Amanikwenu
Senior Member
- Dec 1, 2009
- 187
- 0
Jana (12/11/2010) wakati akitangaza matokeo ya uchaguzi wa Spika, Katibu wa Bunge Dr. Thomas Kashililah alisema kuwa Anne Makinda alipata kura 265 kati ya kura 327 zilizopigwa. Aliutaja ushindi huu wa Anne Makinda kuwa ni asilimia 74.2 ya kura zote. Naona hapa Katibu wa Bunge aliteleza au alipigwa chenga kidogo na hesabu za asilimia. Kwa kura alizopata Anne Makinda ki-asilimia ni 81.04 na si asilimia 74.2 kama alivyoutangazia umma wa Watanzania na dunia. Vinginevyo atuambie kuwa kura alizopata mama Anne Makinda ni 242.5 na wala si 265. Mbaya zaidi vyombo vyetu vingi vya habari vimeendelea kutaja hizo asilimia 74.2 badala ya kugundua kwamba kuna kasoro katika kile alichokitangaza Katibu wa Bunge