Stuxnet
JF-Expert Member
- Feb 12, 2011
- 10,339
- 17,862
Joel NANAUKA ndiyo nani? Hii siyo mada ya kuwa Jukwaa La Siasa. Lapda iende Jamii picturesKATIBU MKUU WA CCM TAIFA CDE DANIEL CHONGOLO AFANYA MAZUNGUMZO MAALUMU NA JOEL NANAUKA, DODOMA.
28.03.2022
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Cde Daniel Chongolo, Leo amekutana na Ndg Joel Nanauka na kufanya naye mazungumzo katika ofisi Kuu za CCM jijini Dodoma.
Katika mazungumzo hayo wamejadiliana mambo mbalimbali ikiwemo mchango wa Ndg Nanauka katika program mbalimbali za uimarishaji wa chama kwa ujumla na program maalumu zinazohusu vijana.
Ndg Joel Nanauka , alimpongeza Katibu Mkuu kwa kazi kubwa anayofanya na alimhakikishia kuwa yuko tayari kuendelea kutoa mchango wake kwa chama kuanzia ngazi ya Taifa hadi chini kabisa Kama ambavyo amekuwa akifanya siku zote.
Ndg Nanauka ambaye ni balozi wa Mtwara, alitumia nafasi hiyo pia kuwasilisha mambo mbalimbali ya kisekta yenye manufaa kwa mkoa wa Mtwara.
Baada ya Mazungumzo, Ndg Nanauka alimkabidhi Katibu Mkuu Zawadi ya baadhi ya Vitabu alivyoandika na kumtakia kila la Kheri katika mkutano Mkuu maalumu wa CCM Taifa unaofanyika tarehe 01.04.2022.
@joelnanauka_
Mtwara Online Tv
Habari Kiganjani Kwako