Katika mazingira haya, tutarajie nini?

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,172
7,428
germinated-seed.jpg
Katika Mazingira ambayo tunalalamika kwa yale yanayotokea lakini hatufanyi chochote ili kesho na kesho kutwa yasitokee tena, tutarajie nini?

Katika mazingira ambayo hata mtu akianzisha mjadala wa maana; Watanzania hawataki hata kuchangia achilia mbali kuchukua hatua; tutarajie nini?

Katika mazingira ambayo hakuna kuaminiana na ikitokea mtu anaaminiwa anageuka na anakuwa haaminiki, tutarajie nini?

Katika mazingira ambayo watanzania wengi hujikuta wakivutiwa na kutumia muda mwingi zaidi kufuatilia na kujadili udaku kuliko mambo ya msingi, tutarajie nini?

Katika mazingira ambayo kila mtu humfanyia mwenzake unafiki huku akidhani mwenzake ni mwaminifu kumbe naye mnafiki pia tutarajie nini?

Katika mazingira ambayo mwananchi na kiongozi wake wote wanaamini siasa ni ulaghai na uongo, na kupata nafasi ya uongozi maana yake ni "kuula" tutarajie nini?

Katika mazingira ambayo hakuna mtu ambaye ana hisia za ndani za kutenga angalau masaa mawili kila siku kufanya kitu chenye manufaa kwa wengine, tutarajie nini?

Dunia kwa asili yake haitupi kile tunachotamani, bali kile tunachostahili. Kujua ni kipi tunachostahili tunatakiwa tuangalie ni kipi tunapanda kwa kuwa apandacho mtu ndicho avunacho.Usifikirie atapanda mwenzako, panda wewe ili baadae tukutane kwenye kuvuna, ila kama kila mtu akidhani mwenzake atapanda, mwishowe unaweza ukakuta hakuna aliepanda, au aliepanda kapanda miiba.

Nchi hii ipo hivi leo kwa kuwa tumeamua kuwa hivi tulivyo na vile itakavyokuwa kesho, itategemeana na vile tutakavyoamua kuwa sasa. Ikumbukwe kesho huandaliwa leo. Kama hatuwazi kesho na kesho kutwa tunataka tuweje kama nchi, tunafanyaje ili tuwe na tukaanza kufanya; hali tutakayokutana nayo sasa na baadae hakutakuwa na wakumlalamikia kwa kuwa ndicho tutakachokuwa tumejichagulia.

Kila mtu aanze kutimiza wajibu wake sasa wakati anasoma uzi huu na wewe ukifanya na mwingine na mwingine hatimaye tutakuwa tunasogea lakini tukiendelea hivi hivi tutakuwa tunaendelea kupita njia mbaya.
 
mkuu tengeneza maisha yako na familia yako
watanzania michosho sana
unamwamini leo lakini kesho anakugeuka
tena nakushauri acha kuamini wanasiasa ingawaje kwa bahati mbaya ndio wanaendesha dunia

PERIOD!

Umemaliza kila kitu hapo mkuu, hii nchi saizi pambana mkeo, watoto na familia yako kwa ujumla waishi vizuri tu basi, ukijifanya mjuaji kwenye huu utawala utakuja kuwapa shida ndugu zako tu.
 
mkuu tengeneza maisha yako na familia yako
watanzania michosho sana
unamwamini leo lakini kesho anakugeuka
tena nakushauri acha kuamini wanasiasa ingawaje kwa bahati mbaya ndio wanaendesha dunia
Mkuu, naomba nikushawishi ubadili fikra hii. kwa sababu zifuatazo.

1. Maisha ya binadamu yanategemeana sana. Wewe unakuwa kama ulivyo kwa sababu pamoja na mambo mengine kuna watu wengine wanasababisha kwa namna moja amma nyingine uwe kama ulivyo ama moja kwa moja au kwa kutengeneza mifumo fulani.

2. Binadamu hawezi kujitosheleza kila kitu mwenyewe, hata uwe mtu wa namna gani lazima utategemea vitu vingine kwa watu wengine ili uweze kuishi maisha yenye heshima. Kwa hiyo uwepo na ustawi wa ngenine unakuwa ni muhimu.

3. Lengo la kuumbwa mwanadamu sio kujipigania mwenyewe bali kufanya vitu ambavyo vitasaidia wengine, kwa maana kwamba kila mtu akifanya hivyo hatimaye ndio dunia inaweza kuwa sehemu salama ya kuishi. Vinginevyo itakuwa sehemu yenye machafuko na maisha hayatawezekana.

