Mungi
JF Gold Member
- Sep 23, 2010
- 16,975
- 9,566
POLISI mkoani Rukwa inamshikilia Katibu Mwenezi wa CCM wa Mkoa, Patrick Maufi (48), kwa tuhuma za kumwua mkewe, Tuli Mwakibinga (38) kwa kipigo kutokana na kilichoelezwa
kuwa ni wivu wa mapenzi.
Taarifa za Polisi Mkoa wa Rukwa, zilisema jana kuwa Tuli ambaye ni Mhudumu wa Afya
katika hospitali ya mkoa mjini hapa alifariki dunia jana asubuhi katika chumba cha
wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu (ICU), hospitalini hapo.
Habari zilidai kuwa Tuli alifikishwa hospitalini hapo kutoka Hospitali Teule ya Manispaa ya Dk. Atman, kwa ajili ya kupata matibabu baada ya kupigwa na kuumizwa vibaya sehemu mbalimbali hata kichwani.
Inadaiwa kuwa kabla ya kupigwa, juzi saa nne usiku, Maufi alipata taarifa kwamba mkewe yuko baa mjini hapa na alimfuata na kumpeleka nyumbani eneo la Kristu Mfalme.
Kwa mujibu wa madai hayo, wakiwa nyumbani, walianza mzozo na alimtuhumu kuwa na uhusiano na mwanamume mwingine, wakapigana.
Majirani walioshuhudia ambao hawakuwa tayari kutajwa gazetini, walieleza kuwa walimchukua mwanamke huyo na kumkimbiza Hospitali ya Dk. Atman ili apate matibabu, lakini hali ilikuwa mbaya zaidi.
Ilipofika saa 2.30 jana asubuhi Tuli alipelekwa hospitali ya rufaa mjini hapa, akiwa amepoteza fahamu na kulazwa ICU lakini alifariki dunia muda mfupi baadaye.
Mganga Mkuu wa Mkoa, Dk. Sadun Kabuma, alithibitisha kutokea kwa kifo hicho na kueleza kuwa baada ya uchunguzi wa kitabibu, ilibainika kuwa alivuja damu nyingi kwenye ubongo na shingo ilivunjika.
Inawezekana kuwa muuaji alikuwa akibamiza kichwa cha marehemu ukutani kwa nguvu
hali iliyosababisha kuvuja kwa damu nyingi kwenye ubongo.
Hata hivi ninavyozungumza nawe, baada ya saa kadhaa kupita, mwili bado unavuja damu puani, alisema Dk. Kabuma.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Rukwa, Isuto Mantage, alithibitisha kukamatwa kwa Maufi na kwamba atafikishwa mahakamani baada ya uchunguzi wa awali kukamilika.
My take: huyu angelikuwa na katibu wa chadema lazima angeshamalizwa na polisi wa ccm. kwakuwa ni wa magamba basi mtasikia mara aliua bila kukusudia, au marehemu alianguka akafa, hata postmoterm itachakachuliwa.
kuwa ni wivu wa mapenzi.
Taarifa za Polisi Mkoa wa Rukwa, zilisema jana kuwa Tuli ambaye ni Mhudumu wa Afya
katika hospitali ya mkoa mjini hapa alifariki dunia jana asubuhi katika chumba cha
wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu (ICU), hospitalini hapo.
Habari zilidai kuwa Tuli alifikishwa hospitalini hapo kutoka Hospitali Teule ya Manispaa ya Dk. Atman, kwa ajili ya kupata matibabu baada ya kupigwa na kuumizwa vibaya sehemu mbalimbali hata kichwani.
Inadaiwa kuwa kabla ya kupigwa, juzi saa nne usiku, Maufi alipata taarifa kwamba mkewe yuko baa mjini hapa na alimfuata na kumpeleka nyumbani eneo la Kristu Mfalme.
Kwa mujibu wa madai hayo, wakiwa nyumbani, walianza mzozo na alimtuhumu kuwa na uhusiano na mwanamume mwingine, wakapigana.
Majirani walioshuhudia ambao hawakuwa tayari kutajwa gazetini, walieleza kuwa walimchukua mwanamke huyo na kumkimbiza Hospitali ya Dk. Atman ili apate matibabu, lakini hali ilikuwa mbaya zaidi.
Ilipofika saa 2.30 jana asubuhi Tuli alipelekwa hospitali ya rufaa mjini hapa, akiwa amepoteza fahamu na kulazwa ICU lakini alifariki dunia muda mfupi baadaye.
Mganga Mkuu wa Mkoa, Dk. Sadun Kabuma, alithibitisha kutokea kwa kifo hicho na kueleza kuwa baada ya uchunguzi wa kitabibu, ilibainika kuwa alivuja damu nyingi kwenye ubongo na shingo ilivunjika.
Inawezekana kuwa muuaji alikuwa akibamiza kichwa cha marehemu ukutani kwa nguvu
hali iliyosababisha kuvuja kwa damu nyingi kwenye ubongo.
Hata hivi ninavyozungumza nawe, baada ya saa kadhaa kupita, mwili bado unavuja damu puani, alisema Dk. Kabuma.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Rukwa, Isuto Mantage, alithibitisha kukamatwa kwa Maufi na kwamba atafikishwa mahakamani baada ya uchunguzi wa awali kukamilika.
My take: huyu angelikuwa na katibu wa chadema lazima angeshamalizwa na polisi wa ccm. kwakuwa ni wa magamba basi mtasikia mara aliua bila kukusudia, au marehemu alianguka akafa, hata postmoterm itachakachuliwa.