aisee hata mimi sijui, ila ni mtanzania, unataka umlinganishe ubongo wake na kabila lake nini? ila jamaa alikuwa anafanania sana na chama chake.
Mrema vyama anavyokuwa mwenyekiti anaviendesha kama kiosk chake cha vinywaji baridi. Ina maana Mbowe anaweza kuhamka tu na kumfuza Dr Slaa?
Please vyama vipewe grade sasa this is too LOW au alikuwa amelala?
Mi nilikuwa najiuliza kama wajumbe wa mkutano ule hawakuwa wamevutishwa bangi au kupewa "Takrima" na Mzee wa Kiraracha?
Kama demokrasia ndiyo staili ile ya Mrema, basi tumekwisha!
Mi namshauri Tao aende Mahakamani maana uonevu unaonekana waziwazi hata kwa kipofu. naamini haki itatendeka ingawa kwa Mahakama zetu mwenye fedha ndiye mwenye haki, ikiwa hilo litazingatiwa Tao atakuwa hana chake.
Hivi Mrema alizaliwa awe Mwenyekiti wa vyama tu na nafasi nyingine hazimtoshi? Wakati umefika sasa kwa wanachama wakereketwa wa TLP kuilinda hadhi ya chama chao na kumfukuza adui wa demokrasia huyu Mrema ambaye ni kama mcheza michezo ya comedy. CCM katika hili wanachekea tumboni maana kibaraka wao Mrema anatimiza wanachotaka kwa uaminifu mkubwa, sijui wananchi wa huko walikomchagua nduli huyu wanajisikiaje wanapomwona akiipondaponda demokrasia.
magamba waige mfano huu wa kumvua gamba mtu live live! hi! hi! hi! hi! hi!..,mapacha 3 wavuliwe uanachama kwa style ile ya TLP, looh! haponi mtu siku hiyo.
Inafaa sasa Mtikufu Lyatonga atangaze tu TLP ni mali yake binafsi,wanapigania demokrasia lakini hao wenyewe ni zaidi ya madikteta
Wanakula kodio zetu bure tu, naamini na hiki chama kila kula mgawo kutoka hazina kila mwezi, cha kusikitisha huu mgawo ni kodi za wafanyakazi maskini ambao kila mwezi wanakatwa na watawala
Ni Hamad Tao
hii weekend bwana....kwa hiyo mkuu unataka kwenye fomu za maadili ya umma akitangaza mali zake,asipoweka TLP awe amedanganya mkuu?
Katibu wa TLP taifa ametimuliwa kazi leo na Mwenyekiti wa chama hicho mh. Mrema.
Source: ITV habari