4. Jiulize kama kila mtu angeamua awe anajiangalia mwenyewe tu, wewe mwenyewe tu ungekuwepo duniani? vitu ulivyonavyo ungekuwa navyo?
 
PERIOD!

Umemaliza kila kitu hapo mkuu, hii nchi saizi pambana mkeo, watoto na familia yako kwa ujumla waishi vizuri tu basi, ukijifanya mjuaji kwenye huu utawala utakuja kuwapa shida ndugu zako tu.
Ukiona unaishi vizuri na uko salama na familia yako; ujue kuna watu wako mahali wanatumia muda, akili, nguvu na rasilimali ili uweze kuishi hivyo unavyoishi. Nao kama wakiamua wajiangalie wao wenyewe tu, hayo maisha mazuri hayawezi kutokea. Hata hizo njia unazodhani utapita ili kufikia hayo maisha mazuri zitakuwa hazipitiki. Sehemu ya vikwazo unavyokumbana navyo hata sasa; miongoni mwa mambo mengine, vinasababishwa na watu ambao wameamua kupigania maslahi yao tu bila kujali madhara yanayoweza kutokea kwa wengine.

Sasa kama unaamini kuwa watu wengine pamoja na mambo mengine wanalo jukumu la kutengeneza mazingira ambayo yatakusaidia wewe kufikia hayo maisha mazuri unayoyaota, amini pia nawe una wajibu wakutoa mchango wako kuwasaidia wengine nao kupifikia hayo maisha mazuri. Ni msingi huo unaoturudisha kwenye tafakuri ya uzi wa msingi.

Ukitaka kulielewa hili vizuri, jiulize tu hivi lengo la Mungu kukuumba ni nini? je? ni ili uje kulalamika? je? ili uje kulaumu wengine? je? ni ili uhujumu wengine? ni ili uje uishi maisha mazuri kama unavyosema? lakini kama ni kuishi maisha mazuri, unayatamani tu hayo haisha kisha hutokea au kuna vitu unatakiwa kufanya na wengine wafanye pia ili yatokee?
 
Nakupa siri ya mafanikio, usijihangaishe kuibadirisha Tanzania au Africa, jikite kuboresha familia yako, jikite kuwashauri wanao na kuwalea vema, jikite kuweka akiba kwa ajili ya uzeeni,

Jifanye huwasikii wanasiasa
 
Nakupa siri ya mafanikio, usijihangaishe kuibadirisha Tanzania au Africa, jikite kuboresha familia yako, jikite kuwashauri wanao na kuwalea vema, jikite kuweka akiba kwa ajili ya uzeeni,

Jifanye huwasikii wanasiasa
Hiyo hela unayoitumia kuna mtu anaitengeneza. Hiyo akiba unayoisema kuna mtu anaiweka. Kama kila mtu akiamua kutizama mambo katika level hiyo unayoisema; unaweza kuweka hakiba na siku ukiita usipewe. hapo vipi? utafanya nini? ili uipate hiyo hela ya kuweka hakiba, uweke akiba bila kuibiwa, na siku ukiitaka uipate, kuna watu wengi hushiriki kwenye zoezi hilo na wakiwa "corrupt" au na mtizamo kama huu unaousisitiza, hutafanikiwa hata ufanye nini. Ni katika mazingira kama hayo ambapo huwezi kuikwepa siasa.

Katika mambo ambayo watu wengi tunakosea; ni kudhani tunaweza kuikwepa siasa hali ya kuwa bado tuko hai duniani. Mkuu maadamu tuko duniani, maisha yetu kwa kukusudia au bila kukusudia, kwa kupenda au bila kupenda ni "ya kisiasa" na hakuna namna tunaweza kujitoa humo. Tunachoweza kufanya ni kuhakikisha tunakuwa na jamii ya watu wazuri ili pia tuwe na siasa nzuri.

Wazo lako ni kama kale ka msemo ka "ukiona maisha yanakuzingua achana nayo fanya ishu nyingine"
 
Dispiline kwenye mambo madogo madogo ambayo tunayafanya kwenye maisha yetu ya kila siku ndio hiyo hiyo hutujengea nidhamu kwenye mambo makubwa au hata tunapokuwa na majukumu makubwa zaidi. Kama hauwezi kujenga nidhamu kwenye vitu vidogo vidogo vya kila siku, hauwezi ukawa na nidhamu kwenye mambo makubwa. Ni kwa namna hiyo taifa bora au lisilobora hujengeka.

