haki kwa kila mtu anayetimiza masharti ya kugombea (Diwani, Bunge, Rais) agombee anapotaka. Na atakapojitokeza kugombea aondolewe kwa taratibu zilizowekwa, na si kusema eti hafai kwa kuwa Baba na Kaka yake wamewahi kuwa maRais.
 
tatizo lako wewe hujui karume balozi huyu ameshawahi kuua kwa kurepu mtu huu na ndio maana akatoroshwa na kupewa ubalozi na kumbuka magereza imebadilishwa jina kwa nini kikaitwa chuo cha mazunzo sababu ya huyu kuua ikaonekana itakuwa soo ndio ikabadilishwa jina huyu ni muuaji alimuua mtoto wa kike pale maisara anaitwa shadia uliza uambiwe na sio kurukia tu hakuna tatizo ikiwa ukoo mmoja watakuwa wote marais poa hata wajukuu pia na weje kuwa marais lakini basi hakuna mwengine lazima wawe ni wao kisa baba alikuwa ni mmoja wa aliye pindua hujui historia ya znz lakini ujue kuna makubwa zaidi yatatokea sasa ukoo huu kazi yao ni kuua karime ni muuaji watoto wa karume ni wauaji wajukuu itakuwaje mbona nyinyi bara hamkumuunga mkono awe rais
 
hali ilivyo ni kuwa upo uwezekano mkubwa chini ya ccm zanzibar isiyo na mwelekeo wala visheni ya kule visiwa vinavyokotakiwa kuwa baada ya 2015....sasa wanazua jambo juu ya jambo.

Nalo sio jingine ila lile la uwezekano wa kuwa na the karume aristocracy in zanzibar. Hivi tunahitaji tena uongozi wa kina karume kweli visiwani. Na akingia hali hii basi itakuja hali ya wajukuu wa mzee abedi nao kuwa maraisi na vitukuu wao na hili ndio sera ya serikali ya mapinduzi.

Wazanzibari wenzangu, ndugu zangu, wandani wangu haiwezekani kuwa na demokrasia ya kweli visiwani kwa sababu kwanza kuna kitu haramu ambacho kiko katika katiba. Nacho sio kingine ila ni kile kinachoitwa baraza la mapinduzi.

Bila baraza hilo kufutwa kikatiba sio rahisi kwa ujinga tuliokuwa nao zanzibari kuhimili vishindo vya kushinikizwa na bara na viongozi wa visiwani wasiokuwa na sifa wala uwezo wa uongozi kuwa ndio viongozi wetu. Hili linafanyika wakati nusu ya wazanzibari wenye uwezo wa uongozi mara 10 ya uwezo wa kina karume wanatengwa kisiasa chini ya huruma, ulinzi na rehema ya ccm bara.

tatizo kuwa zanzibar haiko huru kuchaguwa wampendae>
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom