Katibu wa Bunge na Hesabu za Asilimia

Amanikwenu

Senior Member
Dec 1, 2009
187
0
Jana (12/11/2010) wakati akitangaza matokeo ya uchaguzi wa Spika, Katibu wa Bunge Dr. Thomas Kashililah alisema kuwa Anne Makinda alipata kura 265 kati ya kura 327 zilizopigwa. Aliutaja ushindi huu wa Anne Makinda kuwa ni asilimia 74.2 ya kura zote. Naona hapa Katibu wa Bunge aliteleza au alipigwa chenga kidogo na hesabu za asilimia. Kwa kura alizopata Anne Makinda ki-asilimia ni 81.04 na si asilimia 74.2 kama alivyoutangazia umma wa Watanzania na dunia. Vinginevyo atuambie kuwa kura alizopata mama Anne Makinda ni 242.5 na wala si 265. Mbaya zaidi vyombo vyetu vingi vya habari vimeendelea kutaja hizo asilimia 74.2 badala ya kugundua kwamba kuna kasoro katika kile alichokitangaza Katibu wa Bunge
 
Jana (12/11/2010) wakati akitangaza matokeo ya uchaguzi wa Spika, Katibu wa Bunge Dr. Thomas Kashililah alisema kuwa Anne Makinda alipata kura 265 kati ya kura 327 zilizopigwa. Aliutaja ushindi huu wa Anne Makinda kuwa ni asilimia 74.2 ya kura zote. Naona hapa Katibu wa Bunge aliteleza au alipigwa chenga kidogo na hesabu za asilimia. Kwa kura alizopata Anne Makinda ki-asilimia ni 81.04 na si asilimia 74.2 kama alivyoutangazia umma wa Watanzania na dunia. Vinginevyo atuambie kuwa kura alizopata mama Anne Makinda ni 242.5 na wala si 265. Mbaya zaidi vyombo vyetu vingi vya habari vimeendelea kutaja hizo asilimia 74.2 badala kugundua kwamba kuna kasoro katika kile alichokitangaza Katibu wa Bunge
Amani kwako pia!
 
Jana (12/11/2010) wakati akitangaza matokeo ya uchaguzi wa Spika, Katibu wa Bunge Dr. Thomas Kashililah alisema kuwa Anne Makinda alipata kura 265 kati ya kura 327 zilizopigwa. Aliutaja ushindi huu wa Anne Makinda kuwa ni asilimia 74.2 ya kura zote. Naona hapa Katibu wa Bunge aliteleza au alipigwa chenga kidogo na hesabu za asilimia. Kwa kura alizopata Anne Makinda ki-asilimia ni 81.04 na si asilimia 74.2 kama alivyoutangazia umma wa Watanzania na dunia. Vinginevyo atuambie kuwa kura alizopata mama Anne Makinda ni 242.5 na wala si 265. Mbaya zaidi vyombo vyetu vingi vya habari vimeendelea kutaja hizo asilimia 74.2 badala kugundua kwamba kuna kasoro katika kile alichokitangaza Katibu wa Bunge

hii do bongo bwana kanyaga twende:bolt:
 
yaai ukizoea kuchakachua mpaka calculator unashindwa kuitumia kabisa..hayo ndo madhara ya kuchakachua
 
nili hoji kuhusu suala hili jana katika thread moja iliyokuwa ikitutangazia live uchaguzi wa speaker.

Huhitaji calculator kujua kuwa hesabu hazijakaa sawa kwa kutumia logic tu hata kama hesabu zinakupiga chenga. Ikiwa 53 ni 17% na 265 ni 74%, kura 9 ni 9% ya 327?

aibu ni kuwa hakuna mwandishi aliyehoji hili jana kutwa nzima wakati ni kitu kilicho dhahiri kabisa.
 
Jana (12/11/2010) wakati akitangaza matokeo ya uchaguzi wa Spika, Katibu wa Bunge Dr. Thomas Kashililah alisema kuwa Anne Makinda alipata kura 265 kati ya kura 327 zilizopigwa. Aliutaja ushindi huu wa Anne Makinda kuwa ni asilimia 74.2 ya kura zote. Naona hapa Katibu wa Bunge aliteleza au alipigwa chenga kidogo na hesabu za asilimia. Kwa kura alizopata Anne Makinda ki-asilimia ni 81.04 na si asilimia 74.2 kama alivyoutangazia umma wa Watanzania na dunia. Vinginevyo atuambie kuwa kura alizopata mama Anne Makinda ni 242.5 na wala si 265. Mbaya zaidi vyombo vyetu vingi vya habari vimeendelea kutaja hizo asilimia 74.2 badala ya kugundua kwamba kuna kasoro katika kile alichokitangaza Katibu wa Bunge

Kuna tofauti ya kura 22 ambazo ni za CUF, hii inawezekana CUF walimpigia Marando lakini wakaamua kuziondoa ili kuchonganisha upinzani
 
Kuna tofauti ya kura 22 ambazo ni za CUF, hii inawezekana CUF walimpigia Marando lakini wakaamua kuziondoa ili kuchonganisha upinzani

Kura zimetimia kwa mgawanyiko wa 265,53 na 9 na kufanya 327, asilimia ndo iligomba.

au unataka kusema asilimia ndo correct na kura ndo zimekosewa?
 
Jana (12/11/2010) wakati akitangaza matokeo ya uchaguzi wa Spika, Katibu wa Bunge Dr. Thomas Kashililah alisema kuwa Anne Makinda alipata kura 265 kati ya kura 327 zilizopigwa. Aliutaja ushindi huu wa Anne Makinda kuwa ni asilimia 74.2 ya kura zote. Naona hapa Katibu wa Bunge aliteleza au alipigwa chenga kidogo na hesabu za asilimia. Kwa kura alizopata Anne Makinda ki-asilimia ni 81.04 na si asilimia 74.2 kama alivyoutangazia umma wa Watanzania na dunia. Vinginevyo atuambie kuwa kura alizopata mama Anne Makinda ni 242.5 na wala si 265. Mbaya zaidi vyombo vyetu vingi vya habari vimeendelea kutaja hizo asilimia 74.2 badala ya kugundua kwamba kuna kasoro katika kile alichokitangaza Katibu wa Bunge

Watanzania hatuko makini na ndio maana tunaibiwa kirahisi.

Nimeshangazwa na magazeti yote kurudia asilimia ambayo ina makosa. Yaani vyombo vyetu ni kama kasuku, vinaimba tu kile walichoambiwa au ndio dunia ya copy and paste? Hata yule mwandishi wa Reuters naye kachemsha.

Na wale wabunge walioenda kusimamia kuhesabu kura, walikuwa wanasimamia nini?
 
CCM: 265/327=81%
CHADEMA:53/327=16%
CHAKACHUA FORUM: 9/327= 3%

UKIZOEA KULA NYAMA YA MTU UTAENDELEA KULA HADI MWISHO:By Mwl.Nyerere. CCM wamezoea vya kunyonga AIBU YAO AIBU YETU???? AIBU YAOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOO
 
Kura zimetimia kwa mgawanyiko wa 265,53 na 9 na kufanya 327, asilimia ndo iligomba.

au unataka kusema asilimia ndo correct na kura ndo zimekosewa?

Tatizo kubwa la waandishi wa habari wa Tanzania ni kufanya utafiti b4 hawajaandika. Ndio maana wamekuwa wanatoa habari ambazo sometimes ni only 10% correct. Hatari iliyopo ni kuwa wanamisslead waTZ sana
 
Tanzania kila kitu kinawezekana. Hata bunge lililopita walichakachua mswada wa sheria za matumizi katika uchaguzi na wote wakakubali chenga hilo kasoro Dr Slaa.
Hii inahitaji umakini.
 
Jana (12/11/2010) wakati akitangaza matokeo ya uchaguzi wa Spika, Katibu wa Bunge Dr. Thomas Kashililah alisema kuwa Anne Makinda alipata kura 265 kati ya kura 327 zilizopigwa. Aliutaja ushindi huu wa Anne Makinda kuwa ni asilimia 74.2 ya kura zote. Naona hapa Katibu wa Bunge aliteleza au alipigwa chenga kidogo na hesabu za asilimia. Kwa kura alizopata Anne Makinda ki-asilimia ni 81.04 na si asilimia 74.2 kama alivyoutangazia umma wa Watanzania na dunia. Vinginevyo atuambie kuwa kura alizopata mama Anne Makinda ni 242.5 na wala si 265. Mbaya zaidi vyombo vyetu vingi vya habari vimeendelea kutaja hizo asilimia 74.2 badala ya kugundua kwamba kuna kasoro katika kile alichokitangaza Katibu wa Bunge


Gregory Teu alikuwa mbali naye?
 
Du! JF Wakati mwingine Mnanishangaza.

Mmefanya consideration ya kura zilizoharibika?
 
Jana (12/11/2010) wakati akitangaza matokeo ya uchaguzi wa Spika, Katibu wa Bunge Dr. Thomas Kashililah alisema kuwa Anne Makinda alipata kura 265 kati ya kura 327 zilizopigwa. Aliutaja ushindi huu wa Anne Makinda kuwa ni asilimia 74.2 ya kura zote. Naona hapa Katibu wa Bunge aliteleza au alipigwa chenga kidogo na hesabu za asilimia. Kwa kura alizopata Anne Makinda ki-asilimia ni 81.04 na si asilimia 74.2 kama alivyoutangazia umma wa Watanzania na dunia. Vinginevyo atuambie kuwa kura alizopata mama Anne Makinda ni 242.5 na wala si 265. Mbaya zaidi vyombo vyetu vingi vya habari vimeendelea kutaja hizo asilimia 74.2 badala ya kugundua kwamba kuna kasoro katika kile alichokitangaza Katibu wa Bunge

Ahsante niliona hiyo pia jana pale katibu wa Bunge alipotangaza matokeo.
Anne kura (265 x 100)/ 327=81.03%
Marando (53 x 100)/327=16.2%
Zilizoharibika (9 x 100 )/327=2.8%
 
Hawa watu wamezoea kuchakachua, ni aibu kubwa kwa watu wa ngazi nzito kama ile kukosea namna hii. Nafikiri Mungu ameamua kuwaumbua na kuweka makosa yao peupe. Something very serious is hidden behind this!!
Hata matokeo ya kura za Uraisi hesabu zake hazieleweki. Ukijumlisha kura walizopata wagombea pamoja na zilizoharibika unapata waliopiga kura ni 8,626,303 lakini tume ya uchaguzi ilitangaza kuwa waliopiga kura ni 8,626,283. Hapo kuna tofauti ya kura 20, kuthibitisha kuwa matokeo hayo ni ya kupikwa au KUCHAKACHULIWA.
Mwenyekiti wa NEC alianza kwa kutoa takwimu zifuatazo:
Waliojiandikisha: 20,137,303
Waliopiga kura: 8,626,283 sawa 42.64% (ukifanya hesabu utapata 42.84%)
Kura zilizoharibika: 227,889
Kura halali zilzopigwa: 8,398,394

KUGA PETER MZIRAY
APPT - MAENDELEO
96,933
1.12%
KIKWETE JAKAYA MRISHO
CCM
5,276,827
61.17%
SLAA WILLIBROD PETER
CHADEMA
2,271,941
26.34%
LIPUMBA IBRAHIM HARUNA
CUF
695,667
8.06%
RUNGWE HASHIM SPUNDA
NCCR-MAGEUZI
26,388
0.31%
MGAYWA MUTTAMWEGA BHATT
TLP
17,482
0.20%
DOVUTWA YAHMI NASSORO DOVUTWA
UPDP
13,176
0.15%
SPOILT VOTES

227,889
2.64%
TOTALS

8,626,303
100.00%


Hii ni sehemu tu ya kasoro kibao zilizojitokeza kwenye mchakato mzima wa uchaguzi. Hivi NEC watatueleza nini? Wanadai eti wanatumia teknolojia mpya ya computer!!! Computer gani hizi haziwezi hata kufanya hesabu za kujumlisha na kutafuta asilimia. Mbona hata mtoto wa darasa la nne angeweza kujumlisha na kutoa majibu sahihi tena kwa kichwa bila hata msaada wa calculator?

NEC bila hata aibu wanadiriki kutamka hadharani eti kwamba wataalam wa kutumia kompyuta ni wachache nchi hii. Nakubali nchi hii ina wataalam wachache katika maeneo mengi lakini hatujafikia kukosa watu wa kufanya entries za kitoto kama hizo kwenye computer au kushindwa kufanya hesabu hizo za kujumlisha.
 
Mnawaonea! Mdahalo bubu wa JK alikiri kwamba hakupenda hesabu shuleni (sijui alifauluje uchumi). Mnategemeaje wajue hesabu wakati hazifundishwi tena mashuleni tz? Halafu zoezi lile la uchaguzi bungeni halikufadiliwa na wawekezaji, Tena kanuni za bunge haziruhusu consultants waingie ukumbi wa bunge.

Msiwaonee kabisa!
 
Ni hatari sana sana. Matokeo ya urais yalikosewa, tukanyamaza. Matokeo ya uspika yamekosewa tumenyamaza. Mungu atuepushie uozo huu
 
Hali ya ukosefu wa umakini hapa nchini inasikitisha sana. Ni aibu sana kuona kuwa Katibu wa Bunge tena mwenye PhD anafanya makosa kama hayo na bado amekaa kimya bila kufanya masahihisho na kuuomba radhi umma wa Watanzania na Wabunge.

Kwa upande mwingine kama mchangiaji mmoja alivyosema kuhusu uidhaifu wetu katika Hisabati hali inasikitisha sana. Ukiangalia takwimu zinaonyesha kuwa wastani wa asilimia 82.8 ya watoto wetu wanaofanya mtihani wa kumaliza darasa la saba hufeli somo la Hisabati lakini karibu asilimia 40 huchaguliwa kuendelea na masomo ya Sekondari. Hatujui matokeo ya mwaka huu yatakuaje. Kwa ngazi ya kidato cha nne hali nayo ni mbaya sana tu, kwani zaidi ya asilimia 75 ya wanafunzi wanaofanya mtihani wa kumaliza kidato cha nne hupata F katika Hisabati.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom