Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,633
- 697,791
Baada ya kumsiikiliza Gwajima katika hotuba yake hapo jana. Nimeshangazwa na habari aliyozungumza kuwa yeye ndiye aliyeweka walinzi wake kumlimda Dr. Slaa nyumbani kwake.
Kama habari hii inaukweli basi kuna tatizo kubwa sana CHADEMA. CHADEMA ni chama cha siasa ambacho kina watu kutoka imani tofauti. Huyu kiongozi wa kanisa anawezaje kuhurusiwa na chama kumwekea Katibu mkuu walinzi wake?
Tunaambiwa tuna red brigade, sasa kazi yao ni nini kama hawawezi hata kumlinda Katibu Mkuu na badala yake anawekewa walinzi na kiongozi wa dini?.
Huyu mlinzi aliyewekwa na kanisa anaripoti kwa Gwajima au kwenye Chama. Hii habari sio njema na inabidi uongozi wa CHADEMA ujitafakari katika hili.
Yaani hiki chama ni sheedah, ndo maana sioni kama kuna waislamu wengi watakipigia kura! Chadema wamejidhihirisha kabisa ni chama cha kidini
Chadema Chama cha hovyo kuwahi kutokea Tanzania.
Wanafanya mambo hovyo hovyo.
Hivi kanisa lina walinzi? Hivi unajua makubaliano yao yalikuwa ni yapi? Hivi ulijaribu kuwasiliana na CHADEMA na kupata kauli yao kabla hujakurupuka kukimbilia JF kupost hiki kiroja na kupata support ya hawa wenye mawazo mgando kama yako?