KARLO MWILAPWA
JF-Expert Member
- Apr 10, 2019
- 2,590
- 4,600
Utaratibu, mila, desturi na utamaduni wa wanaCCM na watanzania kukosoa serikali na CCM ni jambo si la kukoma wala kuacha. Katika moja ya mikutano yake, Katibu Mkuu wa CCM amewaasa wanachama wa chama hicho kikongwe Afrika kuwa huru kuikosoa serikali na CCM kwa sababu ni utamaduni uliopo na yeye kama katibu mkuu hana’ mandate’ ya kuutoa utaratibu huo wala chama hakina nia hiyo.
CCM kinajiimarisha kwa kadiri kinavokoselewa na kikiimarika maana yake kitakuwa ni bora Zaidi katika kuisimamia serikali yake. Kutokana na kauli hii, naweza kusema CCM ya sasa ambayo ni imara katika kuisimamia serikali ni zao la kukubali kukosolewa na kufanyia kazi kasoro hizo. Katibu mkuu wa CCM anaposema kukosoa ni utamaduni na desturi ya CCM ana maana ya kwamba CCM imejengwa katika msingi huo na kila mwanaCCM kuanzia kwa mwenyekiti wa CCM taifa anafuata utaratibu huo.
Mengine yanayosemwa nje kwenye vibaraza na vijiwe kuwa CCM ya sasa haikosolewi ni ya kuachana nayo kwa sababu si utamaduni na utaratibu wa CCM na mwenye jukumu la kutukumbusha utaratibu huo ni Katibu mkuu wetu wa CCM na kasema kuwa utaratibu huo ni mzuri, uendelee kufuatwa. Nikiri kusema KM wa CCM na Mwenyekiti wake ni moja ya zao huru la fikra kupitia kukosoa na kukosolewa.
Utaratibu, utamaduni, mila na desturi hii ya CCM kukosoa, kukosolewa na kukosoana ni jambo muhimu katika ukuaji wa demokrasia nchini. Kwa maana hii, nikiri kusema kuwa CCM kwa Tanzania ndicho chama kinachoitafsiri na kuiishi demokrasia kwa vitendo na hakina mpinzani katika hilo. Wale wanaohoji demokrasia ya CCM, wanalijua hili? Pengine hawalijui na wanahitaji kufafanuliwa ili walijue.
Huwezi kujenga taasisi imara na yenye demokrasia kubwa kama CCM ukiwaziba midomo wasikosoe hivyo CCM imetokana na kukosoa, kukosolewa na kukosoana. Demokrasia iliyopo Tanzania ni zao la utaratibu, utamaduni, mila na desturi za CCM katika kukosoa.
CCM ingekuwa hahitaji kukosolewa, ninaamini leo bajeti ya wizara ya mambo ya ndani ingekuwa kubwa kuliko bajeti ya wizara ya ujenzi kwa maana kwamba bajeti ya wizara ya wizara ya mambo ya ndani ingeongezeka ili kujenga magereza mengi kwa ajili ya wakosoaji lakini si hivyo, wizara ya ujenzi ndio kubwa kwa sababu ukosoaji unajenga uchumi.
Kutokana na utamaduni huu wa kukosoa unavyoishi ndani ya CCM na kufanya CCM kuwa ni chama kinachoitafsiri na kuiishi demokrasia kwa vitendo na si mdomoni, upinzani una mengi ya kujifunza kutoka CCM. Upinzani umeonesha ombwe kubwa kwa mtu mwenye fikra mbadala
Hata wapinzani wenyewe wanakuwa huru Zaidi kuikosoa CCM kuliko vyama vyao kwa sababu utaratibu, utamaduni, mila na desturi za kukosoa ndani ya upinzani haujawa wazi kuliko ule wa CCM. CCM inachukulia kukosoa ni fikra mbadala lakini wenzetu wanaamini kukosoa ni usaliti.
CCM kinajiimarisha kwa kadiri kinavokoselewa na kikiimarika maana yake kitakuwa ni bora Zaidi katika kuisimamia serikali yake. Kutokana na kauli hii, naweza kusema CCM ya sasa ambayo ni imara katika kuisimamia serikali ni zao la kukubali kukosolewa na kufanyia kazi kasoro hizo. Katibu mkuu wa CCM anaposema kukosoa ni utamaduni na desturi ya CCM ana maana ya kwamba CCM imejengwa katika msingi huo na kila mwanaCCM kuanzia kwa mwenyekiti wa CCM taifa anafuata utaratibu huo.
Mengine yanayosemwa nje kwenye vibaraza na vijiwe kuwa CCM ya sasa haikosolewi ni ya kuachana nayo kwa sababu si utamaduni na utaratibu wa CCM na mwenye jukumu la kutukumbusha utaratibu huo ni Katibu mkuu wetu wa CCM na kasema kuwa utaratibu huo ni mzuri, uendelee kufuatwa. Nikiri kusema KM wa CCM na Mwenyekiti wake ni moja ya zao huru la fikra kupitia kukosoa na kukosolewa.
Utaratibu, utamaduni, mila na desturi hii ya CCM kukosoa, kukosolewa na kukosoana ni jambo muhimu katika ukuaji wa demokrasia nchini. Kwa maana hii, nikiri kusema kuwa CCM kwa Tanzania ndicho chama kinachoitafsiri na kuiishi demokrasia kwa vitendo na hakina mpinzani katika hilo. Wale wanaohoji demokrasia ya CCM, wanalijua hili? Pengine hawalijui na wanahitaji kufafanuliwa ili walijue.
Huwezi kujenga taasisi imara na yenye demokrasia kubwa kama CCM ukiwaziba midomo wasikosoe hivyo CCM imetokana na kukosoa, kukosolewa na kukosoana. Demokrasia iliyopo Tanzania ni zao la utaratibu, utamaduni, mila na desturi za CCM katika kukosoa.
CCM ingekuwa hahitaji kukosolewa, ninaamini leo bajeti ya wizara ya mambo ya ndani ingekuwa kubwa kuliko bajeti ya wizara ya ujenzi kwa maana kwamba bajeti ya wizara ya wizara ya mambo ya ndani ingeongezeka ili kujenga magereza mengi kwa ajili ya wakosoaji lakini si hivyo, wizara ya ujenzi ndio kubwa kwa sababu ukosoaji unajenga uchumi.
Kutokana na utamaduni huu wa kukosoa unavyoishi ndani ya CCM na kufanya CCM kuwa ni chama kinachoitafsiri na kuiishi demokrasia kwa vitendo na si mdomoni, upinzani una mengi ya kujifunza kutoka CCM. Upinzani umeonesha ombwe kubwa kwa mtu mwenye fikra mbadala
Hata wapinzani wenyewe wanakuwa huru Zaidi kuikosoa CCM kuliko vyama vyao kwa sababu utaratibu, utamaduni, mila na desturi za kukosoa ndani ya upinzani haujawa wazi kuliko ule wa CCM. CCM inachukulia kukosoa ni fikra mbadala lakini wenzetu wanaamini kukosoa ni usaliti.