Katibu Mkuu wa CCM, Dk. Bashiru Ally akiri wazi kuwa CCM bado kuna maovu: Adai Makundi ya Uchaguzi bado yanaendelea.

Mgambilwa ni mntu

JF-Expert Member
May 30, 2017
2,869
3,188
IMG_7115.JPG


Katibu Mkuu wa CCM, Dk. Bashiru Ally, akiongea jijini Dodoma jana wakati wa kufunga Kikao cha Baraza la Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT), amewaonya Makada wa Chama hicho walioanza mbio za kusaka urais, akisema Chama hicho hakitamvumilia kiongozi yeyote kutumia muda, rasilimali za Serikali kwa lengo la kusaka na kuendesha makundi ndani ya Chama hicho.

Tuna Chama kimoja na Rais mmoja, kusaka urais kabla ya muda huko ni kujishushia sifa. Kila mmoja jina lake tunalo, kipindi kikifika tutasema wapi walipokutana na muda ukifika tuta-print na tutawaonyesha."

Dk. Bashiru alikumbushia maneno aliyoyasema pia akiwa huko Zanzibar hivi karibuni wakati alipokwenda kujitambulisha: "Cheo hiki (urais) ni cha watu wote, si mtu kujipitisha. Urais si wa mapambo ni sifa na ikumbukwe kuwa mtu anayefaa kuwa Rais anaombwa."

Vilevile, Bashiru aliongelea juu ya uwepo wa makundi ndani ya Chama na kukiri kuwa hali si shwari kwani kuna viashiria vya makundi. Alisema kuwa, Ndani ya CCM kuna maovu yanayoendelea na yaliyokuwa yakifanyika na kusababisha makundi. Maovu hayo ni:
  • Makundi ya Uchaguzi.
  • Kutosimsmia Muungano.
  • Utovu wa nidhamu.
  • Kukosekana kwa umoja ndani ya Chama na (kati ya) Viongozi wa Chama na Serikali.
Onyo hilo la Bashiru dhidi ya Makada wanaojipitisha pitisha huku wakitumia rasilimali za Serikali, linaonyesha wazi kuwa kuna hofu kubwa ndani ya CCM kwa baadhi ya Makada wake walioko serikalini kuwa wako hatarini kupotezwa kisiasa hasa katika ndoto zao za kuwania urais, endapo hawatafanya kitu cha kujionyesha mbele za watu.

Hali ya Watia nia wa kuwania urais mwaka 2015 ya ku-keep "low profile" inawezekana haijawasaidia the way walivyotaka kwani kila kukicha, equilibrium inazidi kuwatupa mkono na now they feel as if they keep being marginalized every how and then.

Cha ajabu Watia nia wengi wa mwaka 2015, wame-struggle kiutendaji katika Serikali ya Awamu ya Tano, licha ya baadhi yao kuwa katika nafasi za kuwafanya waonekane. Hali hiyo imetoa room ya kuibuka kwa Makada wengine wapya ambao waliojaza vacuum ya utii (kwa Rais) na ya kiutendaji iliyoonyeshwa na baadhi ya Watia nia wa 2015.

Hivyo, kwa hofu ya kupotezwa kisiasa na Siasa za Awamu ya Tano, Makada hao ndio maana wameanza mapema kuunda mitandao yao mapema.

Ni akina nani walengwa hapa wanaotumia rasilimali za Serikali kusaka urais?

IMG_7115.JPG
IMG_7119.JPG
 
Ndani ya CCM kuna maovu yanayoendelea na yaliyokuwa yakifanyika na kusababisha makundi. Maovu hayo ni:
  • Makundi ya Uchaguzi.
  • Kutosimsmia Muungano.
  • Utovu wa nidhamu.
  • Kukosekana kwa umoja ndani ya Chama na (kati ya) Viongozi wa Chama na Serikali.
CCM mnauweza Unafki..Makundi Haya yakiwa Upande wa Chadema analaumiwa Mwenyekiti..ila Upande wenu Mnajieleza tofauti..
Sasa Huyu Mwenyekiti ameshindwa kuleta Umoja kwenye Chama ataweza Kwenye Nchi?
 
Makundi yatazidi kuwepo CCM haiwezekani Leo MTU anajiuzuru upinzani anaingia CCM na siku hiyohiyo amapewa nafasi ya kugombea ubunge/udiwani ili hali sisi makada wa chama tupo.haiwezekani
 
Katika hali isiyo ya kawaida jana katika mitaa ya kinondoni hasa mitaa ya Ufipa(makao makuu ya wauza madawa ya kulevya) kumesikika miziki na watu wakinywa pombe sana huku wakishangilia taarifa ya Makonda kukemewa na rais kuhusu suala la makontena.

Wauza madawa hawa wanaona muda wa Makonda kuondoka Dares salaam umefika hivyo kuwaachia uhuru wa kufanya biashara yao bila kubanwa.

Ikumbukwe tu kuwa biashara ya madawa ya kulevya haiathiri Makonda wala familia yake ,hao hao mnaoshangilia watoto wenu na ndiyo watatumia hayo madawa na kuwa vibaka wa kuja kuwaibia huko na wengine watakuja kuwa mazezeta.




Sent using Jamii Forums mobile app
 
Katika hali isiyo ya kawaida jana katika mitaa ya kinondoni hasa mitaa ya Ufipa(makao makuu ya wauza madawa ya kulevya) kumesikika miziki na watu wakinywa pombe sana huku wakishangilia taarifa ya Makonda kukemewa na rais kuhusu suala la makontena.

Wauza madawa hawa wanaona muda wa Makonda kuondoka Dares salaam umefika hivyo kuwaachia uhuru wa kufanya biashara yao bila kubanwa.

Ikumbukwe tu kuwa biashara ya madawa ya kulevya haiathiri Makonda wala familia yake ,hao hao mnaoshangilia watoto wenu na ndiyo watatumia hayo madawa na kuwa vibaka wa kuja kuwaibia huko na wengine watakuja kuwa mazezeta.




Sent using Jamii Forums mobile app
HATA WEWE BIASHARA YA MADAWA IMEKUATHIRI MUDA MWINGI SANA MKUU MAANA WAVUTA SIGARA WENGI NI MARAFIKI ZAKO
 
Katika hali isiyo ya kawaida jana katika mitaa ya kinondoni hasa mitaa ya Ufipa(makao makuu ya wauza madawa ya kulevya) kumesikika miziki na watu wakinywa pombe sana huku wakishangilia taarifa ya Makonda kukemewa na rais kuhusu suala la makontena.

Wauza madawa hawa wanaona muda wa Makonda kuondoka Dares salaam umefika hivyo kuwaachia uhuru wa kufanya biashara yao bila kubanwa.

Ikumbukwe tu kuwa biashara ya madawa ya kulevya haiathiri Makonda wala familia yake ,hao hao mnaoshangilia watoto wenu na ndiyo watatumia hayo madawa na kuwa vibaka wa kuja kuwaibia huko na wengine watakuja kuwa mazezeta.




Sent using Jamii Forums mobile app
Kama huna akili kabisa zilizosalia azima kwa jirani yako! Halafu kuwa na adabu na heshima. Huwezi kutuita watu wote tunaoishi na kufanya biashara zetu manyanya kinondoni kuwa tunauza ngada na tunashangilia kuonyana kwa viongozi wenu!
Kama unamfanyia kazi huyo mgawa sofa jipange vinginevyo ibada ya jumapili lazima ije na ujumbe! Kama vipi jiunge na musiba ah waitara!
 
Katika hali isiyo ya kawaida jana katika mitaa ya kinondoni hasa mitaa ya Ufipa(makao makuu ya wauza madawa ya kulevya) kumesikika miziki na watu wakinywa pombe sana huku wakishangilia taarifa ya Makonda kukemewa na rais kuhusu suala la makontena.

Wauza madawa hawa wanaona muda wa Makonda kuondoka Dares salaam umefika hivyo kuwaachia uhuru wa kufanya biashara yao bila kubanwa.

Ikumbukwe tu kuwa biashara ya madawa ya kulevya haiathiri Makonda wala familia yake ,hao hao mnaoshangilia watoto wenu na ndiyo watatumia hayo madawa na kuwa vibaka wa kuja kuwaibia huko na wengine watakuja kuwa mazezeta.




Sent using Jamii Forums mobile app


Bashite upo? Kajitetee kwa mkulu achana na watu wa Ufipa sio waliozua makontena..
 
CCM mnauweza Unafki..Makundi Haya yakiwa Upande wa Chadema analaumiwa Mwenyekiti..ila Upande wenu Mnajieleza tofauti..
Sasa Huyu Mwenyekiti ameshindwa kuleta Umoja kwenye Chama ataweza Kwenye Nchi?
Ccm chama. Chadema NGO ya mtu. Kwa hiyo ccm watakisema chama. Kwa upande wa Chadema atasemwa mwenye NGO, mwenyekiti!
 
Hii ni approach nzuri ya kutatua tatizo, kuliweka wazi na kulitafutia suluhu.

2020 bado ni mbali 2025 pia.
 
kama kweli CCM ina maovu inanikumbusha msemo usemao "Kweli taulo la Gest halikaushi maji mwilini!" ikimaanisha, papuchi ya kahaba haikati kiu!
 
Ni Nape M, haa X
Ni January M, X
Ni Mwigulu N, X
Ni Mahiga A, X
Ni Muhongo S, X
Ni Makame M, X
Ni Mwinyi H, X
Ni Karume A, X

Ni mmoja miongoni mwa hao, kaaaaaazi kwelikweli . Karibu Katibu Mkuu umetoka Darasani Kwenye Siasa za Nadharia sasa umeingia kwenye Siasa na Propaganda zenyewe, karibu sana bado yapo mengi yanakuja.
 
Ccm chama. Chadema NGO ya mtu. Kwa hiyo ccm watakisema chama. Kwa upande wa Chadema atasemwa mwenye NGO, mwenyekiti!

Ccm ni chama ama kikundi cha kijeshi kinachopata nguvu kupitia idara za usalama wa nchi kama tiss, jeshi la polisi nk?
 
Ccm chama. Chadema NGO ya mtu. Kwa hiyo ccm watakisema chama. Kwa upande wa Chadema atasemwa mwenye NGO, mwenyekiti!
Kiuhalisia haiko hivyo Mkuu..haya ni Mawazo yako tu..Msajili wa Vyama anatambua Chadema kama chama cha Siasa.
 
Back
Top Bottom