Katibu Mkuu wa CHADEMA: Tunasema tuzae bila kikomo, kuzaa ni jambo jema, hakuna anayepinga kuzaana lakini tuzae kwa mpango

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Mar 9, 2015
14,243
34,899
MASHINJI.jpg


Tunasema tuzae bila kikomo, kuzaa ni jambo jema, hakuna anayepinga kuzaana lakini tuzae kwa mpango, mpangop wa taifa umeelekeza zitengwe fedha kwa ajili ya kutoa elimu ya uzazi wa mpango ili tupate taifa la wazalishaji kwa maendeleo ya taifa hili

Kila ongezeko la watoto linasababisha kuongezeka kwa msongamano darasani, tamko la kuzaana bila kikomo limetolewa Simiyu mkoa ambao watu wake wanazaliana kuliko eneo lolote nchini, ni mkoa uliyo na wananchi wengi wasiojua kusoma na kuandika

Hivi ni nani kati yenu alikwenda kufundishwa jinsi ya kuweka mimba kwa mwanamke au kupokea mimba kutoka kwa mwanamme?

Tusipowafundisha hawa watoto tutegemee ongezeko la mimba za utotoni, Ni jukumu letu kuendelea kuwafundisha kuhusu uzazi wa mpango kwa ajili ya maeneleo ya taifa letu

Kwa mwanamme ni rahisi sana kusema abebe mimba tu, lakini mwanamke anafahamu kichefuchefu anachokipata, madhara wakati wa kujifungua, wanaume wote tunaowajali wanawake tuungane kuhakikisha tunaimarisha uzazi wa mpango na kupeleka wake zetu kliniki

Nyie mnataka wake zetu wawe wanakufa tu hospitalini kwa sababu mnaweza kuoa wake wengine? Hii haikubaliki

Msimamo wa Chadema ni kwamba, watoto wote katika Taifa hili wenye umri wa kwenda shule wapelekwe bila kujali jinsia wala jinsi yake

Tunaambiwa hawa mabinti waliopewa mimba wasirudi shule kusoma, kama unazuia uzazi wa mpango unadhani wataachaje kupata mimba?

Wananchi hivi sasa badala ya kuona kiza, sasa wanapaswa kuwasha mshumaa kuleta nuru

Itakua ni fedheha na aibu kwa mtumishi kukaa na Ilani katika utekelezaji wa maendeleo, ni aibu kubwa

Katika ziara ya Rais tumeshuhudia viongozi wakiwekwa ndani bila sababu za msingi, viongozi wanakaripiwa hii haileti taswira nzuri katika Taifa na hata kwa kiongozi

Taasisi ya urais inapwaya na kama haipwai basi Rais anazungumza maoni yake ambayo sisi wananchi hatuyahitaji, huwezi kumpangia mtu utaratibu wa kuishi

Sio swala la Ng'ombe kuzaa wala kuwa na chakula, kila ongezeko la watu ambalo halina kwenye mpango linaweza kusababisha ongezeko la hali mbaya ya maisha

Ifike wakati tuanze kufungiana "Speed Govener" kiongozi wa nchi anapoanza kuzungumza mawazo yake binafsi tena yasiyokubalika inaleta ukakasi mkubwa katika nchi

"Kuna tatizo la mimba za utotoni, mfano kule alikokuwa anahutubia kuna mabinti wadogo na ukiwaangalia utadhani wana umri mkubwa sasa asipopata elimu ya uzazi tunatengeneza nini?"

Dk. Mashinji amesema, kwa wanaume wanaojali na wanaume wote Tanzania niwaombe tushikane kwa pamoja kuimarisha afya ya uzazi na tuwapeleke wake zetu tukapate elimu ya uzazi wa mpango kwa maendeleo yetu

"Waliopata kadhia katika ziara ya Rais, waelewe ndio hali ya mawasiliano katika Taifa letu na badala ya kulalamika gizani sasa wawashe mshumaa kwenye giza"

Kuhusu suala la CHADEMA kujiimarisha kwa kutumia CUF Zanzibar kama alivyosema Mwenyekiti wa Baraza la Wazee Hashim Juma Issa Dk. Mashinji amesema kama chama bado hawajajadili suala hilo huenda ni matamanio ya wanachama
 
Yani ndugu Huyu katulia press conference kuzungumzia Hilo tu
Dah tunahitaji nguvu ya ziada
 
Sijui niliangalia vibaya ??? Hi nilichoona ni sahihi ?? Eti kwenye Clip ya Mkulu akiponda uzazi wa mpango yule mwanamke anayecheka sana ni Ummy Mwalimu ( Waziri wa Afya)????
 
Sijui niliangalia vibaya ??? Hi nilichoona ni sahihi ?? Eti kwenye Clip ya Mkulu akiponda uzazi wa mpango yule mwanamke anayecheka sana ni Ummy Mwalimu ( Waziri wa Afya)????
sina uhakika lakini kama ni yeye ni aibu, kwanza alitakiwa kesho yake baada ya ile kauli angekuja tena na kuirekebisha angalau aipooze lakini mpaka sasa ni kimya, sijui kama kazaa hata mtoto mmoja!
 
Mashinji amezungumza kama msomi aliyeiva kwenye taaluma yake
Budget yenyewe iliyopo haitutoshi Watanzania tuliopo bado tunataka kuongeza watanzania wengine matokeo yake tunakuwa na watoto wa mitaani wengi bila idadi,ni aibu kubwa sana kwa kiongozi wa serikali kuzungumza vitu kama hivyo!
 
Anasema siku zote kuwa ansema ukweli. Labda tuulize swali hapa ukweli ni nini. What is Truth? Truth is according to who or what? Falsafa inatuambia what is true today might turn into false tomorrow. Labda according to GOD!
 
Sijui niliangalia vibaya ??? Hi nilichoona ni sahihi ?? Eti kwenye Clip ya Mkulu akiponda uzazi wa mpango yule mwanamke anayecheka sana ni Ummy Mwalimu ( Waziri wa Afya)????
Yaani Ummy alishangilia kabisa, mi nikashangaa kabisa. Kheri kuongozwa na kipofu kuliko kichaa!
 
Tatizo mm naona kama hamjamuelewa Mh. Rais ila kadri mtakavyozidi kukuna vichwa mtamuelewa tuu wala msitokwe na mapovu buree
 
Ukiwa na ng'ombe,maziwa yapo,unafanya kazi,nguvu za kuzaa unazo na unauwezo mpango wa uzazi unakusaidia nn? Nendeni mkaijaze dunia,naomba mtii maandiko
 
Back
Top Bottom