Kuna vitu vidogo vidogo tu ambavyo viko ndani ya uwezo wa kila mmoja wetu ambavyo kama kila mmoja angevifanya, kama taifa tungefika mbali sana, lakini tunakosa nidhamu binafsi na msukumo wa kuchagua kuvifanya.Mwishowe tunawaza mambo makubwa ambayo yako nje ya uwezo wetu na kuishia kulaumu na kulalamika.

Ndugu zangu watanzania; kwa kuanzia tuanze tu kwa kuangalia vitu kwa jicho positive, tuanze kutoa maoni positive kwenye vitu, matukio , mijadala mitizamo na michango yetu kuelekea tule tunakotaka kwenda. Hata kama kitu kinachotokea, ni negative; kila mtu afanye linalowezekana kukibadili taratibu taratibu ili kisiendelee kutokea negatively au kupunguza negativity. Haijalisihi ni kwa kiasi au kasi gani mtu unachangia kusababisha mabadiliko; jambo la msingi ni kuchangia kwa kadiri uwezavyo. Hiyo ndio njia pekee itakayotusaidia kuifanya nchi hii iwe bora zaidi siku hadi siku. Kinyume chake kwa kadiri tunavyoongeza negativity ndivyo tunakavyoelekea kwenye negative side ambayo wote tunakubaliana kuwa "it is undesirable"

Wala kinachoweza kutusaidia kwenye nchi hii si kubadilisha viongozi au vyama. Watanzania wengi tuna tatizo kubwa juu ya namna tunavyoitazama dunia, maisha na nafasi pamoja na mchango tunaopaswa kutoa tukiwa duniani. Hapo ndipo tatizo la msingi lilipo.
 
Dispiline kwenye mambo madogo madogo ambayo tunayafanya kwenye maisha yetu ya kila siku ndio hiyo hiyo hutujengea nidhamu kwenye mambo makubwa au hata tunapokuwa na majukumu makubwa zaidi. Kama hauwezi kujenga nidhamu kwenye vitu vidogo vidogo vya kila siku, hauwezi ukawa na nidhamu kwenye mambo makubwa. Ni kwa namna hiyo taifa bora au lisilobora hujengeka.

Kuna vitu vidogo vidogo tu ambavyo viko ndani ya uwezo wa kila mmoja wetu ambavyo kama kila mmoja angevifanya, kama taifa tungefika mbali sana, lakini tunakosa nidhamu binafsi na msukumo wa kuchagua kuvifanya.Mwishowe tunawaza mambo makubwa ambayo yako nje ya uwezo wetu na kuishia kulaumu na kulalamika.

Ndugu zangu watanzania; kwa kuanzia tuanze tu kwa kuangalia vitu kwa jicho positive, tuanze kutoa maoni positive kwenye vitu, matukio , mijadala mitizamo na michango yetu kuelekea tule tunakotaka kwenda. Hata kama kitu kinachotokea, ni negative; kila mtu afanye linalowezekana kukibadili taratibu taratibu ili kisiendelee kutokea negatively au kupunguza negativity. Haijalisihi ni kwa kiasi au kasi gani mtu unachangia kusababisha mabadiliko; jambo la msingi ni kuchangia kwa kadiri uwezavyo. Hiyo ndio njia pekee itakayotusaidia kuifanya nchi hii iwe bora zaidi siku hadi siku. Kinyume chake kwa kadiri tunavyoongeza negativity ndivyo tunakavyoelekea kwenye negative side ambayo wote tunakubaliana kuwa "it is undesirable"

Wala kinachoweza kutusaidia kwenye nchi hii si kubadilisha viongozi au vyama. Watanzania wengi tuna tatizo kubwa juu ya namna tunavyoitazama dunia, maisha na nafasi pamoja na mchango tunaopaswa kutoa tukiwa duniani. Hapo ndipo tatizo la msingi lilipo.
Kwa ulipo malizia ndio kina mantiki.

Unafikiri huu ukweli jawauju?? Watanzania walio wengi hasa wenye ujuzi hii point uliyomaliza nayo wanaielewa lakini hawataki ifuatwe na watanzania

Ni vigumu sana kuishi nje ya siasa, lakini wanasiasa wanaitumia hii falsafa kujinufaisha. Wengi hutuaminisha kuwa chama au mtu furani ndio atatuletea maendeleo

Wanasiasa walio wengi bahati mbaya ni wale wenye nafasi ya kuamini sana, mfano mtu ni mtaalam wa uchumi lakini ni mwanasiasa ambaye anayo nafadi ya kuamini na sisi wanainchi hohe hahe, lakini hatatwambia ukweli kwa nini sisi ni masikini na tunapaswa kufanya.
Kitakachofuatia ataitumia hii fulsa kumchafua mwanasiasa mwingine na kujivutia nafasi yake yeye.

