Katibu Mkuu wa CCM, Dkt. Bashiru kumuagiza RC Morogoro kufuatilia ubadhirifu ujenzi wa kituo cha afya ni sawa kimamlaka?

The Sheriff

JF-Expert Member
Oct 10, 2019
603
1,760
Hivi juzi pale mkoani Morogoro, wakati Katibu Mkuu wa CCM Dk. Bashiru Ally akiwa ziarani kwa siku tatu kwa ajili kukagua utekelezaji wa ilani ya chama chake, kwenye mradi wa ujenzi wa kituo cha afya Mikese, ilibainika uwepo wa ujenzi wa jengo jingine la mapokezi linalojengwa kwa fedha za fidia ya SGR kufuatia kubomolewa kwa zahanati ya Mikese kupisha ujenzi wa reli ya mwendokasi, ujenzi ambao haujalingana na thamani ya fedha iliyotolewa.

Dk. Bashiru Ally alimuagiza Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Loata Ole Sanare kufanya uchunguzi wa kina ili kubaini gharama halisi iliyotumiwa na Kampuni ya Reli ya Mwendokasi (SGR) kwenye ujenzi wa kituo cha afya Mikese kutokana na uwepo wa ubadhirifu wa milioni 300.

Je, Katibu Mkuu wa chama ana mamlaka ya kumtuma, kumwamuru, kumuamrisha RC suala hilo?
 
Popote anaposimama RC au DC anasimama kama kamisaa wa chama na kwa nafasi hiyo kiongozi wa chama ana mamlaka ya kumuagiza na maagizo yake yakatekelezwa kama RC.

Katibu mkuu yupo sahihi na mamlaka hayo anayo kufanya hivyo kwa makamisaa wa chama.

Hata ingekuwa Rais sio mwenyekiti, angeagizwa na mwenyekiti angetekeleza.
 
Hivi juzi pale mkoani Morogoro, wakati Katibu Mkuu wa CCM Dk. Bashiru Ally akiwa ziarani kwa siku tatu kwa ajili kukagua utekelezaji wa ilani ya chama chake, kwenye mradi wa ujenzi wa kituo cha afya Mikese, ilibainika uwepo wa ujenzi wa jengo jingine la mapokezi linalojengwa kwa fedha za fidia ya SGR kufuatia kubomolewa kwa zahanati ya Mikese kupisha ujenzi wa reli ya mwendokasi, ujenzi ambao haujalingana na thamani ya fedha iliyotolewa.

Dk. Bashiru Ally alimuagiza Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Loata Ole Sanare kufanya uchunguzi wa kina ili kubaini gharama halisi iliyotumiwa na Kampuni ya Reli ya Mwendokasi (SGR) kwenye ujenzi wa kituo cha afya Mikese kutokana na uwepo wa ubadhirifu wa milioni 300.

Je, Katibu Mkuu wa chama ana mamlaka ya kumtuma, kumwamuru, kumuamrisha RC suala hilo?
Hapo hata mm nakubali. TRC ni wapigaji sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Popote anaposimama RC au DC anasimama kama kamisaa wa chama na kwa nafasi hiyo kiongozi wa chama ana mamlaka ya kumuagiza na maagizo yake yakatekelezwa kama RC.

Katibu mkuu yupo sahihi na mamlaka hayo anayo kufanya hivyo kwa makamisaa wa chama.

Hata ingekuwa Rais sio mwenyekiti, angeagizwa na mwenyekiti angetekeleza.
Nasema haya maneno ya jukwaani sio taratibu wala miongozi, mkuu wanmkoa ni serikali sio chama. Kutofuata kwa sheria na katiba na miongozo ya kazi shida yake ni umbwe la uongozi na kauli za kijinga kama hizi.
 
Katibu wa chama, RC na DC wote wanapiga debe tu hawana check number kwenye payroll ya Serikali. Mkurugenzi yupo anawachora tu.
 
Hivi juzi pale mkoani Morogoro, wakati Katibu Mkuu wa CCM Dk. Bashiru Ally akiwa ziarani kwa siku tatu kwa ajili kukagua utekelezaji wa ilani ya chama chake, kwenye mradi wa ujenzi wa kituo cha afya Mikese, ilibainika uwepo wa ujenzi wa jengo jingine la mapokezi linalojengwa kwa fedha za fidia ya SGR kufuatia kubomolewa kwa zahanati ya Mikese kupisha ujenzi wa reli ya mwendokasi, ujenzi ambao haujalingana na thamani ya fedha iliyotolewa.

Dk. Bashiru Ally alimuagiza Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Loata Ole Sanare kufanya uchunguzi wa kina ili kubaini gharama halisi iliyotumiwa na Kampuni ya Reli ya Mwendokasi (SGR) kwenye ujenzi wa kituo cha afya Mikese kutokana na uwepo wa ubadhirifu wa milioni 300.

Je, Katibu Mkuu wa chama ana mamlaka ya kumtuma, kumwamuru, kumuamrisha RC suala hilo?
Wanaotekeleza au kusimamia utekelezaji wa ilani ya chama ni WATENDAJI, bosi wao ni MTENDAJI MKUU WA HICHO CHAMA CHENYE ILANI ambaye ni Bashiru. Kwahiyo anaweza hata waelekeza mawaziri na Majaliwa akiwemo.Ndo maana Majaliwa huwasilisha taarifa ya utendaji wa mawaziri kwenye chama.

Magu atakumbukwa kwa mengi muda wake ukiisha, pamoja na kufundisha watu siasa bila kukusudia. Mwenendo wa utendaji wake umetufuza wengi muundo wa serikali ulivyo a umuhimu wa chama cha siasa na ilani. Wengi wetu tulikuwa hatujatafakari hasa uhusiano wa serikali na chama baada ya uchaguzi. Nguvu ya chama na ilani / usimamizi wa ilani na watendaji umejitokeza hadharani zaidi kipindi hiki.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom