Katika kuadhimisha siku ya Wanawake Duniani tukumbuke na haya

Bunchari

JF-Expert Member
Aug 31, 2017
489
531
MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI 2018


Na Anthony Daniel
Tukiwa tunasheherekea siku ya wanawake duniani tusiigeuze ikawa siku ya starehe kama ilivyo sikukuu zingine bali tupaze sauti zetu zisikike kila sehemu kuna wanawake wananyanyasika ndani ya ndoa, katika familia zao, kazini kwao, mitaani hivyo ifike mahali tuseme IMETOSHA na mwanamke apate uhuru wake.
Mfumo dume unawakandamiza wanawake hivyo tupige marufuku, tusiishie mijini kupiga kelele, matukio ya ajabu yapo vijijini hivyo sauti zetu ziwafikie huko ndani ndani na kwa pamoja tukaipate Tanzania tuitakayo isiyokuwa na ukandamizaji na unyanyasaji wa aina yoyote ile ya mwanamke.
Naungana na wanaharakati wote kila kona kutetea haki za wanawake wote.

*Happy women's day all*
 
Back
Top Bottom