Mwalimu Makini
Member
- Dec 5, 2009
- 65
- 23
Leo kulifanyika Kongamano kubwa lililoitishwa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjro Mhe. Meja Jenerali Mstaafu Said Kalembo. Kongamano hilo lililofanyika katika ukumbi wa YMCA lilihudhuriwa na Wakuu wote wa Wilaya za Mkoa wa Kilimanjaro, Viongozi na watumishi wote wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Wakurugenzi wa Halmashauri zote, madiwani wote walimu kadhaa wa shule za msingi na za sekondari mjini Moshi, wanafunzi kadha wa shule za msingi na za sekondari, viongozi wa vyama vya siasa pamoja na viongozi wa madhehebu ya dini.
Baada ya mada kutolewa uwanja uliwekwa wazi kwa ajili ya waalikwa kuchangia katika mada kuu " MIAKA 50 YA UHURU NA CHANGAMOTO ZAKE" Katika hali ya kutatanisha Katibu wa CHADEMA mkoa wa Kilimanjaro Ndg. Basil Lema alipata nafasi ya kuchangia akiwa mtu wa tano. Baada tu ya kujitambulisha mic ilizimika ikabidi aende hadi mbele kabisa akachukua mic ya RC. Ilimchukua pungufu ya dk 1 kuanzisha hoja yake kuhusu uhuru na maendeleo ndipo ghafla RC Kalembo akasimama akasema hajatoa nafasi za watu kuhutubia. Mshereheshaji alichukua mic kutoka mkononi kwa Lema na kuita mchangiaji mwingine.
Lema alirudi kwenye kiti chake kwa aibu na kuonekana wazi kuwa amechemka na aibu zimemjaa usoni. Hii ni matokeo ya kutaka kuchafua hali ya hewa kwenye ukumbi kwa vijembe vya siasa. Inashangaza kuwa kuna watu hawaoni maendeleo ambayo Tanzania imepiga kwa miaka hii 50 ya uhuru.
Baada ya mada kutolewa uwanja uliwekwa wazi kwa ajili ya waalikwa kuchangia katika mada kuu " MIAKA 50 YA UHURU NA CHANGAMOTO ZAKE" Katika hali ya kutatanisha Katibu wa CHADEMA mkoa wa Kilimanjaro Ndg. Basil Lema alipata nafasi ya kuchangia akiwa mtu wa tano. Baada tu ya kujitambulisha mic ilizimika ikabidi aende hadi mbele kabisa akachukua mic ya RC. Ilimchukua pungufu ya dk 1 kuanzisha hoja yake kuhusu uhuru na maendeleo ndipo ghafla RC Kalembo akasimama akasema hajatoa nafasi za watu kuhutubia. Mshereheshaji alichukua mic kutoka mkononi kwa Lema na kuita mchangiaji mwingine.
Lema alirudi kwenye kiti chake kwa aibu na kuonekana wazi kuwa amechemka na aibu zimemjaa usoni. Hii ni matokeo ya kutaka kuchafua hali ya hewa kwenye ukumbi kwa vijembe vya siasa. Inashangaza kuwa kuna watu hawaoni maendeleo ambayo Tanzania imepiga kwa miaka hii 50 ya uhuru.