Hapa tutaaminishwa kuwa tukichagua chama fulani ama mtu fulani maisha yetu yatakuwa bora iki hali ukweli unajulikana. Ukizisikiliza siasa zetu unaweza sema chama fulani cha siasa kimetunza maisha bora yetu mifukoni mwao, siku kikichaguliwa tutakabidhiwa maisha yetu yakiwa bora.

Wanasiasa wengine wanalitambua kabisaa kuwa mabadiliko huanza taratibu kutoka vichwani mwa wanainchi, yasni mwanainchi mwenyewe aweze kuthamini hata kike kitu kidoogo saana anachoweza kufanya na amini ndio hatua ya mabadiliko.

Tukiamini ya kuwa mabadiliko hayaanzi baada ya chaguzi baaso amini na kwambia kuwa tutaipiga hatua kubwa sana..

Ifikie hatua jukumu la mabadiliko na ukombozi wa maisha ya mtanzania akabidhiwe yeye mwenyewe ajue kuwa mabadiliko huanza na yeye. Kwa bahati mbaya saana, siasa zetu nchini hazilitaki hili lieleweke ndio maana ujiwasikiliza wanasiasa kwa kutumia ngoma ya sikio huku ukimtizama kwa jicho la tatu, utagundua kuwa wote wanaingana katika kuuficha ukweli huu, awe mpinzani ama chama tawala hawa huwa wanaungana kumficha mtz ukweli huu.

Kwa nini wanafanya hivi?

Wanasiasa waliowengi hutegemea ujinga wa watanzania kutoelewa hili jukumu na kuitumia kama mtaji katika shuguri zao za kisiasa.

Katika mantiki hiyo ndio wanasiasa hulaumiwa lakini kwa bahati mbaya huwa hawapendi lawama zao zijulikane.
Hapa ndio maana baadhi ya wajuvi wa mambo hujitaidi saana kutowaamini wanasiasa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mkuu tengeneza maisha yako na familia yako
watanzania michosho sana
unamwamini leo lakini kesho anakugeuka
tena nakushauri acha kuamini wanasiasa ingawaje kwa bahati mbaya ndio wanaendesha dunia
Kungekuwa Petition ya Kuzia wanasiasa na fablications zao,ingekuwa poa sana,lakini kusini mwa jangwa la sahara excepy SA kuna shida sana.
 
Sawa ila tuwafanye nini viongozi ambao wanatugawa?
Swali la kwanza lisiwe "tuwafanyaje" swali la kwanza ujiulize wewe kama wewe unafanya nini kama mchango wako ili kusababisha mambo kadhaa mazuri yatokee, au kusaidia kuwaunganisha hao unaodhani wamegawanywa. Ukianza kusema ni wao, na kila mtu akasema ni wao mwishowe hakuna anayefanya kitu na anayefanya anaweza kufanya kitu cha kuharibu zaidi ya kujenga. Tatizo linaanzia pale kila mtu anapodhani ni mwenzake.
 
Na kumlamu mwenzako kuwa amepanda au anapanda mbegu mbaya wakati wewe nawe unapanda hiyo hiyo au haupandi chochote, sio sawa maana ikifika muda wa kuvuna hicho hicho kilichopandwa ndicho kitakachokuwepo kwa wote.
 
PERIOD!

Umemaliza kila kitu hapo mkuu, hii nchi saizi pambana mkeo, watoto na familia yako kwa ujumla waishi vizuri tu basi, ukijifanya mjuaji kwenye huu utawala utakuja kuwapa shida ndugu zako tu.
Una mawazomgando na ya hovyo kabisa, unadhani utafanikiwa kama nchi haitakaa sawa??acha ubinafsi wa kiafrika
 
Una mawazomgando na ya hovyo kabisa, unadhani utafanikiwa kama nchi haitakaa sawa??acha ubinafsi wa kiafrika

Haha pole sana mkuu, najua una hasira na uchungu wa nchi yako ila haya mambo hayahitaji hasira wala mihemko kwasababu haitosaidia kitu,
By the way huu ni mtazamo wangu tu.

CHILL.
 
He! Azizi Musa hongera, bahati mbaya JF utani mwingi, tafadhali wenye hekima zenu endeleeni kuweka peupe muda si mrefu yatatimia kwa kuwa mnapanda mbegu njema!!! (ebu angalia katika andiko lako ..............taratibu taratibu ili kisiendelee kutokea 'positevely' ( sio 'negatively?') au kupunguza 'positivity'. Tuweke sawa ndugu.)
 
germinated-seed.jpg
Katika Mazingira ambayo tunalalamika kwa yale yanayotokea lakini hatufanyi chochote ili kesho na kesho kutwa yasitokee tena, tutarajie nini?

Katika mazingira ambayo hata mtu akianzisha mjadala wa maana; Watanzania hawataki hata kuchangia achilia mbali kuchukua hatua; tutarajie nini?

Katika mazingira ambayo hakuna kuaminiana na ikitokea mtu anaaminiwa anageuka na anakuwa haaminiki, tutarajie nini?

Katika mazingira ambayo watanzania wengi hujikuta wakivutiwa na kutumia muda mwingi zaidi kufuatilia na kujadili udaku kuliko mambo ya msingi, tutarajie nini?

Katika mazingira ambayo kila mtu humfanyia mwenzake unafiki huku akidhani mwenzake ni mwaminifu kumbe naye mnafiki pia tutarajie nini?

Katika mazingira ambayo mwananchi na kiongozi wake wote wanaamini siasa ni ulaghai na uongo, na kupata nafasi ya uongozi maana yake ni "kuula" tutarajie nini?

Katika mazingira ambayo hakuna mtu ambaye ana hisia za ndani za kutenga angalau masaa mawili kila siku kufanya kitu chenye manufaa kwa wengine, tutarajie nini?

Dunia kwa asili yake haitupi kile tunachotamani, bali kile tunachostahili. Kujua ni kipi tunachostahili tunatakiwa tuangalie ni kipi tunapanda kwa kuwa apandacho mtu ndicho avunacho.Usifikirie atapanda mwenzako, panda wewe ili baadae tukutane kwenye kuvuna, ila kama kila mtu akidhani mwenzake atapanda, mwishowe unaweza ukakuta hakuna aliepanda, au aliepanda kapanda miiba.

Nchi hii ipo hivi leo kwa kuwa tumeamua kuwa hivi tulivyo na vile itakavyokuwa kesho, itategemeana na vile tutakavyoamua kuwa sasa. Ikumbukwe kesho huandaliwa leo. Kama hatuwazi kesho na kesho kutwa tunataka tuweje kama nchi, tunafanyaje ili tuwe na tukaanza kufanya; hali tutakayokutana nayo sasa na baadae hakutakuwa na wakumlalamikia kwa kuwa ndicho tutakachokuwa tumejichagulia.

Kila mtu aanze kutimiza wajibu wake sasa wakati anasoma uzi huu na wewe ukifanya na mwingine na mwingine hatimaye tutakuwa tunasogea lakini tukiendelea hivi hivi tutakuwa tunaendelea kupita njia mbaya.
Waafrika wengi wana ubinafsi sana. Mfano mtu hawezi panda mti ambao mavuno yake yatapatikana akiwa mzee au amekufa (ataona kuwa huo mti hautamfaidisha), Vivyo hivyo hata kuweka mambo yetu ya kisiasa, kiuchumi na kiutamaduni watu wanajitazama wao na familia zao tu pasipo kuangalia mustakabari wa baadaye wa watoto wetu na watoto wao baadaye.

Unaweza ukawa una unafuu wa maisha na ukajaribu kuongea na mtu mwenye hali mbaya kimaisha juu ya mfano siasa na jinsi zinavyo athili maisha yake, lakini hawezi kukuelewa na kukwambia hata wakija wengine watakuwa hivyo hivyo. Wengi wao wako hivyo, unachofanya nawe nikuamua kuangalia maisha yako tu. Ni kweli kuna athali baadaye lakini utakuta huna jinsi ya kufanya ingawa baadaye kuna madhara makubwa yanaweza kutokea, mfano pale ambapo ubongo wa watu wengi utahamia tumboni na na tumbo litakuwa kichwani, wakati huo tunaosema tunaangalia maisha yetu hatutakuwa salama na Vitz zetu katika foleni ama majumbani mwetu.
 
He! Azizi Musa hongera, bahati mbaya JF utani mwingi, tafadhali wenye hekima zenu endeleeni kuweka peupe muda si mrefu yatatimia kwa kuwa mnapanda mbegu njema!!! (ebu angalia katika andiko lako ..............taratibu taratibu ili kisiendelee kutokea 'positevely' ( sio 'negatively?') au kupunguza 'positivity'. Tuweke sawa ndugu.)
Nilikosea nikarekebisha, asante

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom