Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,529
Guys... Who is legal advisor wa Rais Magufuli? Au advisor wa namna yeyote ile?
Hii ziara ya Pwani yametokea matamko ya Rais ya kusema "katika utawala wangu" but kwangu naona hakuna jitihada kuweka mfumo, kanuni Na Sheria Imara zinazoeleweka ili uwajibikaji uwe ni kitu Na tunu ya kawaida si mfumo w utegemezi wa kiongozi mkuu wa nchi au hamasa yake kuongoza Na "kunyoosha" Taifa!
JPM alipokujaa alishangaa kukuta madudu na machafu kupindukia, sababu yawezekana sana kuwa JK naye alisema "katika utawala wangu" akajifanyia mambo Na maamuzi mengi ambayo Magufuli anayashangaa.
Labda naye Kikwete alikuta aliyoyarithi ambayo yalifanywa kwa mantiki ya "katika utawala wangu.." iwe ni Serikalini au hata katika Chama.
Leo Magufuli anaongoza nchi na kufanya kila kitu kwa kigezo cha "katika utawala wangu"
Kesho akiondoka Magufuli, atakayekuja naye atasema "katika utawala wangu" na kubadilisha Yale yaliyofanya "katika utawala wangu" wa Magufuli !
Now nikiangalia kwa nini kuna non-responsive kutoka taasisi, mashirika, Serikali, watendaji Na hata wananchi, jibu lake ni kila mtu anajua "katika utawala wangu" utapita Na kuna expiry date Na si mfumo unaoeleweka kisheria... Wanapuuzia wanajua wakisema "ametukuta, ataondoka, atatuacha"!
Nchi imekuwa ikiendeshwa au kuongozwa na maamuzi kufanywa kwa dhana na fikra za "katika utawala wangu.." kuanzia Rais mpaka Mkuu wa Wilaya au hata mwenyekiti wa kijiji kupuuzia kabisa mipaka ya kisheria, mamlaka,kanuni hata katiba.
Zaidi, dhana hii ya "Katika utawala wangu.." si kwamba imekwamisha maendeleo ya jamii na Taifa, lakini hata imepunguza uwajibikaji wa kweli, kujenga kiburi nauungwana wa kukiri makosa, kujikosoa au kujisahihisha kunakosekana.
Mfano inawezekana DC wa Hai juzi akivunjavunja shamba la Mbowe alitumia kigezo hicho cha "katika utawala wangu.." au leo Mkuu wa TRA Arusha anaposema ukikutwa huna risiti fainielfu thelathini, naye anatumia nguvu ya "katika utawala wangu".
Keshoanapokuja mtendaji au kiongozi mwingine naye akasema "katika utawala wangu" (mfano mzuri ni Nape na Mwakyembe wizara ya habari) naye akaamua kusema anabadilisha na kufuta kila kilichofanywa na aliyemtangulia kwa kuwa "katika utawala wangu" haoni manufaa.
Kuna tofauti ya kufanya mambo "katika utawala wangu" kama mambo hayo hayahusu kanuni, sheria, taratibu, katiba au maamuzi yenye impact kubwa kwa jamii na Serikali.
Ni haki kusema "katika utawala wangu" uvivu,uzembe, ubabaishaji, uchelewaji, umangimeza, uhujumu nu mwiko na kamwe hautavumiliwa. Lakini kuna haja ya kuweka na kurejea misingi iliyopo na kuhoji kwa nini utovu wa nidhamu upo na au unaongezeka!
Leo Rais Magufuli kawasema Brela mpaka kutoa tamko (presidential executive order) verbally kuwa wenye nia ya kuanzisha viwanda au biashara wasisubiri Brela, waanze mchakato maana Brela wanajivutavuta na kupunguza kasi ya maendeleo na azma ya viwanda ya awamu ya tano. Najiuliza je kwa nini Brela leo ni miezi 20 tangu awamu ya Tano iingie madarakani bado inajivutavuta na kuwa na umangimeza au ukiritimba ambao unakwamisha ufanisi? je hawana kanuni za uwajibikaji? au usimamizi wa kanuni za uwajibikaji na majukumu zina mapengo na mianya ya uzembe, uhujumu au hata kulea rushwa na kero?
Je yawezekana huko Brela hakuna hizi kanuni kwa kuwa kila mkubwa wa sehemu anafanya mambo ya "katika utawala wangu" na kujiamulia mambo na wafanyakazi wa chini kwa kukosa mfumo unaoeleweka na kushuhudia kwao wakubwa wakifanya mambo kwa itikadi ya "katika utawala wangu" basi wanajijengea kiburi cha "alitukuta, atapita, atatuacha hapahapa"?
May be tukiongelea mambo kwa mtazamo huu, ubishi na ushabiki unaopinga kujengwa kwa mfumo huru Imara kuanzia Katiba, Sheria na Kanuni hata uwajibikaji wake utaangalia mambo kiuhalisia Na si kushangilia current happenings ambazo "baada ya utawala wangu" tutarudi kule kule au atakuja mwingine na mtazamo wake na kusema "katika utawala wangu"?
