Katika wachafu mia, Je msafi mmoja ataonekana?

Aventus

JF-Expert Member
Mar 8, 2013
1,914
1,977
KATIKA WACHAFU MIA MSAFI MMOJA ATAONEKANA???

Najiuliza kimyakimya wanatokea makwapurwa mia lakini ndani yao kuna msafi mmoja tu utamwona?

Na mpaka umwone huyu ni msafi ama anaafadhali lazima ufanye shughuli ya ziada.

Katika kundi la wapinga nduru(kelele)mia je ni rahisi kumwona mtulivu mmoja? Wote hao kila kitu ni NDIO MZEE.we ukisema hapana hata kwa kupayuka hutasikika.

Katika familia ya watu mia ukiwa huna mamlaka yeyote na hupendezwi na uwongozi wa hiyo familia uwezi tu kukurupuka na kusema sipendezwi na sikubaliana na huo uwongozi mana hutasikilizwa.

Lazima uwe na strategize. Unakubaliana nao kwa kila jambo.Unaweka mkakati thabiti ili uweze kukamata uwongozi wa juu.ukishapata sasa unaweza kubadili mfumo.

JE, KAMA NI WEWE MSAFI MMOJA UNAWEZA KUWASHAWISHI WACHAFU MIA WAWE WASAFI?
 
Back
Top Bottom