Synthesizer
JF-Expert Member
- Feb 15, 2010
- 11,023
- 18,563
Hili tatizo la mpaka kati ya Tanzania na Malawi hadi leo halijatatuliwa. Suala ni kwamba, kuna dalili za mafuta ndani ya Ziwa Nyasa, ambalo Malawi wanaliita Ziwa Malawi. Na suala la uwezekano wa mafuta lilizua upendezi mpya wa ziwa kwa Malawi wakasema kwamba mpaka kati ya Tanzania na Malawi siku zote umekuwa mwisho wa ziwa Nyasa kwa upande wa Tanzania, yaani ziwa lote liko ndani ya Malawi.
Tanzania wakasema hakuna kitu kama hicho. Siku zote mpaka ni mstari wa katikati ya ziwa ili kutenganisha Malawi na Tanzania, na hiki ndicho kinachokubalika kimataifa kunapokuwa na maji makubwa kati ya nchi mbili. Malawi hawakukubaliana na msimamo wa Tanzania, na wakadai wataweka watafiti wa mafuta ndani ya ziwa lao (Nyasa). Tanzania ikawaambia Malawi watafiti hao wakiingia upande wa Tanzania watakiona cha mtema kuni.
Marais wa Malawi waliopita walikuwa na msimamo mkali kuhusu ziwa Nyasa wakidai ziwa lote liko Malawi na hata walitumia jambo hili katika kampeni zao. Sijui msimamo wa huyu raisi mpya wa Malawi ukoje. Mgogoro huu ulikuwa usuluhishwe na SADC na Thabo Mbeki na Joachim Chisano walipewa jukumu la kuutatua. Sijui ripoti yao iliishia wapi, au kama waliweza kumaliza kazi yao.
Huko nyuma niliwahi kupendekeza humu JF kwamba jambo kubwa linalofanya kuwe na mgogoro wa mpaka ni mafuta ndani ya ziwa Nyasa. Nikapendekeza kwamba, kwa nini Tanzania wasikubaliane na Malawi kwamba mafuta yote yatakayopatikana ndani ya ziwa Nyasa uwe mradi wa pamoja kati ya Tanzania kwa kugawana 50:50? Sijui kama kuna walionisikiliza.
Sasa basi, kwa kuwa tuna Rais mpya Malawi, ambae ameonyesha ukaribu na Magufuli, ushauri wangu kwa Magufuli ni kutumia fursa hii kumaliza hili suala la mpaka wetu na Malawi. Nachela tusipolimaliza sasa huko mbele linaweza kuja kuzaa vita kati ya Tanzania na Malawi.
Mambo ya vita yamepitwa na wakati. Wanajeshi siku hizi hawapigani wanajenga madaraja na kujenga nyumba nk. Rais Magufuli hebu ongea na Rais wa Malawi tumalize jambo hili na kuanza kutumia hayo mafuta kujenga SGR, Stiegler Gorge, flyovers, lami hadi vijijini, nk, tuifanye Tanzania kama Ulaya!
Angalia pia;
Tanzania wakasema hakuna kitu kama hicho. Siku zote mpaka ni mstari wa katikati ya ziwa ili kutenganisha Malawi na Tanzania, na hiki ndicho kinachokubalika kimataifa kunapokuwa na maji makubwa kati ya nchi mbili. Malawi hawakukubaliana na msimamo wa Tanzania, na wakadai wataweka watafiti wa mafuta ndani ya ziwa lao (Nyasa). Tanzania ikawaambia Malawi watafiti hao wakiingia upande wa Tanzania watakiona cha mtema kuni.
Marais wa Malawi waliopita walikuwa na msimamo mkali kuhusu ziwa Nyasa wakidai ziwa lote liko Malawi na hata walitumia jambo hili katika kampeni zao. Sijui msimamo wa huyu raisi mpya wa Malawi ukoje. Mgogoro huu ulikuwa usuluhishwe na SADC na Thabo Mbeki na Joachim Chisano walipewa jukumu la kuutatua. Sijui ripoti yao iliishia wapi, au kama waliweza kumaliza kazi yao.
Huko nyuma niliwahi kupendekeza humu JF kwamba jambo kubwa linalofanya kuwe na mgogoro wa mpaka ni mafuta ndani ya ziwa Nyasa. Nikapendekeza kwamba, kwa nini Tanzania wasikubaliane na Malawi kwamba mafuta yote yatakayopatikana ndani ya ziwa Nyasa uwe mradi wa pamoja kati ya Tanzania kwa kugawana 50:50? Sijui kama kuna walionisikiliza.
Sasa basi, kwa kuwa tuna Rais mpya Malawi, ambae ameonyesha ukaribu na Magufuli, ushauri wangu kwa Magufuli ni kutumia fursa hii kumaliza hili suala la mpaka wetu na Malawi. Nachela tusipolimaliza sasa huko mbele linaweza kuja kuzaa vita kati ya Tanzania na Malawi.
Mambo ya vita yamepitwa na wakati. Wanajeshi siku hizi hawapigani wanajenga madaraja na kujenga nyumba nk. Rais Magufuli hebu ongea na Rais wa Malawi tumalize jambo hili na kuanza kutumia hayo mafuta kujenga SGR, Stiegler Gorge, flyovers, lami hadi vijijini, nk, tuifanye Tanzania kama Ulaya!
Angalia pia;