Hii ziara ya Pwani yametokea matamko ya Rais ya kusema "katika utawala wangu" but kwangu naona hakuna jitihada kuweka mfumo, kanuni Na Sheria Imara zinazoeleweka ili uwajibikaji uwe ni kitu Na tunu ya kawaida si mfumo w utegemezi wa kiongozi mkuu wa nchi au hamasa yake kuongoza Na "kunyoosha" Taifa!
JPM alipokujaa alishangaa kukuta madudu na machafu kupindukia, sababu yawezekana sana kuwa JK naye alisema "katika utawala wangu" akajifanyia mambo Na maamuzi mengi ambayo Magufuli anayashangaa.
Labda naye Kikwete alikuta aliyoyarithi ambayo yalifanywa kwa mantiki ya "katika utawala wangu.." iwe ni Serikalini au hata katika Chama.
Leo Magufuli anaongoza nchi na kufanya kila kitu kwa kigezo cha "katika utawala wangu"
Kesho akiondoka Magufuli, atakayekuja naye atasema "katika utawala wangu" na kubadilisha Yale yaliyofanya "katika utawala wangu" wa Magufuli !
Now nikiangalia kwa nini kuna non-responsive kutoka taasisi, mashirika, Serikali, watendaji Na hata wananchi, jibu lake ni kila mtu anajua "katika utawala wangu" utapita Na kuna expiry date Na si mfumo unaoeleweka kisheria... Wanapuuzia wanajua wakisema "ametukuta, ataondoka, atatuacha"!
Nchi imekuwa ikiendeshwa au kuongozwa na maamuzi kufanywa kwa dhana na fikra za "katika utawala wangu.." kuanzia Rais mpaka Mkuu wa Wilaya au hata mwenyekiti wa kijiji kupuuzia kabisa mipaka ya kisheria, mamlaka,kanuni hata katiba.
Zaidi, dhana hii ya "Katika utawala wangu.." si kwamba imekwamisha maendeleo ya jamii na Taifa, lakini hata imepunguza uwajibikaji wa kweli, kujenga kiburi nauungwana wa kukiri makosa, kujikosoa au kujisahihisha kunakosekana.
Mfano inawezekana DC wa Hai juzi akivunjavunja shamba la Mbowe alitumia kigezo hicho cha "katika utawala wangu.." au leo Mkuu wa TRA Arusha anaposema ukikutwa huna risiti fainielfu thelathini, naye anatumia nguvu ya "katika utawala wangu".
Keshoanapokuja mtendaji au kiongozi mwingine naye akasema "katika utawala wangu" (mfano mzuri ni Nape na Mwakyembe wizara ya habari) naye akaamua kusema anabadilisha na kufuta kila kilichofanywa na aliyemtangulia kwa kuwa "katika utawala wangu" haoni manufaa.
Kuna tofauti ya kufanya mambo "katika utawala wangu" kama mambo hayo hayahusu kanuni, sheria, taratibu, katiba au maamuzi yenye impact kubwa kwa jamii na Serikali.
Ni haki kusema "katika utawala wangu" uvivu,uzembe, ubabaishaji, uchelewaji, umangimeza, uhujumu nu mwiko na kamwe hautavumiliwa. Lakini kuna haja ya kuweka na kurejea misingi iliyopo na kuhoji kwa nini utovu wa nidhamu upo na au unaongezeka!
Leo Rais Magufuli kawasema Brela mpaka kutoa tamko (presidential executive order) verbally kuwa wenye nia ya kuanzisha viwanda au biashara wasisubiri Brela, waanze mchakato maana Brela wanajivutavuta na kupunguza kasi ya maendeleo na azma ya viwanda ya awamu ya tano. Najiuliza je kwa nini Brela leo ni miezi 20 tangu awamu ya Tano iingie madarakani bado inajivutavuta na kuwa na umangimeza au ukiritimba ambao unakwamisha ufanisi? je hawana kanuni za uwajibikaji? au usimamizi wa kanuni za uwajibikaji na majukumu zina mapengo na mianya ya uzembe, uhujumu au hata kulea rushwa na kero?
Je yawezekana huko Brela hakuna hizi kanuni kwa kuwa kila mkubwa wa sehemu anafanya mambo ya "katika utawala wangu" na kujiamulia mambo na wafanyakazi wa chini kwa kukosa mfumo unaoeleweka na kushuhudia kwao wakubwa wakifanya mambo kwa itikadi ya "katika utawala wangu" basi wanajijengea kiburi cha "alitukuta, atapita, atatuacha hapahapa"?
May be tukiongelea mambo kwa mtazamo huu, ubishi na ushabiki unaopinga kujengwa kwa mfumo huru Imara kuanzia Katiba, Sheria na Kanuni hata uwajibikaji wake utaangalia mambo kiuhalisia Na si kushangilia current happenings ambazo "baada ya utawala wangu" tutarudi kule kule au atakuja mwingine na mtazamo wake na kusema "katika utawala wangu"?