Katika hili, wanasheria tusaidieni kutafsiri Katiba na Sheria

Ss Jr

JF-Expert Member
Jan 15, 2018
577
450
Wadau nachukua nafasi hii kuwatakia heri ya Pasaka.
Kama mnavyojua jumatano iliyopita tarehe 31/03/2021 wakati wa kumwapisha makamu wa Rais, mh Rais alitangaza baraza jipya la mawaziri, lakini mimi sina uhakika kama alikuwa sahihi.

Hoja yangu ni kwamba je ni halali kutangaza baraza jipya la mawaziri bila kuteua kwanza waziri mkuu?
Na je waziri mkuu anakuwaje halali wakati alikula kiapo kwa Rais tofauti na huyu wa sasa?
Na ni kwa nini mawaziri anaowaongoza ni mawaziri walioapishwa na Rais tofauti na aliyemwapisha?

Mbona yeye kama Rais alikula kiapo kwanza kabla ya kuwa Rais halafu awe na waziri mkuu ambaye hajala kiapo mbele yake?
Tafadhari wajuvi wa mambo tusaidieni tafsiri halali ya kisheria na kikatiba. Ni hayo tu wadau wa jf.
 
Ilitafsiriwa kuwa halazimiki kuvunja baraza la mawaziri(kumtoa Waziri Mkuu) ila anaweza kufanya hivyo.
Ilitafsiriwa na nani na nikifungu kipi cha Katiba kinachosema kwa kushika nafasi hiyo ya PM siyo lazima kuapishwa?
 
TLS walishatoa ufafanuzi wakupinga wakapinga tafta huo uzi usome hakuna majibu mengine zaidi ya hayo
 
TLS walishatoa ufafanuzi wakupinga wakapinga tafta huo uzi usome hakuna majibu mengine zaidi ya hayo
Rudia kusoma huo ufafanuzi wa kwanza kabisa wameeleza kuteua waziri mkuu pamoja na baraza kwa ujumla ndani ya siku 14
 
soma katiba yenyewe wewe mwenyewe kabla ya kusikiliza hii miluzi mingine, kisha leta tafsiri ya ulivyoelewa!

Baada ya hapo sasa chambua hiyo miluzi mingine kwa kuzingatia ulivyoelewa

Baada ya hapo sasa Weka/Tengeneza picha ya AKINA NANI NA WENYE NIA GANI WAPO NYUMA YA HIYO MILUZI

(the easiest way of interpreting the Law)
 
Ngoja nitie kambi naweza kupata kitu hapa ...

Civics ilinipigaa chenga
 
CCM akili zao kama makambare na wananchi akili zetu kama Mbuzibee 🐐. Tanzania haifuati Katiba wala sheria kama huamini anza na uchaguzi ulivyokwenda mpaka kuishia. Jiulize kuna Katiba au sheria iliofuatwa?


Mbuzibee 🐐
 
Unamaanisha kutoka tarehe 19/03/2021 hazijatimia siku 14 ambazo kwa mjibu wa katiba Rais anatakiwa kuunda baraza jipya la mawaziri?
Rais Samia hajaunda serikali mpya anamalizia awamu ya mtangulizi wake kwa mujibu wa katiba
 
Unataka kusema kwamba kiapo chake ni kwa niaba ya Rais siyo Rais kamili?
Ikiwa kiapo kina hama Nani atastahimili kwenye serikali hii? Wote walio apishwa na Mwendazake watakuwa wametenguliwa kupisha uteuzi mpya. TLS walijichanganya na hawakujibu swali lolote siku Ile zaidi ya kukimbia
 
Katiba ya Tanzania ina Ombwe,na ukijumuisha na Wananchi kutoijua basis watawala wanafanya wanavyo taka-by the way haya yote ni kwa sababu Watanzania ni malimbukeni.
 
Na ndiyo maana katiba mpya inahitajika, lakini kwa wasiojitambua wanabeza upatikanaji wa katiba mpya
 
Back
Top Bottom