Mwanahabari Huru
JF-Expert Member
- Mar 9, 2015
- 14,243
- 34,899
Kiongozi lazima awe na maono, hasa mwenye nafasi ya juu kama Rais. Fikra zake lazima ziwe pana na asiishi kama karani.
Binti mwanafunzi kapata mimba ya utotoni anaondolewa shule. Anaenda kujifungua na kuleta Mtanzania mwingine/wengine. Anaambiwa hawezi kusoma tena labda aende VETA, na huko VETA hawakusaili kama huna cheti walau cha form 4!
Binti ana opt kuwa mama lishe ili alee mtoto, huku mzazi mwenzie akiwa jela miaka 30! Pamoja na Karama zote ambazo Mwenyezi Mungu kamjalia...hapo ndo mwisho wake!
Kwangu mimi, kauli ya Rais kuhusu Mimba kwa Wanafunzi ni sawa na "hukumu ya kifo kwa kosa la wizi wa kuku"
Tusimwangalie huyu binti katika umri wake wa miaka 16, 17 mpaka 22 anapopata mimba bali tumwangalie kwa ukamilifu wake mpaka kwenye "Life Expectancy yake ambayo ni miaka 62 kwa Tanzania"
Kwa kumzuia kwenda shule haumkomoi yeye na wala hauzuii mchezo huu kwani zaidi ya 70% ya Watanzania wanaishi vijijini na 39% wapo katika umaskini uliokithiri. Hawajui maana na Elimu na umuhimu wake. Hivyo tuna kazi ya kufanya watambue kwanza maana ya Elimu.
Mheshimiwa Rais atakuwa shahidi wa maisha ya kijijini na hata umuhimu wa Elimu. Isingekuwa Elimu asingeweza hata kuwa Mwalimu wa Kemia na pia anajua maisha yalivyo magumu kijijini. Hebu tuwe binadamu kidogo na kuwawezesha hawa mabinti ili watoe mchango wa maendeleo kwa Taifa.
Bado naamini kupata Elimu ni Haki ya kila mmoja wetu na hata kama ni mfungwa!
Binti mwanafunzi kapata mimba ya utotoni anaondolewa shule. Anaenda kujifungua na kuleta Mtanzania mwingine/wengine. Anaambiwa hawezi kusoma tena labda aende VETA, na huko VETA hawakusaili kama huna cheti walau cha form 4!
Binti ana opt kuwa mama lishe ili alee mtoto, huku mzazi mwenzie akiwa jela miaka 30! Pamoja na Karama zote ambazo Mwenyezi Mungu kamjalia...hapo ndo mwisho wake!
Kwangu mimi, kauli ya Rais kuhusu Mimba kwa Wanafunzi ni sawa na "hukumu ya kifo kwa kosa la wizi wa kuku"
Tusimwangalie huyu binti katika umri wake wa miaka 16, 17 mpaka 22 anapopata mimba bali tumwangalie kwa ukamilifu wake mpaka kwenye "Life Expectancy yake ambayo ni miaka 62 kwa Tanzania"
Kwa kumzuia kwenda shule haumkomoi yeye na wala hauzuii mchezo huu kwani zaidi ya 70% ya Watanzania wanaishi vijijini na 39% wapo katika umaskini uliokithiri. Hawajui maana na Elimu na umuhimu wake. Hivyo tuna kazi ya kufanya watambue kwanza maana ya Elimu.
Mheshimiwa Rais atakuwa shahidi wa maisha ya kijijini na hata umuhimu wa Elimu. Isingekuwa Elimu asingeweza hata kuwa Mwalimu wa Kemia na pia anajua maisha yalivyo magumu kijijini. Hebu tuwe binadamu kidogo na kuwawezesha hawa mabinti ili watoe mchango wa maendeleo kwa Taifa.
Bado naamini kupata Elimu ni Haki ya kila mmoja wetu na hata kama ni mfungwa!