Katibu wa CCM Mkoa wa Morogoro, Shaka Hamdu Shaka asimamishwa kwa tuhuma za rushwa

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,221
217,186
HABARI_ Rais John Magufuli amesema, Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimemsimamisha ka ( 345 X 640 ).jpg


Anatuhumiwa kushiriki rushwa wakati wa mchakato wa kumpata Meya wa Manispaa hiyo.

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa CCM Mh Magufuli akiwa ziarani Mkoani humo.

====



Katibu CCM asimamishwa kwa rushwa, Magufuli asema…


KATIBU wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Morogoro, Shaka Hamidu Shaka, amesimamishwa kazi na chama hicho, kupisha uchunguzi wa tuhuma za kula rushwa kutoka kwa madiwani wakati wa mchakato wa upatikanaji wa meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro. Anaripoti Mwandishi Wetu, Morogoro

Taarifa hiyo imetolewa leo Alhamisi tarehe 11 Februari 2021, na Rais wa Tanzania, John Magufuli, wakati anazindua Soko Kuu la Mkoa wa Morogoro.

Licha ya kutomtaja jina, Rais Magufuli ambaye ni Mwenyekiti huyo wa CCM Taifa, amesema, Shaka atajadiliwa kwa tuhuma za kula rushwa za madiwani.

“Na bahati mbaya, hata utafutaji wa meya hapa ulijaa rushwa ndio maana katibu wa CCM hapa tumemsimisha kazi, atajadiliwa kwa sababu alikula rushwa kwa madiwani,” amesema Rais Magufuli.

Rais Magufuli alitoa taarifa hiyo wakati anazungumzia upatikanaji wa meya wa manispaa hayo, Pascal Kihanga, ambapo amesema hakustahili kuwa Meya wa Manispaa ya Morogoro.
Rais John Magufuli

Kiongozi huyo wa CCM Taifa, amesema aliyestahili kuwa meya wa manispaa hiyo hamkurudisha, hivyo amemuagiza Kihanga kusimamia wananchi waliomchagua.

“Na wewe mstahiki meya nataka ubadilike, najua umeupata umeya wa bahati bahati hapa, mimi napenda kuzungumza ukweli. Nasema uongo ndugu zangu? Hukutakiwa kuwa meya, aliyetakiwa sikumrudisha kuwa meya,” amesema Rais Magufuli.

Madiwani wa Halmshauri ya Manispaa ya Morogoro, walifanya uchaguzi wa meya tarehe 23 Novemba 2020, ambapo majina mawili yalifungana kwa zaidi ya mara tatu, baada ya kura zao kufanana kila walipopigiwa.

Baada ya majina hayo kufungana, uchaguzi huo ulirudiwa tarehe 1 Disemba 2020, ambao pia walifungana kwa kupata kura 21 kila mmoja.

Madiwani waliofungana walikuwa ni Seifu Chomoja na Paschal Kihanga, ambapo majina yao yalipelekwa katika Kamati Kuu ya CCM Taifa, ambayo ilirlirudisha jina la Kihanga.


 
View attachment 1700064

Anatuhumiwa kushiriki rushwa wakati wa mchakato wa kumpata Meya wa Manispaa hiyo

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa CCM Mh Magufuli akiwa ziarani Mkoani humo
Ukifika Kule Kilimanjaro, ukumbuke pia kumtumbua Miriam Kaaya, Katibu wa CCM wilaya ya moshi vijiji na vunjo. Kila rushwa kwa wajumbe waliotia nia kugombea ubunge 2020
 
Back
Top Bottom