Imeandikwa tarehe 05 Desemba 2012 | Mwandishi wa HabariLeo
KATIBU wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) James Mpalaza wa Wilaya ya Mbeya Vijijini amenaswa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) akipokea rushwa ya Sh 73,000.
Taarifa zilizolifikia gazeti hili jana zinasema kuwa, Mpalaza ambaye pia ni Katibu wa Baraza la Ardhi katika Kata ya Nsalala alidai rushwa kutoka kwa Mwenyekiti wa CCM wa Kata hiyo, Ahadi Ndile kwa lengo la kumpatia hukumu iliyotolewa na Baraza hilo.
Ndile alikuwa kwenye mzozo wa mpaka na Diwani wa Kata ya Ikukwa Viti Maalumu, Monica Degua (CCM) na Baraza hilo lililopo Mbeya vijijini lilimpa ushindi Degua. Ndile alithibitisha kutokea tukio hilo akisema;
"Sikuridhishwa na hukumu ya Baraza, nikaamua kuomba nakala ya hukumu ili nisonge mbele, mwanzo waliniambia nipeleke Sh 10,000 ili niandikiwe taarifa nzuri sana.
"Nilipokwenda na fedha hizo ambazo walidai ni gharama za Baraza, walidai hazitoshi na nitapewa endapo tu nitapeleka Sh 73,000. Sikuona sababu ya kupeleka fedha hizo ndipo nilipowasiliana na Takukuru ambao leo (jana) wamefanya kazi yao," alisema.
Kwa upande wake, Kamanda wa Takukuru mkoani Mbeya, Daniel Mtuka alikiri kumshikilia Mpalaza kwa tuhuma hizo kwa pamoja na Mwenyekiti wa Baraza hilo, Asia Haruna.
Akizungumzia tukio hilo alisema Novemba 26 mwaka huu ofisi za Takukuru mkoani hapo zilipata taarifa kutoka kwa mlalamikaji aliyefahamika kwa jina la Ahadi Ndile ambaye alikuwa na kesi ya madai namba 26, 2012 ya kugombea mpaka yeye na jirani yake Monica Degula.
Alisema kutokana na mgogoro huo wa mpaka, walipeleka kesi katika Baraza hilo ambapo baada ya uamuzi, Ndile alishindwa na Monica na hakuridhika na uamuzi huo na hivyo kuamua kuomba kupatiwa mwenendo wa shauri pamoja na hukumu.
Mtuka alisema wakati akiomba kupatiwa hukumu hiyo ndipo alipotakiwa kuhonga Sh 73,000 kwa Mpalaza ambaye ni Katibu wa Baraza hilo ikiwa ni pamoja na Sh 10,000 kwa ajili ya gharama ya kesi.
Hata hivyo Mtuka alisema migogoro ya ardhi imekuwa kero katika eneo hilo na kwamba Takukuru ina majalada mengi yatokanayo na malalamiko kutoka kwa wananchi wakitakiwa kutoa rushwa na kudhulumiwa haki zao.
Alisema bado wanahojiana na Ndile pamoja na Mwenyekiti lakini aliyepokea fedha hizo ni Mpalaza.
KATIBU wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) James Mpalaza wa Wilaya ya Mbeya Vijijini amenaswa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) akipokea rushwa ya Sh 73,000.
Taarifa zilizolifikia gazeti hili jana zinasema kuwa, Mpalaza ambaye pia ni Katibu wa Baraza la Ardhi katika Kata ya Nsalala alidai rushwa kutoka kwa Mwenyekiti wa CCM wa Kata hiyo, Ahadi Ndile kwa lengo la kumpatia hukumu iliyotolewa na Baraza hilo.
Ndile alikuwa kwenye mzozo wa mpaka na Diwani wa Kata ya Ikukwa Viti Maalumu, Monica Degua (CCM) na Baraza hilo lililopo Mbeya vijijini lilimpa ushindi Degua. Ndile alithibitisha kutokea tukio hilo akisema;
"Sikuridhishwa na hukumu ya Baraza, nikaamua kuomba nakala ya hukumu ili nisonge mbele, mwanzo waliniambia nipeleke Sh 10,000 ili niandikiwe taarifa nzuri sana.
"Nilipokwenda na fedha hizo ambazo walidai ni gharama za Baraza, walidai hazitoshi na nitapewa endapo tu nitapeleka Sh 73,000. Sikuona sababu ya kupeleka fedha hizo ndipo nilipowasiliana na Takukuru ambao leo (jana) wamefanya kazi yao," alisema.
Kwa upande wake, Kamanda wa Takukuru mkoani Mbeya, Daniel Mtuka alikiri kumshikilia Mpalaza kwa tuhuma hizo kwa pamoja na Mwenyekiti wa Baraza hilo, Asia Haruna.
Akizungumzia tukio hilo alisema Novemba 26 mwaka huu ofisi za Takukuru mkoani hapo zilipata taarifa kutoka kwa mlalamikaji aliyefahamika kwa jina la Ahadi Ndile ambaye alikuwa na kesi ya madai namba 26, 2012 ya kugombea mpaka yeye na jirani yake Monica Degula.
Alisema kutokana na mgogoro huo wa mpaka, walipeleka kesi katika Baraza hilo ambapo baada ya uamuzi, Ndile alishindwa na Monica na hakuridhika na uamuzi huo na hivyo kuamua kuomba kupatiwa mwenendo wa shauri pamoja na hukumu.
Mtuka alisema wakati akiomba kupatiwa hukumu hiyo ndipo alipotakiwa kuhonga Sh 73,000 kwa Mpalaza ambaye ni Katibu wa Baraza hilo ikiwa ni pamoja na Sh 10,000 kwa ajili ya gharama ya kesi.
Hata hivyo Mtuka alisema migogoro ya ardhi imekuwa kero katika eneo hilo na kwamba Takukuru ina majalada mengi yatokanayo na malalamiko kutoka kwa wananchi wakitakiwa kutoa rushwa na kudhulumiwa haki zao.
Alisema bado wanahojiana na Ndile pamoja na Mwenyekiti lakini aliyepokea fedha hizo ni Mpalaza.