Katibu Mkuu wa UVCCM apata mapokezi ya kihistoria Mbinga, avunja kijiwe cha CHADEMA

the horse

JF-Expert Member
Sep 27, 2011
652
441
Katibumkuu wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM)Taifa Ndugu Sixtus Mapunda amepata makubwa wilayani Mbinga yaliyoachagumzo kubwa wilayani hapo. Mapunda ambaye alitoke wilaya ya Nyasaamepokelewa kwa kishindo kikubwa na viongozi wa CCM pamoja na mamiaya wananchi wa wilaya ya Mbinga ambako ndipo alikozaliwa.

Mapundaameingia Mbinga jana akitokea wilaya ya Nyasa ambapo ni muendelezo waziara yake ya siku tano (5) Mkoani Ruvuma. Ziara ambayo inalengakukagua na kuhamasisha ujenzi na uimara wa jumuiya mkoani humo pamojana kusimamia utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha mapinduzi ya mwaka2010-2015.

Katika hotuba yakeKatibu Mkuu amewataka wananchi wa Mbinga kujitokeza kwa wingi nakuwachagua wagombea wanaotokana na Chama Cha Mapinduzi katikauchaguzi wa Serikali za mitaa unaotegemewa kufanyika mapema mweziujao pamoja na uchaguzi Mkuu utakaofanyika mwishoni mwa mwaka 2015.

Pia Katibu Mkuu,Mapunda amemtembelea Mzee Constantine O. Millinga mmoja wa waasisikumi na watano (15) walioanzisha Chama Cha Ukombozi cha TANUwakiongozwa na Marehemu Baba wa Taifa Mwalimu Julius KambarageNyerere, mnamo tarehe 7.7 1954. Mzee Millinga ni miongoni mwa wawilikati ya waasisi hao ambao wako hai mpaka hivi sasa.

Mapunda ametoa witokwaWatanzania, wananchama wa Chama Cha Mapinduzi na hasa Vijana waTaifa hili, kuwaenzi na kuwatembelea wazee ambao ni waasisi,wazalendo wa kweli na wapigania uhuru wa nchi hii, ambao wametuwekeamisingi ya Umoja na Utaifa ambayo imeifanya Tanzania kuwa nchi yaamani na utulivu.

Katibu Mkuu huyo waUVCCM anaendelea na ziara yake Mkoani Ruvuma ambapo atatembeleawilaya ya Namtumbo na baadae Songea Mjini ambako atahutubia mkutanomkubwa wa hadhara katika wilaya hiyo ambayo ni makao makuu ya Mkoa waRuvuma.
attachment.php

attachment.php
 

Attachments

  • 10253914_742044062537178_1342623994266714427_n.jpg
    10253914_742044062537178_1342623994266714427_n.jpg
    45.5 KB · Views: 2,072
  • 11408_742046725870245_2183110387755377799_n.jpg
    11408_742046725870245_2183110387755377799_n.jpg
    52.7 KB · Views: 581
  • mapunda.jpg
    mapunda.jpg
    60.7 KB · Views: 2,182
  • 10616255_742006742540910_7821578982643513671_n.jpg
    10616255_742006742540910_7821578982643513671_n.jpg
    79.5 KB · Views: 586
Picha kama hizi na tafiti ya TWAWEZA kwanini Dr Slaa asidondoshe chozi hadharani.

0sisahau kuwalipa sh 2000 hao wamama mliowapandisha kwenye Malori mkawacha walalamike kama wakule kigoma, Hao ma driver wa bodaboda nimeongea nao ujira wao wa 15000 Muwalipe pia.. Hiyo ndio kidumu chama cha Mafisadi
 
chama cha kilaghai, badilisheni mbinu za kuwadanganya watu mlizo nazo zisha fulia
 
Ma-escrow mnatumia nguvu kuuubwa, kamsafara kenyewe kaduchu tu hako, tena hao waliowengi ni kwa sababu mmewaahidi nauli na pilau vinginevyo msingepata watu kabisa... UKAWA TUMAINI LETU!
 
Ma-escrow mnatumia nguvu kuuubwa, kamsafara kenyewe kaduchu tu hako, tena hao waliowengi ni kwa sababu mmewaahidi nauli na pilau vinginevyo msingepata watu kabisa... UKAWA TUMAINI LETU!
UKAWA ndio kitu gani.,watu wamechoshwa na uhuni na story za kutengeneza..,wameamua kurudi katika njia sahihi na njia ya sawasawa ya CCM.
 
0sisahau kuwalipa sh 2000 hao wamama mliowapandisha kwenye Malori mkawacha walalamike kama wakule kigoma, Hao ma driver wa bodaboda nimeongea nao ujira wao wa 15000 Muwalipe pia.. Hiyo ndio kidumu chama cha Mafisadi
Hii ni UVCCM yenye kutoa matumaini mapya kwa vijana, yenye kuimarisha na kuhimiza ukuaji wa uchumi kwa vijana. Jumuiya ambayo inasaidia na kuunganisha vijana nchi nzima.,inayopaza sauti za vijana na kuwasemea katika mamlaka yaliyo juu.
 
Hii ni UVCCM yenye kutoa matumaini mapya kwa vijana, yenye kuimarisha na kuhimiza ukuaji wa uchumi kwa vijana. Jumuiya ambayo inasaidia na kuunganisha vijana nchi nzima.,inayopaza sauti za vijana na kuwasemea katika mamlaka yaliyo juu.
Hii ambayo kiongozi wake mkuu ni Sadifa ( mzee wa matusi ) ?
 
Naona kuna magari makubwa ya kusomba watu.

swissme;
Kuliko hayo yakosekane ni heri wakuu wale nyasi pesa ipatikane kulipia hayo magari ya kusomba watu. Tatizo kuubwa ni kwamba hayo magari tikiti yake ni njia moja tu yaani kupelekwa mkutanoni, mkutano unaisha usiku, hivyo wanalala uwanjani, madarasani na unajua wakina nyapee wengi huzaliwa huko hukoooo. CCM kaazi ipo, vijisenti vya BMK tayari ameanza kujitanua navyooooo. Ptuuuuu
 
Kijana kusomeshwa na wazazi halafu kuja kufanya hii kazi ya kufukia uchafu unaofanywa na wakubwa zako ni sawa na kumtukana mzazi wako, hivi unawezaje kupigia debe ccm na kuwadanganya wananchi na uongo wa kazi nzuri za ccm wasizo ziona? Wakati huu kushabikia ccm lazima uwe na matatizo ya akili, kama sio chizi, basi mtindio wa ubongo unakuhusu.
 
Back
Top Bottom