WilsonKaisary
JF-Expert Member
- Apr 4, 2017
- 392
- 946
Swali langu limetokana na awamu zote za serikali za Tanzania kwanzia Serikali ya awamu ya kwanza hadi ya sasa.
Serikali zetu zimeshindwa kuwekeza kwenye wananchi wake, hususa kwenye tasnia ya elimu (Aina ya elimu, mitahara ya elimu, mifumo ya elimu, miundo mbinu ya elimu).
Hali hii kupelekea kuzalisha nguvu kazi kubwa yenye kujua kusoma na kuandika, kuzalisha wasomi wasio weza katika ushindani wa ajira hata tu ule wa kikanda kama ule Afrika Mashariki.
Graduate wa Kitanzania huwezi mfananisha na graduate wa Kikenya, hata kwenye ushindani wa kiajiri wa Kitanzania wanaoweza kushindana na Wakenya ni asilimia ndogo sana.
Serikali ya awamu ya tano imelenga na kuelekeza nguvu kubwa kwenye miundo mbinu, huku ikiifanya elimu kuwa bure. Jambo hili lina faida na hasara pia.
Hasara ni kuwa tunazidi ididmiza elimu yetu, maana serikali yetu haina uchumi wa kutoa elimu bora bure. Sana sana itaweza kutoa bora elimu, sasa bora elimu katika Karne hi ya 21 haitakiwi. Pili, hasara nyingine ni serikali inazidi kujiingiza kwenye matumizi makubwa ya fedha za ki-serikali.
Faida ni kuwa serikali inajipatia Watanzania wa shule ya msingi na sekondari wanaojua kusoma na kuandika.
Sasa ni bora serikali ikazalisha Watanzania 1,000,000 ambao wapo competent na wamepata elimu bora kwenye tasnia mbali mbali kuliko kuzalisha Watanzania 40,000,000 wanaojua kusoma na kuandika?
Sera ya elimu haikufikiriwa kwa upana sana, ilikuwa ni sera ya kisiasa tokana na ugumu wa uchaguzi wa mwaka 2015.
Maendeleo ya taifa lolote duniani, ni Aina ya wananchi walio nchini. Yani kiufupi serikali ikishindwa kuandaa wananchi wake kwenye fikra na kielimu basi hilo taifa litapata matokeo ya kiuchumi tokana na aina ya wananchi ilio waandaa.
Serikali za Tanzania zinapaswa kuwekeza nguvu nyingi na fedha nyingi kwenye tasnia ya elimu, afya na ndio vingine vifuate.
Faida za standard gauge au Stigler's Gorge si pana Kama ambavyo zile zingepatikana baada ya uboreshaji wa elimu (Aina ya elimu, mitahara ya elimu, mifumo ya elimu, miundo mbinu ya elimu).
Taifa letu ujinga, ufukara, umaskini na afya ndio changamoto sana na ni kikwazo kwa taifa hili kushindwa fikia malengo ya uchumi wa kati.
Watanzania wakielimika, wanaweza jenga standard gauge, Stigler's Gorge, fly overs, air port na kuanzisha viwanda.
Watanzania wakielimika wanaweza kuunda mifumo Bora ya kiutawala ya ki-serikali, pia hata wakielimika wanaweza unda katiba Bora.
Ni kheri umpatie mtu fikra na akili za kutafuta mali au umpatie Mali?
Serikali zetu zimeshindwa kuwekeza kwenye wananchi wake, hususa kwenye tasnia ya elimu (Aina ya elimu, mitahara ya elimu, mifumo ya elimu, miundo mbinu ya elimu).
Hali hii kupelekea kuzalisha nguvu kazi kubwa yenye kujua kusoma na kuandika, kuzalisha wasomi wasio weza katika ushindani wa ajira hata tu ule wa kikanda kama ule Afrika Mashariki.
Graduate wa Kitanzania huwezi mfananisha na graduate wa Kikenya, hata kwenye ushindani wa kiajiri wa Kitanzania wanaoweza kushindana na Wakenya ni asilimia ndogo sana.
Serikali ya awamu ya tano imelenga na kuelekeza nguvu kubwa kwenye miundo mbinu, huku ikiifanya elimu kuwa bure. Jambo hili lina faida na hasara pia.
Hasara ni kuwa tunazidi ididmiza elimu yetu, maana serikali yetu haina uchumi wa kutoa elimu bora bure. Sana sana itaweza kutoa bora elimu, sasa bora elimu katika Karne hi ya 21 haitakiwi. Pili, hasara nyingine ni serikali inazidi kujiingiza kwenye matumizi makubwa ya fedha za ki-serikali.
Faida ni kuwa serikali inajipatia Watanzania wa shule ya msingi na sekondari wanaojua kusoma na kuandika.
Sasa ni bora serikali ikazalisha Watanzania 1,000,000 ambao wapo competent na wamepata elimu bora kwenye tasnia mbali mbali kuliko kuzalisha Watanzania 40,000,000 wanaojua kusoma na kuandika?
Sera ya elimu haikufikiriwa kwa upana sana, ilikuwa ni sera ya kisiasa tokana na ugumu wa uchaguzi wa mwaka 2015.
Maendeleo ya taifa lolote duniani, ni Aina ya wananchi walio nchini. Yani kiufupi serikali ikishindwa kuandaa wananchi wake kwenye fikra na kielimu basi hilo taifa litapata matokeo ya kiuchumi tokana na aina ya wananchi ilio waandaa.
Serikali za Tanzania zinapaswa kuwekeza nguvu nyingi na fedha nyingi kwenye tasnia ya elimu, afya na ndio vingine vifuate.
Faida za standard gauge au Stigler's Gorge si pana Kama ambavyo zile zingepatikana baada ya uboreshaji wa elimu (Aina ya elimu, mitahara ya elimu, mifumo ya elimu, miundo mbinu ya elimu).
Taifa letu ujinga, ufukara, umaskini na afya ndio changamoto sana na ni kikwazo kwa taifa hili kushindwa fikia malengo ya uchumi wa kati.
Watanzania wakielimika, wanaweza jenga standard gauge, Stigler's Gorge, fly overs, air port na kuanzisha viwanda.
Watanzania wakielimika wanaweza kuunda mifumo Bora ya kiutawala ya ki-serikali, pia hata wakielimika wanaweza unda katiba Bora.
Ni kheri umpatie mtu fikra na akili za kutafuta mali au umpatie Mali?