Katibu Mkuu CHADEMA asante kwa kuwatambua nakukaribisha maoni kwa Wananchi

Paf

JF-Expert Member
May 25, 2021
1,703
3,304
Hapa nina mawazo/maoni juu ya fedha iliyochangwa na wapenda haki na demokrasia ya kweli ili ninyi muwe huru kupigania demokrasia.

PESA HIYO IWE KWENYE MOJA YA;
1. Kujenga ofisi ya kisasa makao Makuu(CHADEMA HQ)

2. Uwepo mpango wa kujenga Chuo kukuza taaluma ya demokrasia ya chama ikiwa nisehemu ya kumbukumbu ya upambanaji
(CHUO CHA DEMOKRASIA MAENDELEO)

3. Zifunguliwe akaunt za kanda zote, fedha igawanywe kwenye kanda na wanachama wachangie kwenye mfuko huo.

NB! Ramani za majengo ya ofisi za kanda ziwe aina moja

Kwakuwa Intelijensia inaonesha kutambua HAKI/DEMOKRASIA nchini kwa sasa;
Kila kanda iunde kamati ndogo ya harambee mbalimbali nchini kwa ajili ya ujenzi wa ofisi za kanda.

HAYO NI MAONI YANGU,
Maoni yako je?
 
Ushauri mzuri sana. Wajenge ofisi zao za wilaya na mikoa
 
Kwa kuwa fedha zilichangwa na wananchi bila kujali itikadi napendekeza Baraza kuu lipange matumizi Bora ya fedha hizo au la kila mchangiaji arudishiwe fedha zake
 
Nashauri CHADEMA waitumie hela hiyo kujenga kitu cha kutumika na uma, mfano zahanati kama 2 au 3 zitumike kwa manufaa ya wananchi maana hata wachangiaji walikuwa wananchi. SIASA NI MAENDELEO
 
Mpeni mbowe zote maana anamtukuna mtu aliyetangulia mbele za haki kila iitwayo Leo kuwa kafilisi biashara zake
 
Back
Top Bottom